Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g96 7/8 kur. 7-8
  • Kushinda Vizuizi vya Mawasiliano

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kushinda Vizuizi vya Mawasiliano
  • Amkeni!—1996
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Utofauti wa Kitamaduni Miongoni mwa Mashahidi wa Yehova
  • Vizuizi Vinavyozuia Mawasiliano
    Amkeni!—1996
  • Nimekwama Katikati ya Tamaduni Tofauti—Nifanyeje?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1
  • Je, Unawaona Wengine Kama Yehova Anavyowaona?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Utamaduni wa Wenyeji na Kanuni za Kikristo—Je, Zapatana?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1996
g96 7/8 kur. 7-8

Kushinda Vizuizi vya Mawasiliano

HATUKUCHAGUA familia au taifa ambalo tulizaliwa ndani yalo, wala hatukuamua ni utamaduni gani ungefanyiza njia yetu ya kufikiri. Hatukuwa na uwezo wowote juu ya mambo hayo. Sote hupatwa na wakati na hali. Lakini twaweza kudhibiti jinsi tunavyowaona wengine na kuwatendea.

Biblia hufafanua jinsi tuwezavyo kufanya hivyo. Fikiria kanuni chache zitakazotusaidia kuwasiliana na wale ambao huenda wanatoka katika malezi yanayotofautiana na yetu.

“Mungu aliyeufanya ulimwengu na vitu vyote vilivyomo . . . alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja, wakae juu ya uso wa nchi yote.” (Matendo 17:24, 26) Sisi sote ni washiriki wa familia ileile ya kibinadamu na basi tuna mambo mengi yanayofanana. Kutazama mambo tuliyo nayo ambayo yafanana hufanya mawasiliano yawe rahisi zaidi. Sisi sote twataka marafiki wazuri nasi twahitaji kuhisi tunapendwa na kustahiwa. Kila mtu hujaribu kuepuka maumivu ya kimwili na ya kihisia-moyo. Watu wa tamaduni zote hupenda muziki na sanaa, kusema mambo yachekeshayo, na kuamini kutendeana kwa adabu, nao hutafuta njia za kuwa na furaha.

‘Usitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, umhesabu mwenzako kuwa bora kuliko nafsi yako.’ (Wafilipi 2:3) Hili halimaanishi kwamba tuwaone wengine kuwa bora kuliko sisi kwa kila kitu. Badala ya hivyo, twapaswa kung’amua kwamba katika maeneo fulani ya maisha, wengine ni bora. Hatupaswi kamwe kufikiri kwamba ama sisi ama utamaduni wetu hufanya mambo yote vizuri kushinda wengine.

“Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema.” (Wagalatia 6:10) Kuchukua tu hatua ya kuwa mwenye urafiki na mwenye kusaidia wengine, hata wawe wa malezi gani ya kitamaduni kwaweza kusaidia sana kuziba pengo la mawasiliano.

“Hayo mnajua, ndugu zangu wapenzi. Basi kila mtu na awe mwepesi wa kusikia, bali si mwepesi wa kusema; wala kukasirika.” (Yakobo 1:19) Wawasilianaji wazuri ni lazima wafanye mengi zaidi ya kusema tu; ni lazima wawe wasikilizaji wenye hisia-mwenzi.

“Mashauri ya moyoni ni kama kilindi; lakini mtu mwenye ufahamu atayateka.” (Mithali 20:5) Uwe chonjo kufahamu hisia na masuala yanayomfanya mtu awe na tabia fulani kwa nje. Jaribu kujua watu vizuri zaidi.

“Mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.” (Wafilipi 2:4) Uwe mwenye hisia-mwenzi kwa kutazama masuala jinsi mwingine ayaonavyo. Usiwe mwenye ubinafsi.

Utofauti wa Kitamaduni Miongoni mwa Mashahidi wa Yehova

Jambo la kwamba kanuni hizo kwa kweli zinafanya kazi laonekana katika muungano wenye kustaajabisha wa Mashahidi wa Yehova, ambao wanatenda katika nchi 232 za dunia. Wao ni watu ambao wametoka “kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha” na ambao wameazimia kujipatanisha na mwongozo wenye upendo wa Yehova katika mambo yote.—Ufunuo 7:9; 1 Wakorintho 10:31-33.

Mashahidi mmoja-mmoja hawadharau utamaduni wa wengine. Wala wale wanaokuwa Mashahidi hawakatai utamaduni ambamo walilelewa, ila tu kama huo unapinga kanuni za Biblia. Katika hali kama hizo wao hufanya mabadiliko maishani mwao. Wao hutambua kwamba katika kila utamaduni kuna mambo mazuri sana na kwamba hayo hukuzwa hata zaidi katika watu wanaokubali ibada ya kweli.

Wao hujaribu kuona dunia yetu jinsi ambavyo lazima Mungu awe anaiona—yenye kung’aa na buluu na maridadi—ikizunguka angani. Ni dunia yenye watu na tamaduni tofauti-tofauti ajabu. Mashahidi wa Yehova watazamia wakati ambapo wote walio duniani watafurahia maisha wakiwa familia ambayo kikweli imeungana.

[Picha katika ukurasa wa 8]

Mashahidi wa Yehova wamejifunza kushinda vizuizi vya kitamaduni

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki