Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g95 6/8 kur. 15-16
  • Fasihi za Biblia Zathaminiwa Katika Ule Uliokuwa Muungano wa Sovieti

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Fasihi za Biblia Zathaminiwa Katika Ule Uliokuwa Muungano wa Sovieti
  • Amkeni!—1995
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Magazeti Yenye Urangi-Rangi Yathaminiwa
  • Fasihi Nyingine Zathaminiwa
  • Warusi Wathamini Sana Uhuru wa Kuabudu
    Amkeni!—2000
  • Watu Wanaopenda Amani Watetea Jina Lao Zuri
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Ziara ya Kurudi Urusi
    Amkeni!—1995
  • Ukuzi Wenye Kutazamisha
    Amkeni!—1992
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1995
g95 6/8 kur. 15-16

Fasihi za Biblia Zathaminiwa Katika Ule Uliokuwa Muungano wa Sovieti

Na mleta-habari wa Amkeni! katika Urusi

MAPEMA katika 1991 ule uliokuwa bado Muungano wa Sovieti ulifanyizwa kwa Urusi na jamhuri nyinginezo 14. Tangu wakati huo, hizo jamhuri zimekuja kuwa nchi zilizo huru. Hata hivyo, Urusi ina idadi kubwa zaidi kuliko zile nchi nyinginezo 14 zikiunganishwa na ina zaidi ya mara tatu eneo la bara kuliko hizo jamhuri. Kufikia Septemba 1994, kulikuwa na Mashahidi wa Yehova 117,276 katika ule uliokuwa Muungano wa Sovieti ambao walikuwa wakishiriki kweli za Biblia pamoja na jirani zao.

Leo viwango vikubwa vya magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! vinachapishwa kila mwezi kwa Kirusi kwa utumizi katika ule uliokuwa Muungano wa Sovieti. Kwa kuongezea, trakti nyingi na vitabu vilivyojalidiwa vinagawanywa huko. Kwamba fasihi hii ya Biblia imethaminiwa sana yaonekana wazi kutokana na barua zilizopokewa kwenye ofisi ya Urusi ya Mashahidi wa Yehova karibu na St. Petersburg.

Magazeti Yenye Urangi-Rangi Yathaminiwa

Mwanamume fulani kutoka Siberia ya kati aliandika hivi: “Ilikuwa bila kutazamia kabisa kwamba niliona Mnara wa Mlinzi mikononi mwa mfanyakazi mwenzangu. Nilimwomba anionyeshe. Kwanza nilitazama picha nyangavu tu zenye rangi kamili. Halafu nikasoma zaidi na zaidi . . . Kabla nitambue, nilikuwa nimesoma gazeti hilo kutoka jalada hadi jalada. Maswali yaliulizwa katika njia yenye kupendeza, yenye kuchangamsha, na ya namna ya mazungumzo.”

Mwanamume mwingine kutoka Siberia alieleza hivi: “Kwa tukio la ghafula nilipokea toleo la gazeti lenu. Sitaki kuwasifu bure, lakini hii ni habari bora zaidi ya zote ambayo nimepata kusoma kuhusu imani.”

Mwuguzi kutoka St. Petersburg, jiji la pili kwa ukubwa katika Urusi, aliandika hivi: “Asanteni sana kwa mfululizo wa makala katika Amkeni! la Januari 8, 1995 juu ya kuungua nishati. Makala hizi hazikuondoa matatizo yangu lakini zilinipa utegemezo ambao nilikuwa nimeungoja na kuutafuta.”

Mwanafunzi fulani mwenye umri wa miaka 17 aliandika hivi: “Ninashukuru sana wale wote wanaochapisha fasihi zenye kupendeza jinsi hiyo. Marafiki wangu nami tulipokuwa tukitoka kwenye jumba la sinema, tuliona machache ya magazeti hayo yameachwa kwenye kiti kitupu. Tuliyachukua. . . . Nilipokuwa nikisoma Mnara wa Mlinzi, singeweza kuamini macho yangu. Je, wakati ujao utakuwa hivyo kweli? Sasa ninasoma zile Gospeli na najaribu kuzielewa. Magazeti yenu hueleza vizuri mno lile Biblia husema.”

Mwanamume fulani mwenye umri wa miaka 26 alisema: “Nashukuru sana kwa makala ‘Je! Suluhisho Ni Kujiua?’ katika Amkeni! la Aprili 8, 1994. Kwa sababu ya mtazamo wangu kuelekea mshuko wa moyo na zoea la kupiga punyeto, mara nyingi sana nimefikiria ujiuaji. Lakini Neno la Mungu na sala kwa Yehova vilinizuia kumaliza uhai wangu. Makala hii iliongezea nguvu itikadi yangu katika rehema ya Mungu na itikadi yangu kwamba Mungu atanisaidia kushughulikia na kujaribu kushinda matatizo yangu. Yeye aona toba yangu. Yeye ataka niishi. Namshukuru kwa utegemezo wake uliotolewa kupitia makala hii.”

Kuhusu makala hiyohiyo ya Amkeni!, msichana mwenye umri wa miaka 15 alieleza hivi: “Gazeti hili limetimiza fungu kubwa sana maishani mwangu. Nilipokuwa na umri wa miaka minane, nilianza kuhisi kwamba hakuna aliyenihitaji. Wazazi wangu hawakuwa na wakati wa kuzungumza nami, nami nilijaribu kutatua matatizo yangu mwenyewe. Nilijitenga mwenyewe. Niligombana na watu wangu wa ukoo kwa kuendelea. Halafu wazo la ujiuaji likaja akilini mwangu. Jinsi nilivyofurahi kukutana na Mashahidi wa Yehova!”

Mwanamke fulani kutoka sehemu ya Urusi ya Ulaya alisema hivi: “Wakati mmoja nilisikia kwa mbali mazungumzo ya Biblia kati ya wanaume wachanga wawili kwenye kituo cha basi. Nilipendezwa na nikawakaribia. Wanaume hawa wachanga walinipa nakala ya Mnara wa Mlinzi. Nikiwa na furaha na upendezi, nilisoma gazeti hilo, na nataka kujua zaidi kuhusu Biblia. Ningependa kuwasiliana nanyi kupitia kwa magazeti yenu, na nataka kujua na kujifunza Biblia kwa ukawaida.”

Fasihi Nyingine Zathaminiwa

Mwanamke fulani mchanga kutoka Caucasus aliandika: “Mwanamke fulani alikuja ofisini mwetu na kuanza kutuambia juu ya aina fulani ya kusanyiko. Niliona shangwe na idili aliyokuwa nayo, na nikapendezwa. Siku iliyofuata alinipa kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Nilikisoma haraka kwa matamanio makubwa. Kilikuwa chenye kushangaza na kupendeza. Nilihisi kwamba baada ya kuzunguka-zunguka katika giza, nilikuwa nimepata mlango uongozao kwenye nuru. Baada ya kutafuta kwa muda mrefu mno, nilipata majibu kwa maswali yangu yote katika kitabu kimoja tu. Hii ni shangwe isiyoweza kufafanuliwa.”

Mwanamume fulani kutoka Asia ya Kati alionelea hivi: “Mimi ni mparishi wa Good News Church la kievanjelisti. Tuna upungufu mkubwa mno wa fasihi ya kiroho. Twawaomba kwa uharaka mtupelekee vitabu, broshua, na vijitabu kwa ajili ya funzo na ugawanyaji zaidi.”

Mtu fulani kutoka Armenia, karibu na Bahari Nyeusi, aliandika hivi: “Nilisoma broshua Je, Kweli Mungu Anatujali?, na ilikuwa kama mpumuo wa hewa safi. Hatimaye nimepata fasihi ambayo itanisaidia kujifunza Biblia. Nawaomba tafadhali mnipelekee vitabu kwa ajili ya funzo kama hilo.”

Mwanamke fulani kutoka Siberia alisema hivi: “Mmoja wa Mashahidi wa Yehova alizuru nyumbani mwetu na kuacha nakala ya kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Ingawaje nimekuwa asiyeamini kuwapo kwa Mungu tangu nilipokuwa shuleni, nilichosoma kilinitia moyo kutafakari kwa kina na kuanza kujifunza Biblia.”

Mama ya watoto wawili alionyesha shukrani zake kwa ajili ya kitabu hichohicho juu ya maisha ya Yesu Kristo na akaeleza hivi: “Kinafahamika kwa watoto na ni chenye upendezi kwao. Hicho huamsha tamaa zaidi ya kujifunza Biblia na kusoma fasihi ya kidini. Kitabu hicho kimechapishwa na kutengenezwa kwa ubora.”

Mwaka jana, watu 34,608 katika ule uliokuwa Muungano wa Sovieti walionyesha uthamini wao kwa lile walilokuwa wakijifunza kwa kubatizwa. Na fasihi za Kibiblia zinazochapishwa na Mashahidi wa Yehova zipate ugawanyaji kamili na ulio mwingi katika sehemu hii ya ulimwengu, na maelfu mengi zaidi yaitikie kweli za Biblia ambazo fasihi hizo huwa nayo!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki