Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g93 9/8 kur. 26-27
  • Je! Kuna Hatari Katika Kufanya Mizungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Kuna Hatari Katika Kufanya Mizungu?
  • Amkeni!—1993
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Uvutano wa Mizungu Katika Historia Yote
  • Aina Tatu za Mizungu
  • Je! Kuna Hatari kwa Wakristo?
  • Ukweli Kuhusu Uchawi na Ulozi
    Je, Umeipata Barabara Inayoongoza Kwenye Uhai wa Milele?
  • Uganga Na Uchawi Ni Mambo Mabaya
    Wewe Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
  • Unachopaswa Kujua Kuhusu Uchawi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Jitihada ya Kutafuta Kisichojulikana Kupitia Mizungu na Uwasiliani-Roho
    Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1993
g93 9/8 kur. 26-27

Maoni ya Biblia

Je! Kuna Hatari Katika Kufanya Mizungu?

‘KUNA mazingira ya mizungu. Kwa ghafula, kimya chavunjwa kwa sauti ya ngoma. Macho yote yakaziwa kwenye watu wawili waliovaa nguo zilizofanana wakibeba bunduki mrao. Wakiinua bunduki-mrao zao mabegani, wamlenga shabaha mfanya mizungu Mchina mwenye vazi lenye madoido. Anashikilia sahani ya udongo mbele ya kifua chake. Bunduki-mrao hizo zatoa ngurumo zinapofyatuliwa. Mara hiyo mfanya mizungu aanguka sakafuni, akivuja damu nyingi. Mazingaombwe ya sahani kuzuia risasi yawa msiba.’ Kasoro kwenye mashine katika mojapo bunduki mrao hizo ilisababisha risasi kutoka na kupenya kwenye kifua cha mfanya mizungu huyo. Ndivyo kitabu Henry Gordon’s World of Magic kinavyosimulia.

Ni kutumia vibaya kama nini zawadi ya uhai—yote hayo kwa sababu ya kutazamisha, misisimko, na vitumbuizo ambavyo hutokana na aina hiyo ya mizungu. Je! hivyo ndivyo wewe huitikia? Au unahisi kwamba ni sehemu tu ya hatari inayohusiana na kufanya mchezo kama huo? Hata itikio lake liwe nini, mazingaombwe haya yalipokosa kufaulu yalikuwa hatari kubwa zaidi. Inatusukuma kuuliza hivi: Je! kuna hatari yenye hila zaidi inayohusiana na zoea hili la mizungu? Ili kupata jibu, acheni tuangalie kiini cha usanii huo wa kale.

Uvutano wa Mizungu Katika Historia Yote

Tangu mwanzo wa historia, mwanadamu amechochewa na kuvutwa kwa hila na fumbo la mizungu. Neno la Kiingereza “magic” linatokana na neno “magi,” jamii ya kikuhani ya Kiajemi ya kale iliyokuwa stadi kwa utendaji wa kidhehebu. Kwa msingi wayo, mizungu ni jitihada ya kudhibiti au kulazimisha nguvu za asili au zenye kupita uwezo wa asili ili zimtumikie mwanadamu. Misri ya karne ya 18 K.W.K. iliajiri makuhani wenye kufanya-mizungu. Mizungu pia ilitimiza sehemu maarufu katika dini ya Wakaldayo wa kale wa Babeli katika karne ya nane K.W.K. (Mwanzo 41:8, 24; Isaya 47:12-14; Danieli 2:27; 4:7) Uvutano huo uliendelea miongoni mwa Wagiriki na Waroma wa kale kufikia Enzi za Kati hadi katika karne yetu ya 20.

Aina tofauti za mizungu zaweza kuwekwa katika vikundi mbalimbali. Robert A. Stebbins katika kitabu chake The Magician anaweka mizungu katika vikundi vitatu.

Aina Tatu za Mizungu

Kuna mizungu ya kifumbo “wonyesho wa nguvu zisizo za kawaida.” Hudai kwamba “matukio au miendo inayopinga akili ya kawaida au ujuzi wa kisayansi” ni “kweli au halali.” Stebbins aeleza zaidi kwamba “mizungu ya kifumbo inatokana na ulozi, . . . uchawi, kugeuza vitu kimafumbo, na chini ya hali fulani, dini.”

Kwa upande wa mizungu ya ulaghai, “wenye mizungu hiyo hufanyia hila au kutumia vibaya uwezo wa kuona uhalisi wa watazamaji kwa sababu ya ukuu wao wenyewe.” Wanajua kwamba wanadanganya umma, lakini kulingana na Stebbins, “wanatia moyo wale wanaoshuhudia mizingu waamini vingine—waamini kwamba, wakiwa wanamizungu, wana uwezo usio wa kawaida au wana uhusiano wa kipekee na viumbe na uwezo huo.”

Mizungu ya kutumbuiza hulenga kutia mshangao kwa uwongo wenye kuvutia. Hivyo huwa katika namna tano za msingi: “mizungu ya jukwaani, mizungu inayofanywa karibu na watazamaji, mbinu za kutumia mikono, mauzauza, na kusoma akili.”

Je! Kuna Hatari kwa Wakristo?

Acheni kwanza tuchunguze mizungu ya kifumbo. Mizungu ya kifumbo huletwa kwa njia mbalimbali. Kwa mfano, waabudu Shetani wako wanaozoea mizungu “myeusi” na “myeupe” pia. Mizungu “myeusi” hutia ndani kufanya ulozi, laana za pekee, kijicho ili kudhuru maadui wa mtu. Mizungu “myeupe,” kwa upande mwingine, inakusudiwa kuleta matokeo mazuri kwa kuvunja ulozi na kuondoa laana. Hata hivyo, yote hiyo ni maonyesho ya nguvu zisizo za kawaida au ya kifumbo. Kwa pindi fulani mizungu ya kifumbo hata hutumiwa ili kujaribu kupata mavuno mazuri au kushinda mashindano ya michezo. Ingawa hivyo, kuhusu aina hii ya mizungu ya kiroho, Biblia husema waziwazi hivi: ‘wala msifanye ulozi, wala kutumia utambuzi [mizungu, NW].’—Mambo ya Walawi 19:26; Kumbukumbu la Torati 18:9-14; Matendo 19:18, 19.

Hatari inajibanza wapi katika mizungu yenye ulaghai? Wenye kusoma viganja vya mkono, wabashiri, na waponyaji wa imani, kwa kutaja wachache tu, hutumia mizungu yenye ulaghai ili kuendeleza mapendezi yao wenyewe. Je! wao hawaendelezi uwongo katika kazi yao? Neno la Mungu husema hivi: “Msidanganye, wala msiambiane uongo.”—Mambo ya Walawi 19:11.

The Encyclopedia Americana yasema: “Katika visa fulani, matendo ya mizungu yaweza kutumika kukaribisha roho.” Je! twataka kualika matatizo kutoka kwa roho za mashetani kwa kujihusisha kwa njia isiyo ya moja kwa moja katika ulimwengu huo? Mashetani wakipewa fursa, wanaweza na watatutumia sisi vibaya. Wao hutafuta ‘wakati ufaao’ na ni wakatili kwa jitihada zao.—Luka 4:13; Yakobo 1:14.

Mkuu wa ufundi wa kudanganya na mauzauza si mwingine ila Shetani Ibilisi. Amekuwa akizoea ufundi huo tangu alipofanya hivyo mbele ya mwanadamu katika shamba la Edeni. (Mwanzo 3:1-19) Ni Mkristo gani ambaye angependa kuwa kama yeye? Badala ya hivyo, Wakristo wanashauriwa ‘wamwige Mungu’ na ‘wamtii Mungu, na wampinge Shetani.’—Waefeso 5:1, NW; Yakobo 4:7.

Hata hivyo, watu wengi, huhusianisha neno “mizungu” na vitumbuizo. Mtu anaweza kutokeza madanganyo na mikono yake, (kiini-macho), akijua kwamba mkono huwa mwepesi kuliko jicho. Huenda kusiwe na katazo la Biblia kuhusu jambo hili. Hata hivyo, ikiwa kuna ujanja wa mizungu ya nguvu zisizo za kawaida, je, Mkristo angetaka kuonekana kuwa mwenye uwezo fulani usio wa kawaida, uwezo usioelezeka? Au ikiwa wengine wanaona ubaya wa michezo ya “mizungu,” je, Mkristo hatataka kuepuka vitumbuizo kama hivyo ili asikwaze wengine? (1 Wakorintho 10:29, 31-33) Kuongezea hilo, kuna hatari yenye nguvu ya mtu kushawishiwa kuendelea zaidi katika kazi za kindani za mizungu.

Kwa hiyo, kwa habari ya mizungu ambayo kwa wazi inahusiana na uwasiliani-roho, Wakristo wa kweli huepuka kwa hekima kuifanya. Zaidi ya hilo, katika kila sehemu ya maisha ya Mkristo—iwe inatia ndani kuajiriwa, tafrija, au vitumbuizo—atataka ‘kuwa na dhamiri njema,’ dhamiri isiyomletea Mungu au mwanadamu suto.—1 Petro 3:16; Matendo 24:16.

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 26]

The Bettmann Archive

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki