Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g92 10/8 kur. 16-17
  • Ni Nani Huwafunza Kuhusu Ngono?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nani Huwafunza Kuhusu Ngono?
  • Amkeni!—1992
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Yale Yanayofunzwa Shuleni
  • ‘Nitanunua Kitabu’
  • Ilinde Familia Yako Dhidi ya Mavutano Yaletayo Uharibifu
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Jinsi ya Kuwafundisha Watoto Kumhusu Mungu—Ni Njia Gani Zinazofaa Zaidi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Wazazi Walindeni Salama Watoto Wenu!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Watoto Wetu Ni Urithi Wenye Thamani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1992
g92 10/8 kur. 16-17

Ni Nani Huwafunza Kuhusu Ngono?

NI FURAHA iliyoje inayoletwa na kitoto kilichozaliwa! Wazazi hukishangilia, hucheza nacho, na kuwaambia marafiki wao karibu kila kitu ambacho kitoto hicho kinatenda. Lakini upesi wanaanza kutambua pia kwamba kinawaletea madaraka makubwa mapya. Lenye maana kati ya hayo ni uhitaji wa kukifunza kujilinda katika ulimwengu unaoendelea kukosa maadili.

Wazazi wanaweza kusaidiaje mtoto kipenzi akue na kuwa mtu mzima atakayeonea shangwe maisha ya familia yenye uchangamfu na furaha na labda kulea watoto wake mwenyewe wenye kumhofu Mungu? Wazazi wengine huenda wakaona hiyo kuwa kazi kubwa mno inayokaribia kupita uwezo wao, kwa hiyo madokezo fulani bila shaka yatathaminiwa nao.

Inaelekea kwamba unafunza watoto wako kwa njia ileile uliyofunzwa na wazazi wako. Lakini wazazi wengi walifunzwa mambo machache sana kuhusu ngono, iwapo walifunzwa lolote. Hata ikiwa ulifunzwa vema, ulimwengu umebadilika, na ndivyo na mahitaji ya watoto. Isitoshe, wasomaji wengi wa gazeti hili wametumia viwango vya juu zaidi na njia bora zaidi ya maisha. Hivyo, unapaswa ujiulize: ‘Je! njia ninayofunza watoto wangu inapatana na maoni yangu ya sasa na mahitaji yanayoongezeka ya watoto wangu?’

Wazazi wengine huwaruhusu watoto wao wajifunze habari hiyo wao wenyewe. Lakini kufanya hivyo kunazusha maswali yenye kutia wasiwasi: Wao watajifunza nini? Lini? Kutoka kwa nani, na katika hali zipi?

Yale Yanayofunzwa Shuleni

Wazazi wengi husema: “Eh, watajifunza hayo shuleni.” Shule nyingi hufunza kuhusu ngono, lakini ni chache zinazofunza kuhusu maadili. Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Elimu katika U.S. William J. Bennett alisema katika 1987 kwamba shule “hazipendi kupambanua hali za maadili.”

Tom, baba ya binti wazuri wawili, aliuliza mwakilishi wa shule yao: “Kwa nini hamsemi tu kwamba ni vibaya kufanya ngono nje ya ndoa?” Mwanamke huyo alisema kwamba angependa kusema hivyo lakini shule yake haiwezi kuwakosea mama wasioolewa wa watoto hao kutia na wanaume-rafiki wanaoishi pamoja nao. Hivyo, shule zitawaambia wanafunzi kwamba wana mambo ya kuchagua lakini mara nyingi hawasemi ni chaguo gani linalofaa.

‘Nitanunua Kitabu’

Huenda wazazi wengine wakasema: “Nitawanunulia kitabu.” Labda kitabu kizuri chaweza kusaidia, lakini unapaswa ukichunguze kwa makini sana uhakikishe kwamba unakubaliana na yale kisemayo. Ni vitabu vichache vinavyohusu habari hii vinavyoshughulikia maadili au hata kutaja yanayofaa na yasiyofaa. Baadhi yavyo hasa hupendekeza mazoea ya ukosefu wa adili. Ni mara chache sana utapata kitabu kinachosema kwamba ngono inapaswa kufanywa tu katika ndoa.

Kwa hiyo, daraka la kufunza watoto maadili huwa pale Mungu alipoliweka mwanzoni—juu ya wazazi wao wenye upendo. Biblia iliwaambia akina baba: “Nawe uwafundishe watoto wako [sheria za Mungu] kwa bidii, na kuyanena, uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo.”—Kumbukumbu la Torati 6:7.

Kwa kweli, wazazi waweza kuwa walimu bora zaidi wa watoto wao. Hakuna kitabu wala shule inayoweza kamwe kuchukua mahali pa uwezo wao wa kusadikisha au mfano bora wa familia. Kama vile William Bennett alivyosema: “Uchunguzi mbalimbali unaonyesha kwamba wakati wazazi wanapokuwa chanzo kikuu cha mafunzo ya ngono, haielekei kwamba watoto watafanya ngono. . . . Wazazi, kuliko mtu mwingine yeyote, ndio hufanyiza tofauti.”

Hata hivyo, wazazi wengine wanahofia kwamba maarifa huenda yakaongoza kwenye kujaribia. Hilo kwa wazi hutegemea kwa kiwango kikubwa juu ya yale yanayofunzwa na jinsi yanavyofunzwa. Jinsi mambo yalivyo hasa ni kwamba ni lazima vijana watajifunza kuhusu ngono. Je! si afadhali zaidi kwao kujifunza kwa njia inayofaa na yenye staha kutoka kwa wazazi wenye maadili na upendo kuliko kutoka kwa mtu mwingine mtaani au katika kiwanja shuleni au kutoka kwa watu wazima wenye akili chafu?

Lakini swali linabaki: Wewe waweza kufunzaje mambo hayo kwa njia yenye kumhofu Mungu na ya heshima? Vijana wanaposikia kwamba “kila mtu anaifanya [ngono],” unaweza kuwasadikishaje kwamba watu wema na wenye furaha zaidi hawaifanyi? Unaweza kuwasaidiaje wang’amue kwamba kuishi kwa kufuata sheria za Biblia ‘kuepukana na uasherati’ kunaongoza kwenye maisha bora na yenye furaha zaidi na pia ndiyo njia pekee inayompendeza Mungu? Makala zinazofuata zitadokeza majibu yenye thamani kwa maswali hayo ya maana.—1 Wathesalonike 4:3.

[Blabu katika ukurasa wa 16]

“Kanuni ambazo wazazi hufunza watoto wao bado zinaonekana kuwa ndizo za maana zaidi.”—U.S. News & World Report

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki