Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g93 4/8 kur. 24-25
  • Je! Ni Lazima Tutimize Nadhiri Zetu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Ni Lazima Tutimize Nadhiri Zetu?
  • Amkeni!—1993
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Hakuna Kutoa Visababu
  • Uwe na Dhamiri Safi
  • Nadhiri Zisizofaa au Zisizo za Kimaandiko
  • Fikiria Nadhiri Zako za Zamani na za Wakati Ujao
  • Timiza Nadhiri Zako
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2021
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • “Kile Unachoweka Nadhiri, Timiza”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Mahubiri ya Mlimani—“Usiape Kabisa”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1993
g93 4/8 kur. 24-25

Maoni ya Biblia

Je! Ni Lazima Tutimize Nadhiri Zetu?

MUME na mke wenye furaha wakabili tatizo lenye kusumbua. Miaka iliyopita, walipokuwa na tatizo kubwa la familia, walitoa nadhiri ya kumpa Mungu sehemu ya kumi ya mapato yao ikiwa angewamalizia matatizo yao. Sasa, wakiwa na umri mkubwa zaidi na wakiwa na matatizo ya pesa yasiyotazamiwa, wanajiuliza, “Je! tunashurutika kutimiza nadhiri hiyo?”

Tatizo lao linakariri shauri la yule mwanamume mwenye hekima dhidi ya uharaka wa kusema: “Ni afadhali usiweke nadhiri, kuliko kuiweka usiiondoe [na usiitimize, NW]. Usikiache kinywa chako kuukosesha mwili wako; wala usiseme mbele ya huyo malaika ya kwamba umepitiliwa.”—Mhubiri 5:5, 6.

Hakuna Kutoa Visababu

Hata ingawa nadhiri za kipuuzi na ahadi zisizotimizwa ni za kawaida katika jamii ya kisasa inayoendekeza mambo, hatuwezi kumtazamia Mungu aamini visababu vilivyobuniwa; hata wafanyabiashara hawawezi kudanganyika. Makala “Uaminifu Katika Biashara: Maneno Yaliyo Kinyume?” katika jarida la biashara Industry Week iliomboleza: “Hatuwatumaini watu tena waseme kweli, wafanye yale yafaayo badala ya kudanganya, wafanye kulingana na makusudio yao.” Ingawa uwongo wenye kunufaisha, kama vile kusema “hundi imekwisha kupelekwa kwa njia ya posta,” huenda ukatokeza wakati wa kuwalipa wadai wa kibinadamu, malaika hawadanganyiki kamwe.

Hiyo haimaanishi kwamba Mungu hutumia malaika ili kuona kwamba nadhiri zimetimizwa kwa njia ambayo mtoa mikopo kwa riba ya juu angeweza kutumia majangili ili kupata pesa kwa riba ya juu kutoka kwa watozwaji walioshindwa kulipa. Badala yake, Mungu kwa upendo hufanya malaika zake wawe “roho watumikao [kwa kujenga], wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu.” (Waebrania 1:14) Wakiwa hivyo, malaika wanaweza na huhusika katika kujibu sala zetu za kutoka moyoni.

Hata hivyo, tukiendelea kutoa ahadi tusizotimiza katika sala zetu, je, tunaweza kwa kufaa kutazamia baraka za Mungu? Yule mwanamume mwenye hekima asema: “Kwani Mungu akukasirikie sauti yako, na kuiharibu [angalau kwa kadiri fulani] kazi ya mikono yako?”—Mhubiri 5:6b.

Hivyo, si hofu ya malaika mwenye kulipa kisasi ambayo yapaswa kutusukuma tutimize nadhiri zetu badala ya kutoa visababu. Badala yake, tunapaswa tuthamini uhusiano mzuri na Mungu na tutamani kwa unyoofu upendeleo wa Mungu katika utendaji wetu. Kama vile mume na mke waliotajwa juu walivyoeleza vizuri: “Tunataka tuwe na dha-miri safi mbele za Mungu na tutende kulingana na mapenzi yake.”

Uwe na Dhamiri Safi

Ili kuwa na dhamiri safi kuhusu kutimiza nadhiri, ni lazima tuwe wanyoofu sisi wenyewe. Kutoa kielezi: Ebu tuseme mtu fulani angekuwia kiasi kikubwa cha pesa lakini kwa sababu ya tatizo fulani anajipata kwamba hawezi kukulipa. Ni nini kingekupendeza zaidi—ikiwa angepuuza deni lote kuwa haiwezekani kukulipa au ikiwa angalau angepanga kukulipa kiasi kidogo cha kawaida kwa kadiri awezavyo?

Kwa njia iyo hiyo ya kufikiri, ebu tuseme nadhiri ya haraka ya kutoa wakati wote wa mtu au nyenzo nyinginezo kwa ajili ya utendaji ufaao wa Kikristo haiwezi kutimizwa. Je! hatupaswi kujihisi kuwa wenye jukumu kiadili kujaribu kutimiza nadhiri yetu kwa kadiri hali zetu za sasa zinavyoruhusu? “Kama nia ipo [kwanza],” akaandika Paulo, “hukubaliwa [hasa],” iwe tuna vingi vya kutoa au tuna vichache. (2 Wakorintho 8:12) Lakini namna gani kuhusu nadhiri zilizotolewa kabla ya mtu kuwa na ujuzi sahihi wa kweli ya Biblia?

Nadhiri Zisizofaa au Zisizo za Kimaandiko

Tukijifunza kwamba nadhiri si safi au si ya kiadili, tunapaswa kuiachilia kama kaa lenye moto! (2 Wakorintho 6:16-18) Mifano ya nadhiri zisizo safi ni:

□ Nadhiri zilizotolewa kwa miungu au miungu-jike bandia, kama “malkia wa mbinguni” wa Babuloni.—Yeremia 44:23, 25.

□ Nadhiri zinazovunja sheria, kama ile nadhiri ya wanaume 40 ya kutokula chakula hadi wawe wamemwua mtume Paulo.—Matendo 23:13, 14.

□ Nadhiri za uasi imani zinazofuata “mafundisho ya mashetani; kwa . . . watu wasemao uongo, . . . wakiwazuia watu wasioe, na kuwaamuru wajiepushe na vyakula, ambavyo Mungu aliviumba vipokewe kwa shukrani na walio na imani wenye kuijua hiyo kweli.”—1 Timotheo 4:1-3.

Kwa hiyo, kwa wazi, huenda tukahitaji kutangua nadhiri za zamani. Lakini kuhusu nadhiri zilizohusu mambo yasiyopinga maandiko, mbona uzitafutie makosa? Je! maarifa sahihi ya sasa tuliyo nayo hayapaswi kutufanya tuonyeshe heshima kuu zaidi kwa nadhiri zetu za zamani kuliko hapo mbeleni?

Fikiria Nadhiri Zako za Zamani na za Wakati Ujao

Pia inamaanisha kwamba tunapaswa kufikiri kwa uzito kabla ya kuongeza nadhiri zozote wakati ujao kwa ibada yetu. Nadhiri hazipaswi kutumiwa ili tu kuchochea mtu afanye au asifanye jambo fulani, kama vile kuongeza wakati atumiao mtu katika ibada ya Kikristo au kujizuia na ulafi. Hata hivyo, Yesu hakupinga viapo vyote, kama kwa mfano, inapohitajiwa katika mahakama. Lakini kwa wazi aliweka mpaka kuhusu viapo vya bila kufikiri, kwa kuwa alionya: “Mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usizuri [usiape bila kutimiza], ila mtimizie Bwana [Yehova, NW] nyapo zako; lakini mimi nawaambia, Usiape kabisa.” (Mathayo 5:33, 34) Kwa nini yeye alichukua msimamo huo? Je! nadhiri zilikuwa hazifai kuliko hapo mbeleni?

Mara nyingi viapo vya waaminifu wa nyakati za kale vilikuwa na masharti. Katika sala yenye kuhisiwa wangemwahidi Yehova, ‘Ikiwa utanisaidia nishinde tatizo hili, nitafanya hivi na hivi kwa ajili yako.’ Lakini Yesu alisema: “Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu.” Badala ya kupendekeza nadhiri zenye masharti kwa waaminifu wa siku zake, Yesu aliwahakikishia hivi: “Hata sasa hamkuomba neno kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapata.”—Yohana 16:23, 24.

Uhakika huo katika jina, au ofisi, ya Yesu wapaswa pia kumfariji yeyote ambaye bado ahisi kuwa mwenye hatia kwa sababu—ingawa anajitahidi—hawezi kutimiza yale aliyomwahidi Mungu “kwa kutamka haraka kwa midomo yake.” (Mambo ya Walawi 5:4-6) Kwa hiyo, bila kupuuza nadhiri zetu za zamani, si kwamba tu tunaweza sasa kusali katika jina la Yesu bali tunaweza pia kumsihi Mungu atumie dhabihu ya fidia ya Yesu kwa ajili ya dhambi zetu, na tunaweza kuomba msamaha katika jina la Yesu. Hivyo tunaweza kupokea “utimilifu wa imani, hali [tumetakasishwa] mioyo tuache dhamiri mbaya.”—Waebrania 10:21, 22.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 24]

Mapadri wakitoa nadhiri katika Montmartre

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki