Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g92 12/8 kur. 28-30
  • Kustahi Wanawake Kundini

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kustahi Wanawake Kundini
  • Amkeni!—1992
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi Gani “Chombo Kisicho na Nguvu”?
  • Ni Nini Linalohitajiwa ili Kuwe na Badiliko?
  • Kile “Chombo Dhaifu Zaidi”—Je, Ni Kuvunjia Wanawake Heshima?
    Amkeni!—1994
  • Mwongozo Wenye Hekima kwa Wenzi wa Ndoa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Kuonyesha Upendo na Staha Ukiwa Mume
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Mwanamume na Mwanamke Wana Wajibu Wenye Kuheshimika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1992
g92 12/8 kur. 28-30

Kustahi Wanawake Kundini

BIBLIA huwawekea Wakristo mfuatano wa ukichwa wa kitherokrasi, Kristo akijitiisha kwa Mungu, mwanamume akijitiisha kwa Kristo, na mwanamke akijitiisha kwa mwanamume. (1 Wakorintho 11:3) Hata hivyo, ujitiisho huo haumaanishi kupiga ubwana. Ukichwa katika familia hautokezwi kwa jeuri, iwe ya kimwili, kiakili, au ya maneno. Zaidi ya hilo, ukichwa wa Kikristo ni wa kadiri na haumaanishi kwamba mume aweza kuwa mwonezi ajionaye kuwa asiyeweza kukosa.a Kujua jinsi na wakati wa kusema “Nasikitika, ulikuwa sahihi” kungeweza kusaidia ndoa nyingi ziwe zenye kuburudisha na zenye kudumu pia. Lakini, jinsi ilivyo rahisi kwa maneno hayo yenye unyenyekevu kukwama kooni!—Wakolosai 3:12-14, 18.

Katika shauri lao la ndoa, mitume Wakristo Paulo na Petro huturudisha daima kwa mfano wa Kristo. Staha hupatikana kwa sababu ya mfano wa mume wenye kuburudisha anapoiga kiolezo alichoweka Kristo, kwa kuwa “mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa [kundi, NW], naye ni mwokozi wa mwili.”—Waefeso 5:23.

Shauri la Petro kwa waume ni dhahiri: “Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili [kulingana na maarifa, NW]” (1 Petro 3:7) Tafsiri ya kisasa ya Kihispania hufafanua mawazo hayo ikisema: “Kuwahusu waume: onyesheni, busara katika maisha mnayoshiriki, mkimfikiria mke.” Maelezo hayo yaonyesha mambo mengi, kutia ndani hisia nyepesi katika uhusiano wa ndoa. Mume hapaswi kumwona mkeye kuwa chombo tu cha kujitosheleza ngono. Mke mmoja aliyetendwa vibaya akiwa mtoto aliandika: “Natamani tu mngesema zaidi juu ya tegemezo ambalo mume anaweza kumpa mke aliyepatwa na jambo hilo. Jambo ambalo wengi wetu tunahitaji kujua tukiwa wake ni kwamba tunapendwa kikweli na kutunzwa, si kwamba tupo hapo tu ili kutosheleza tamaa fulani za kimwili au kuwa mtunza nyumba, pasipo uhusiano wowote wa kihisiamoyo.”b Ndoa ilianzishwa na Mungu ili waume na wake waweze kuwa washiriki na wasaidizi wa mmoja na mwenzake. Ni jambo la kusaidiana na kustahiana.—Mwanzo 2:18; Mithali 31:28, 29.

Jinsi Gani “Chombo Kisicho na Nguvu”?

Petro pia awashauri waume wawape wake staha “kama chombo kisicho na nguvu.” (1 Petro 3:7) Petro alimaanisha nini kwa kusema kwamba mwanamke ni “chombo kisicho na nguvu”? Kwa hakika, kwa wastani, mwanamke ni mdhaifu kimwili kuliko mwanamume. Tofauti za muundo wa mifupa na misuli husababisha hilo. Lakini tukiongea juu ya nguvu za ndani za adili, basi mwanamke si mdhaifu hata kidogo kuliko mwanamume. Kwa miaka mingi wanawake wamevumilia hali ambazo labda wanaume wengi hawangeweza kuvumilia hata kwa muda mfupi—kutia ndani kutendwa vibaya na mwenzi wa ndoa mjeuri au mlevi. Na ebu fikiria juu ya yale ambayo mwanamke huvumilia ili azae mtoto, kutia ndani saa nyingi za maumivu ya uzazi wakati wa kuzaa! Mume yeyote mwenye huruma ambaye ameshuhudia mwujiza wa kuzaa lazima awe na staha nyingi zaidi kwa mke wake na nguvu zake za ndani.

Kuhusu jambo la nguvu za adili, Hannah Levy-Haas, mfungwa Myahudi wa kambi ya mateso ya Nazi ya Ravensbrück aliandika hivi katika kitabu chake cha matukio katika 1944: “Jambo moja hapa linaloniudhi sana, ni hilo la kuona kwamba wanaume ni wadhaifu zaidi ya wanawake na hawawezi kuvumilia magumu kadiri wanawake wanavyovumilia—kimwili na mara nyingi kiadili pia. Wasiweze kujidhibiti wenyewe, wanaonyesha ukosefu mkubwa sana wa nguvu za adili hivi kwamba mtu hana la kufanya ila kuwasikitikia.”—Mothers in the Fatherland, cha Claudia Koonz.

Jambo hilo latoa kielelezo cha kwamba hakuna msingi wowote wa kubagua wanawake kwa kuwa tu huenda wakawa wadhaifu kimwili. Edwin Reischauer aliandika: “Katika nyakati za kisasa, inakubalika kwa ujumla kwamba wanawake wana nguvu nyingi zaidi ya nia na ya kiakili kuliko wanaume.” (The Japanese) Nguvu hiyo yaweza kutumiwa katika kundi la Kikristo wakati ambapo wanawake waliokomaa wanaweza kuwasaidia wanawake wengine ambao wamepatwa na mkazo mkubwa wa kihisiamoyo. Kwa hakika, katika hali nyingine ni rahisi zaidi kwa mwanamke ambaye ametendwa vibaya kumwendea mwanamke aliyekomaa ili apate kitulizo cha mara moja kuliko kumwendea mwanamume. Uhitaji ukitokea, mzee Mkristo aweza kuendewa ili mwongozo zaidi upatikane.—1 Timotheo 5:9, 10; Yakobo 5:14, 15.

Kule kukisia tu kwamba maitikio ya wanawake ni ya kihisiamoyo, na kuyahesabia kuwa “ule wakati wa mwezi” huudhi wanawake wengi sana. Betty Mkristo mtendaji, alisema: “Tunajua, kama alivyoandika mtume Petro, kwamba katika mambo fulani sisi ni ‘chombo kisicho na nguvu’ yaani, yule wa kike, tumeumbwa tukiwa na miili dhaifu. Lakini hiyo haimaanishi kwamba mkubwa au msimamizi wa kazi apaswa kujiona na kudhibiti mambo akifikiria kila itikio la mwanamke husababishwa na kawaida yetu ya hedhi. Sisi ni weledi na tunataka kusikilizwa kwa staha.”

Si wanawake wote huwa wepesi kuonyesha hisia, kama vile si wanaume wote wasioonyesha hisia kwa urahisi. Kila mtu anapasa kuchukuliwa akiwa mtu binafsi. Betty, aliyetajwa mbeleni, aliambia Amkeni! hivi: “Sipendi kuwekwa katika kikundi fulani kwa msingi wa jinsia. Nimeona wanaume wakilia na kuwa wenye kubadilika-badilika hali. Na kuna wanawake wawezao kuwa wenye moyo mgumu sana. Kwa hiyo acheni wanaume watusikilize wakiwa na kusudi bila kujali jinsia.”

Ni Nini Linalohitajiwa ili Kuwe na Badiliko?

Ikiwa hali itabadilika kuwa bora, wengine husema kwamba haitoshi kwa wanawake kupigania haki zao na usawa; wala haitoshi kwa wanaume kufanya tendo dogo tu la kuwastahi wanawake. Katika kila tamaduni na hali, ni lazima wanaume wachunguze daraka lao katika hali hiyo na kujiuliza wenyewe lile wanaloweza kufanya ili maisha yafurahishe na yawe yenye kuburudisha zaidi kwa wanawake.—Mathayo 11:28, 29.

Mwandikaji na mshairi Katha Pollitt aliandika katika Time hivi: “Bila shaka, wanaume wengi, hawalali wanawake kinguvu wala kuwapiga wala kuwaua. Lakini hilo halimaanishi, kama vile wengi wao hufikiri, kwamba hawahusiki hata kidogo na jeuri dhidi ya wanawake. Kila mmoja wetu katika maisha yetu ya kila siku husaida kurekebisha hali na maoni ya utamaduni wetu yanayofasili mipaka ya mambo yanayoruhusiwa. . . . Nazungumza juu ya wanaume kujihusisha katika kujichunguza wenyewe kwa uzito, washinde ubaguzi wao na mapendeleo yao, wakishiriki sehemu fulani ya lawama kwa matatizo tuliyo nayo.”

Lakini hata ikiwa wanaume ulimwenguni pote wanafanya badiliko kubwa katika mitazamo yao kuelekea wanawake, hilo bado halitakuwa utatuzi kamili wa ukosefu wa haki unaoipata ainabinadamu. Kwa nini? Kwa sababu wanaume wanafanya yasiyo haki na mambo ya kikatili si kwa wanawake tu bali pia kwa wanaume wenzao. Vita, jeuri, uuaji wa kimakusudi, vikundi vya kufisha, na uharamia bado ni mambo ya kawaida katika nchi nyingi. Linalohitajiwa ni mfumo mzima mpya wa kutawala dunia nzima. Na elimu mpya kwa ainabinadamu yote. Na hilo ndilo Mungu ameahidi kupitia utawala wa Ufalme wake kutoka mbinguni juu ya dunia. Ni wakati huo tu ndipo haki na usawa wa kweli utakapokuwako kwa—wanaume, wanawake na watoto wote. Ni wakati huo tu ndipo kustahiana kikweli kutakapokuwako kati ya wanaume na wanawake. Biblia hueleza hivi kwenye Isaya 54:13: “Na watoto wako wote watafundishwa na BWANA [Yehova, NW], na amani ya watoto wako itakuwa nyingi.” Ndiyo, elimu ifaayo katika kanuni za Yehova zenye uadilifu itachangia ulimwengu mpya wa kuonyeshana staha.

[Maelezo ya Chini]

a Ona “Ujitiisho Katika Ndoa Humaanisha Nini?” Mnara wa Mlinzi, Desemba 15, 1991, kurasa 19-21.

b Ona Amkeni! Oktoba 8, 1991, kurasa 3-11; Aprili 8, 1992 kurasa 24-7 (Kiingereza).

[Picha katika ukurasa wa 29]

Mara nyingi mwanamke mkomavu aweza kutoa shauri lenye kusaidia

[Picha katika ukurasa wa 30]

Kushiriki kazi za nyumbani ni njia moja ambayo mume aweza kuonyesha staha kwa mke wake

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki