Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g95 1/8 kur. 19-21
  • Naweza Kunyooshaje Maisha Yangu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Naweza Kunyooshaje Maisha Yangu?
  • Amkeni!—1995
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mwana Mwasi Aondoka Nyumbani
  • ‘Alirudiwa na Fahamu Zake’
  • Kunyoosha Mambo Pamoja na Mungu
  • Fanyia Miguu Yako Mapito Manyoofu
  • “Yehova, Mungu Mwenye Rehema na Neema”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Unaweza Kumsaidiaje Mtoto “Mpotevu”?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Kupokea kwa Uchangamshi Wale Wanaorudi
    Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya
  • ‘Mrudieni Mchungaji wa Nafsi Zenu’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1995
g95 1/8 kur. 19-21

Vijana Huuliza. . .

Naweza Kunyooshaje Maisha Yangu?

“SINGEWEZA kamwe kwenda ndani,” akasema John. Alijikuta akisimama nje ya Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova. Akiwa tineja alikuwa ameacha Ukristo na kufuatia maisha ya uhalifu, dawa za kulevya, na ukosefu wa maadili ya ngono. Baada ya miaka ya kuishi hivyo, bado hangeweza kuiondoa Biblia akilini mwake, kwa hiyo akaenda kwenye Jumba la Ufalme—lakini aliogopa mno kuingia. “Wewe huelewi,” akamwambia mtu fulani aliyemtia moyo kwenda ndani. “Nimefanya mengi mno. Sihisi kwamba Yehova aweza kwa vyovyote kunisamehe kwa yale ambayo nimefanya.”

Vijana wasiohesabika huasi dhidi ya sheria za wazazi, dini, na maadili. Hasa ni jambo la kushtua na lenye msiba wakati vijana waliolelewa na wazazi wahofu-Mungu wafanyapo hivi. Ingawa wengi kiasi wamefuata njia hiyo, baada ya muda, wengine wao huanza kuhisi hisia yenye kuwasumbua ya utupu ambao hata mtindo-maisha wa shamrashamra hauwezi kuuziba. (Mithali 14:13) Vijana fulani, wakiisha kuunguzwa na ulimwengu mwovu huu, hutaka kunyoosha maisha zao na kurudia kweli za Biblia walizojifunza wakiwa watoto. Lakini je, kweli yawezekana kwao kufanya hivyo?

Mwana Mwasi Aondoka Nyumbani

Mfano wa Yesu wa mwana mpotevu, au mtapanyaji, upatikanao kwenye Luka 15:11-32 (NW) watokeza ufahamu mwingi wa ndani juu ya jambo hili. Usimulizi huo wasomeka hivi: “Mtu fulani alikuwa na wana wawili. Na yule kijana zaidi kati yao akamwambia baba yake, ‘Baba, nipe sehemu ya mali iliyo fungu langu.’ Ndipo yeye akawagawia njia zake za kujipatia riziki. Baadaye, baada ya siku zisizokuwa nyingi, huyo mwana aliye kijana zaidi alikusanya pamoja vitu vyote akasafiri nchi ya nje akaingia katika nchi ya mbali.”

Hakika kijana huyu hakuasi kwa sababu baba yake alikuwa mkali, mtukanaji, au mwenye sheria kali mno! Kulingana na Sheria ya Kimusa, mwana alikuwa na haki ya kupata hisa kubwa ya mali za baba yake, ingawa kwa kawaida haikuwa hivyo mpaka kifo cha baba yake. (Kumbukumbu la Torati 21:15-17) Ulikuwa usugu ulioje kudai hisa yake mapema! Hata hivyo, baba huyo alimridhia kwa upendo. (Linganisha Mwanzo 25:5, 6.) Basi, kwa wazi mtazamo wa kijana huyo wa kiume—wala si wa baba yake—ndio uliokuwa na kasoro. Kama vile mwanachuo Alfred Edersheim alivyoweka wazo hilo, yawezekana hakupendezwa na “mpangilio na nidhamu ya nyumbani kwao” na alikuwa na “tamaa ya uhuru na ufurahio” yenye ubinafsi.

Kama vile makala fulani iliyotangulia katika mfululizo huu ilivyokubali wazi, si wazazi wote walio wafadhili na wenye kufikiria.a Wakati ambapo mzazi ni mkali au asiyesababu kwa kiasi, uasi silo jibu kamwe; hatimaye huwa ni kujiangamiza mwenyewe. Fikiria, tena, mfano wa Yesu. Baada ya kusafiri mbali na nyumbani, kijana huyo wa kiume “akafuja mali yake kwa kuishi maisha ya ufasiki. Alipokuwa ametumia kila kitu, njaa kali sana ilitokea kotekote katika nchi hiyo, naye akaanza kuwa katika uhitaji.” Hata hili halikumfanya arudiwe na akili. Akiwa bado mwenye kujitumaini, “alienda na kujishikamanisha mwenyewe na mmoja wa raia wa nchi hiyo, naye akamtuma aingie katika mashamba yake ili achunge mifugo ya nguruwe. Naye alikuwa na kawaida ya kutamani kushibishwa kwa matumba ya mkarobu ambayo hao nguruwe walikuwa wakila, na hakuna yeyote aliyekuwa akimpa kitu chochote.”

Asema mwanachuo wa Biblia Herbert Lockyer: “Wayahudi wenye kumsikiliza Yesu lazima wawe walitetemeka kwa maneno haya, ‘kulisha nguruwe,’ kwa maana kwa Myahudi, hakungeweza kuwa na mshusho wa cheo uzidio huo.” Vilevile leo, wale wanaoacha kweli za Biblia hujikuta mara nyingi katika hali ngumu, au hata zenye kushusha heshima. Msichana mmoja Mkristo aliyekimbia nyumbani aungama hivi: “Fedha zangu zote zilitumika kwa dawa za kulevya, nami sikuwa na fedha zozote kwa kitu kingine chochote. Kwa hiyo nikaanza kuiba madukani kitu chochote kile ili nitegemeze mazoea yangu.”

‘Alirudiwa na Fahamu Zake’

Ingawa hivyo, mwana mpotevu aliitikiaje hali zake mwenyewe za shida kubwa? Yesu alisema kwamba mwishowe ‘alirudiwa na fahamu zake.’ Maneno ya asili ya Kigiriki humaanisha “akiisha kuja ndani yake mwenyewe.” Ndiyo kusema, alikuwa amekuwa “kando yake mwenyewe” katika ulimwengu wenye kichaa wa fantasia, akiwa amepofuka asione jinsi hali yake ilivyokuwa ya shida nyingi kwelikweli.—Linganisha 2 Timotheo 2:24-26.

Vijana fulani waasi leo wameshtuliwa hivyohivyo wakaona uhalisi wa mambo. Kuvuna majonzi yaletwayo baadaye na maisha ya ufasiki—jela, majeraha mazito, maradhi yaambukizwayo kingono—kwaweza kuwa tukio la kufanya mtu afikiri kwelikweli. Maneno ya Mithali 1:32 yaligonga maana mwishowe: “Kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua.”

Fikiria Elizabeth kijana, aliyewaacha wazazi wake na kuhusika na dawa za kulevya. “Nilisahau juu ya Yehova,” yeye asema. Hata hivyo, alipokuwa akizuru New York, alipita karibu na makao makuu ya ulimwengu ya Mashahidi wa Yehova. Tokeo? “Maumivu yalipita katika akili na moyo wangu,” akumbuka msichana huyo. “Nilikuwa nimefanya nini? Niliachaje maisha yangu yafutuke kuwa msiba mkubwa hivyo?”

Wakati yule mwana mpotevu alipoikabili kweli mwishowe, alifanya uamuzi wa moyo mkuu—kwenda nyumbani na kunyoosha maisha yake! Lakini baba yake angeitikiaje baada ya kuwa ameumizwa na kusalitiwa na mwanaye? Usimulizi wajibu hivi: “Alipokuwa angali mbali sana, baba yake alimwona mara hiyo naye akasikitika, naye akakimbia akaangukia shingo yake na kumbusu kwa wororo.” Ndiyo, kabla kijana huyo hajaweza kufanya ungamo lake lililofanyiwa mazoezi kwa uangalifu, baba yake alichukua hatua ya kwanza kuonyesha upendo na msamaha!

Kunyoosha Mambo Pamoja na Mungu

Hata hivyo, mwana mpotevu alimwambia baba yake hivi: “Nimefanya dhambi dhidi ya mbingu na dhidi yako.” Somo? Vijana ambao wameelekea kwingine kutoka kwenye njia za Mungu hawawezi kunyoosha maisha zao mpaka ‘wanyooshe mambo’ pamoja na Mungu mwenyewe! (Isaya 1:18, NW) Twaweza kuwa na shukrani kwamba Yehova hufanya upatanisho huo uwezekane. Kwa kweli, yule baba katika mfano wa Yesu ni ufananisho wa Yehova Mungu. Na Mungu huonyesha mtazamo huohuo wa kusamehe kwa kuwaambia hivi watenda-dhambi watubuo: “Nirudieni mimi, nami nitawarudia ninyi.” (Malaki 3:7; linganisha Zaburi 103:13, 14.) Lakini kama wale Wayahudi wakosaji katika nyakati za Biblia, ni lazima watu hao waazimie hivi: “Na tuchunguze njia zetu na kuzijaribu, na kumrudia BWANA [“Yehova,” NW] tena.”—Maombolezo 3:40.

Hii yamaanisha mtu apekue sana mwenendo wake wenye dhambi. Kijana mkosaji afanyapo hivi, apaswa kuhisi akisukumwa kuungama dhambi zake mbele za Yehova Mungu. Alisema hivi mtunga-zaburi: “Niliponyamaza mifupa yangu ilichakaa kwa kuugua kwangu mchana kutwa. . . . Nalikujulisha dhambi yangu, wala sikuuficha upotovu wangu. . . . Nawe ukanisamehe upotovu wa dhambi yangu.”—Zaburi 32:3-5.

Namna gani ikiwa kijana amehusika katika makosa mazito sana—labda utoaji-mimba, maisha ya ovyoovyo, utumizi mbaya wa dawa za kulevya, au uhalifu? Ni jambo lenye kueleweka kwamba huenda mtu huyo akahisi hastahiki msamaha. John, aliyetajwa mwanzoni, alihisi hivyo. Ndiyo sababu alisimama tuli nje ya Jumba la Ufalme mpaka mzee wa kutaniko mwenye fadhili akamkumbusha kwamba Mfalme Manase wa Israeli ya kale alikuwa pia amekuwa na hatia ya dhambi zilizo nzito—kutia na uuaji! Hata hivyo, Yehova alimsamehe. (2 Mambo ya Nyakati 33:1-13) “Mzee huyo aliokoa uhai wangu,” asema John. Akijua kwamba msamaha uliwezekana, John alipata moyo mkuu wa kuingia katika Jumba la Ufalme na kuomba msaada.b

Vijana walio wengi katika mashaka kama hayo wahitaji vilevile msaada wa kunyoosha mambo pamoja na Mungu, na wazee wa kutaniko la kienyeji waweza kusaidia sana katika jambo hili. Wao waweza kusikiliza kwa hisia-mwenzi na uelewevu wakati kijana ‘aungamapo dhambi zake waziwazi.’ Wao waweza pia kutoa nidhamu na msaada wenye kutumika. Kwa kielelezo, wao waweza kupangia kijana huyo awe na mtu wa ‘kumfundisha mafundisho ya kwanza’ ya Neno la Mungu kwa njia ya funzo la Biblia nyumbani. Na ikiwa mkosaji ana ugumu wa kusali, mzee aweza kufanya hivyo kwa ajili yake. “Sala ya imani itamfanya huyo asiyejisikia vizuri apone,” Biblia yatuhakikishia.—Yakobo 5:14-16, NW; Waebrania 5:12.

Fanyia Miguu Yako Mapito Manyoofu

Bila shaka, kunyoosha mambo pamoja na Mungu ni mwanzo tu. Sawa na vile mwana mpotevu alivyoomba radhi kwa baba yake, vijana wakosaji wapaswa kujaribu kutengeneza mambo na wazazi wao. Kuomba radhi kwa moyo mweupe kwaweza kusaidia sana katika kulegeza kadiri fulani ya maumivu ambayo yamewapata na katika kupata tegemezo lao. Kijana mmoja aliyetoroka na kurudi nyumbani akiwa na mtoto haramu akumbuka hivi: “Mama na baba walinionyesha upendo mwingi ajabu.”

Kijana atakaye kumfurahisha Mungu ahitaji ‘kufuliza kufanyia miguu yake mapito yaliyo manyoofu.’ (Waebrania 12:13, NW) Huenda hii ikamaanisha abadili mtindo-maisha, mazoea, na washirika wa mtu. (Zaburi 25:9; Mithali 9:6) Kuanzisha kawaida ya funzo la kibinafsi ni kwa maana pia. Msichana mmoja aliyekuwa mwasi hapo kwanza asema hivi: “Niliisoma Biblia kila siku na kusoma habari zote zenye msingi wa Biblia zilizochapishwa na Mashahidi wa Yehova. Namshukuru Mungu kwa kunipa fursa ya pili.”

John atoa vema muhtasari wa mambo, akisema: “Mimi hutazama nyuma kwenye wakati nilioupoteza. Mimi hufikiria jinsi mambo yangaliweza kuwa, lakini hakuna namna niwezayo kutangua yaliyotendeka.” Kwa kufurahisha, sisi huabudu Mungu mwenye rehema ambaye kwa uchangamfu huwaalika wale ambao wamemwacha wamrudie. Kwa nini usikubali mwaliko wake?

[Maelezo ya Chini]

a Ona “Vijana Huuliza . . . Kwa Nini Napaswa Kutii Wazazi Wangu?” katika toleo letu la Desemba 22, 1994.

b Ikiwa wewe hukulelewa ukiwa Mkristo lakini ungali waona uhitaji wa kubadili njia yako ya maisha, ziara kwenye Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova ni mwanzo mwema. Omba funzo la Biblia nyumbani bila malipo. Kwa njia hii waweza kupata usaidizi wa kibinafsi katika kunyoosha maisha yako.

[Picha katika ukurasa wa 20]

Wakristo wakomavu waweza kukusaidia unyooshe maisha yako

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki