Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g98 2/22 kur. 7-9
  • Ulimwengu Usio na Uhalifu Waja Karibuni!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ulimwengu Usio na Uhalifu Waja Karibuni!
  • Amkeni!—1998
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Elimu Inayohitajika
  • Jinsi Ulimwengu Mpya Utakavyokuja
  • Ulimwengu Mpya wa Mungu U Karibu
  • Ulimwengu Usio na Uvunjaji wa Sheria—Wewe Unautaka Kiasi Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Je, Kuna Utatuzi wa Kudumu?
    Amkeni!—2003
  • Ulimwengu Huu Unaelekea Wapi?
    Amkeni!—2007
  • Wakati Ulimwengu Mpya Utakapokuja
    Amkeni!—1993
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1998
g98 2/22 kur. 7-9

Ulimwengu Usio na Uhalifu Waja Karibuni!

TUNAPOTAZAMA hali ya ulimwengu leo, inakuwa wazi kwamba ni vigumu sana kuepuka kushawishiwa kufanya lililo baya. Kwa kweli, sote huzaliwa tukiwa wasiokamilika, wenye mwelekeo wa kufanya mambo mabaya. (1 Wafalme 8:46; Ayubu 14:4; Zaburi 51:5) Na kwa vile Shetani Ibilisi ameshafukuzwa kutoka mbinguni, anafanya jitihada kubwa zaidi kupita wakati wowote ule kusababisha matata.—Ufunuo 12:7-12.

Matokeo yamekuwa mabaya sana. Uchunguzi wa watoto 4,000 katika Scotland ulionyesha, kwa kielelezo, kwamba thuluthi mbili ya wale wenye umri kati ya 11 na 15 walikuwa tayari wamefanya uhalifu. Uchunguzi uliofanywa kote katika Uingereza ulionyesha kwamba karibu kila tineja mmoja kati ya watatu hakusumbuliwa na dhamiri kuhusu wizi wa madukani. Na zaidi ya nusu walikiri kwamba ikiwa wangerudishiwa pesa nyingi baada ya kununua vitu, wangeziweka.

Kitabu cha Kiitalia Lʹoccasione e lʹuomo ladro (Nafasi na Mwizi) chatoa mwono ndani kuhusu kwa nini watu huiba. Kitabu hicho chasema kwamba wezi wana “kiasi cha chini cha kujidhibiti” na kwamba “hawawezi kuondosha upendezi wao.” Kitabu hicho chaongeza pia kwamba wezi wengi si wataalamu bali ni “wenye kutanguliza tu masilahi yao wakiwa tayari kutumia kila hali.”

Kwa kupendeza, kitabu hicho pia chachunguza kwa nini watu wengi “huepuka kuvunja sheria.” Chamalizia kwamba sababu si kuwa “wanahofu hasara zinazoletwa na kuvunja sheria bali kwa sababu wana kanuni za maadili ambazo huwazuia kufanya hivyo.” Ni wapi ambapo watu wanaweza kujifunza kanuni za maadili zinazofaa za namna hiyo?

Elimu Inayohitajika

Basi, fikiria yale ambayo watu hujifunza kutoka kwa vyanzo vingi vya uwasiliano. Mathalani, ujumbe unaowasilishwa kwa kawaida na filamu na televisheni ni kwamba ujeuri, uzinzi, na tabia ya matusi ni mambo yanayokubalika. Kwa hiyo, haishangazi, kwamba watu ni wenye kiwango cha chini cha kujidhibiti. Biblia, kwa upande mwingine, hufundisha hivi kwa hekima: “Asiye mwepesi wa hasira ni mwema kuliko shujaa; na mtu aitawalaye roho yake kuliko mtu atekaye mji.”—Mithali 16:32.

Kwa kufikiria propaganda ya leo, haipaswi kushangaza kwamba wengi ni “wasioweza kukubali kutoshelezwa.” Tena na tena, watu husikia: “Nunua sasa na ulipe baadaye.” “Uwe mwema kwako mwenyewe.” “Unastahili kilicho bora zaidi.” “Tunza masilahi au hali njema yako.” Kujitosheleza kibinafsi hutolewa kama jambo lililo la kawaida na linalofaa. Lakini mtazamo wa kibinafsi wa namna hiyo ni kinyume cha fundisho la Biblia juu ya ‘kufuliza kuangalia, si masilahi ya kibinafsi ya mambo yenu wenyewe tu, bali pia masilahi ya kibinafsi yale ya wengine.’—Wafilipi 2:4.

Je, hungekubali kwamba wengi wa wasio haki ni wenye kuangalia zaidi masilahi yao wenyewe kuliko ya wengine? Kwa kusikitisha, kuna idadi inayoongezeka ya watu ambao wako tayari kutumia hali kwa faida yao wenyewe. Hawaulizi ikiwa tendo fulani liko sawa kiadili. Hangaiko lao pekee ni, ‘Je, naweza kufanya kitendo hicho na nisishikwe?’

Ni nini linalohitajiwa? Kama ilivyoonyeshwa juu, ni kanuni za kiadili zinazohitajika. Hizi zitawazuia watu kutofanya vitendo vya uhalifu, kukosa kustahi utakatifu wa uhai, kutohalifu utakatifu wa ndoa, kutokiuka vifungo vya tabia zifaazo, na ama sivyo kuingilia haki za wengine. Wale wanaokosa kujifunza kanuni hizo, kama Biblia isemavyo, ‘wanakuwa wamekwisha kuishiwa na hisia zote za adili.’ (Waefeso 4:19) Tabia za kihalifu za watu wa namna hiyo wasiomwogopa Mungu ndizo zinazotuzuia kuonea shangwe ulimwengu usio na uhalifu.

Jinsi Ulimwengu Mpya Utakavyokuja

Bila shaka, watu wengi hujaribu wawezavyo kufuata haki, kutendea binadamu wenzao kwa staha na kwa ufikirio, na kujiepusha na vitendo vilivyo kinyume cha sheria. Lakini lingekuwa jambo la ujinga kufikiri kwamba kila mtu ulimwenguni atafanya jitihada hii. Wengi hawatafanya hivyo, kama vile wengi walioishi katika siku za mwanamume mwadilifu Noa hawakuwa tayari kufanya lililokuwa sawa. Katika ulimwengu huo uliojaa jeuri, ni Noa na familia yake pekee waliojiepusha na mwenendo usio wa kumwogopa Mungu, kwa njia hiyo wakapata kibali cha Mungu. Kwa kuondosha watu wasiomwogopa Mungu katika Gharika ya tufeni pote, Muumba wetu alitokeza kwa muda kuwepo kwa ulimwengu usiokuwa na uhalifu.

Ni jambo la maana kukumbuka kwamba simulizi la Biblia juu ya Furiko na uharibifu wa watu wasiomwogopa Mungu ni zaidi ya hadithi yenye kupendeza tu. Yesu Kristo alieleza: “Sawa na vile ilivyotukia katika siku za Noa, ndivyo itakavyokuwa pia katika siku za Mwana wa binadamu.” (Luka 17:26; 2 Petro 2:5; 3:5-7) Kama vile Mungu alivyoharibu ule ulimwengu uliojaa jeuri kabla ya Furiko, ndivyo pia atakavyoharibu ulimwengu huu uliojaa uhalifu.

Tuna jambo hili la hakika kutokana na chanzo chenye kutegemeka, kama ilivyoonyeshwa na mtume mpendwa wa Yesu Yohana: “Ulimwengu unapitilia mbali na ndivyo na tamaa yao, lakini yeye ambaye hufanya mapenzi ya Mungu hudumu milele.” (1 Yohana 2:17) Mwisho wa ulimwengu huu utatokeza njia kwa ulimwengu mpya ambao katika huo, Biblia husema, “[Mungu] atakaa pamoja na [wanadamu], nao watakuwa vikundi vya watu wake. Na Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. Naye atafuta kabisa kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala ombolezo wala kupaaza kilio wala umivu halitakuwapo tena kamwe.”—Ufunuo 21:3, 4.

Ikifafanua jinsi ulimwengu mpya utakavyokuja, Biblia husema pia: “Bali waovu watatengwa na nchi, nao wafanyao hila watang’olewa.” (Mithali 2:22) Kukiwa na wanyoofu pekee waliobakia duniani, unabii huu wa Biblia utatimizwa: “Wenye upole watairithi nchi, watajifurahisha kwa wingi wa amani.”—Zaburi 37:11.

Katika ulimwengu mpya wa Mungu, hata wanyama watakuwa bila jeuri. Biblia inatabiri: “Mbwa-mwitu atakaa pamoja na mwana-kondoo, na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi; ndama na mwana-simba na kinono watakuwa pamoja, na mtoto mdogo atawaongoza. . . . Hawatadhuru wala hawataharibu katika mlima wangu wote mtakatifu; maana dunia itajawa na kumjua BWANA, kama vile maji yanavyoifunika bahari.”—Isaya 11:6-9; 65:17; 2 Petro 3:13.

Ulimwengu Mpya wa Mungu U Karibu

Habari njema ni kwamba hali zenye amani za namna hiyo karibuni zitatimizwa duniani pote. Kwa nini tunaweza kuwa na hakika hivyo? Kwa sababu ya kile ambacho Yesu alitabiri kingetokea mara tu kabla ya mwisho wa ulimwengu. Miongoni mwa mambo mengine, alitabiri: “Taifa litainuka dhidi ya taifa na ufalme dhidi ya ufalme, na kutakuwa na upungufu wa chakula na matetemeko ya dunia mahali pamoja baada ya pengine.” Aliongezea: “Kwa sababu ya kuongezeka kwa uasi-sheria upendo wa idadi iliyo kubwa zaidi utapoa.”—Mathayo 24:7, 12.

Mtume wa Yesu pia alitabiri: “Katika siku za mwisho [za ulimwengu huu] nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo zitakuwa hapa. Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wapenda-fedha, wenye kujitanguliza, wenye kiburi, wakufuru, wasiotii wazazi, wasio na shukrani, wasio waaminifu-washikamanifu, wasio na shauku ya kiasili, . . wasio na hali ya kujidhibiti, wakali, wasio na upendo wa wema, . . . wenye kuzipenda raha badala ya kuwa wapenda-Mungu.” (2 Timotheo 3:1-5) Bila shaka, tunaishi katika “siku za mwisho” za ulimwengu huu! Kwa hiyo, karibuni, mahali pake patachukuliwa na ulimwengu mpya wenye uadilifu wa Mungu!

Funzo la Biblia limesadikisha mamilioni kwamba ulimwengu usio na uhalifu unaweza kupatikana, na sasa wanatenda kwa kuitikia mwaliko wa kufundishwa katika njia za Muumba wetu, Yehova Mungu. (Isaya 2:3) Je, ungependa kujiunga nao? Je, umejitayarisha kufanya jitihada ili kupata uhai katika ulimwengu mpya usio na uhalifu?

Yesu alionyesha ni nini linalohitajika kwanza kabisa. Alieleza: ‘Hii yamaanisha uhai udumuo milele, wao kuendelea kutwaa ujuzi juu yako wewe, Mungu pekee wa kweli, na juu ya yule uliyemtuma, Yesu Kristo.’ Hivyo, hali njema yako idumuyo milele yategemea kujifunza kwako Neno la Mungu na kutenda kupatana na yale unayojifunza.—Yohana 17:3.

[Picha katika ukurasa wa 8, 9]

Biblia hufafanua ulimwengu mpya usio na uhalifu na kutuambia jinsi tunavyoweza kuuonea shangwe

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki