Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g95 3/22 uku. 31
  • “Mwendee Chungu”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Mwendee Chungu”
  • Amkeni!—1995
  • Habari Zinazolingana
  • “Mwendee Chungu”
    Amkeni!—1991
  • Chungu wa Jangwani Wanaotokeza Asali Tamu
    Amkeni!—2011
  • Jeshi Lasonga Mbele!
    Amkeni!—2003
  • Chungu Wanaepukaje Msongamano Barabarani?
    Je, Ni Kazi ya Ubuni?
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1995
g95 3/22 uku. 31

“Mwendee Chungu”

“CHUNGU WASIO WA KAWAIDA”—kichwa hicho kikuu cha habari cha kigeni kilitokea miaka michache iliyopita katika makala moja ya gazeti kuhusu Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova lililojengwa kwa haraka. Ni nini kilichofanya kuwe na kichwa kikuu hicho? Si vigumu kufahamu unapotazama katika picha iliyochukuliwa kutoka angani ya mahali pa ujenzi kama hapo. Kichwa kidogo katika makala ya gazeti hilohilo kilieleza hivi: “Mashahidi wa Yehova 500 kwenye mahali pa ujenzi—kisuguu kisicho cha kawaida.”

Ulinganisho huo ni wenye uelekevu, labda zaidi ya alivyogundua ripota huyo. Ni kweli, kutoka mbali juu, mamia machache ya watu wakitembea-tembea katika mahali pa ujenzi huenda wakaonekana kama chungu juu ya kisuguu. Lakini katika kisa hiki uonekano huo ni zaidi ya kuwa wa kijuu-juu tu. Kwa nini hivyo? Mashahidi wa Yehova hufikiria kwa uzito shauri la Biblia katika Mithali 6:6, ambayo husema: “Mwendee chungu . . . zitafakari njia zake ukapate hekima.” Mtu aweza kuwaje na hekima kwa kuwatazama chungu?

Kwanza, chungu hutimiza mengi sana. Ensaiklopedia ya Biblia Insight on the Scriptures huonelea hivi: “Si utayarishaji wao kwa ajili ya wakati ujao uonekanao tu bali pia kuendelea kwao bila kukoma na azimio lao, mara nyingi wakibeba au kukokota bila kuacha vitu vilivyo na uzito ulio mara mbili uzito wao wenyewe, wakifanya chochote kiwezekanacho ili kutimiza kazi yao fulani, na kukataa kurudi nyuma hata ingawa huenda wakaanguka, kuteleza, au kubingirika chini kutoka mtelemko wa ghafula.”a

Vilevile, ingawa Mashahidi wa Yehova hawakokoti mara mbili uzito wa miili yao katika vifaa vya ujenzi, wao mara nyingi hushangaza majirani wao kwa yale wanayotimiza kwenye miradi yao ya ujenzi kwa kipindi kifupi sana. Si jambo lisilo la kawaida kuona Majumba ya Ufalme yao yakisimamishwa kutoka kwenye msingi na kumalizwa katika kipindi cha siku mbili au tatu tu!

Wao huweza kutimizaje yote haya? Kwa kuiga chungu katika jambo jingine muhimu. Insight on the Scriptures yasema hivi kuhusu chungu: “Wakishirikiana kwa njia ya kushangaza, wao huweka vichuguu vyao vikiwa safi sana, na huonyesha kujali kwa mfanya-kazi mwenzi, nyakati fulani wakisaidia chungu walioumia au waliochoka kuwarudisha kisuguuni.” Ripota aliyetajwa juu alionekana kuwa amependezwa na roho ya kushirikiana kama hiyo miongoni mwa Mashahidi, akifafanua “tokeo la jitihada lililotimizwa kwa mwelekeo wa shangwe katika hali iliyotulia na wastadi 80 hivi wakiwakilisha kila sehemu ya ujuzi wa ujenzi na kutegemezwa na wajitoleaji 400.”

Hata hivyo, kazi yote ngumu na ushirikiano ambao Mashahidi wa Yehova huweka katika kujenga kwao Majumba ya Ufalme ni mwonjo wa kimbele wa yale yatukiayo ndani ya majumba hayo katika miaka ifuatayo. Hapo wao huendelea kufanya kazi kwa bidii na kushirikiana pamoja, wakipanga kitengenezo kazi yao ya kuhubiri na kufundisha na kutoa mikutano inayojenga na yenye kuelimisha. La maana hata zaidi, wao hujitolea kuonyesha kujali kulekule kwenye upendo kwa mmoja na mwenzake ambako Yesu alionyesha wafuasi wake alipokuwa duniani.—Yohana 13:34, 35.

Ikiwa umeshapata kuona Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova na kujiuliza ni nini kiendeleacho humo, twakukaribisha kwa uchangamfu uje na ujionee mwenyewe. Twaweza kwa hakika kukuhakikishia ukaribishaji mchangamfu na ziara yenye kufundisha.

[Maelezo ya Chini]

a Kilichotangazwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc.

[Picha katika ukurasa wa 31]

Jumba la Ufalme lililojengwa kwa haraka katika Aurillac, Ufaransa

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 31]

Mchoro: Chungu wa Farao. Lydekker

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki