Njoo, Usikie Hotuba ya Watu Wote Bila Malipo “Njia ya Pekee Iongozayo Kwenye Uhai Udumuo Milele”
Karibu miaka 20 iliyopita, Dakt. Alvin Silverstein aliandika hivi katika kitabu chake Conquest of Death: “Tutafumbua kiini cha uhai. Tutaelewa . . . jinsi mwanadamu huzeeka.” Hata alitabiri kuwa: “Hakutakuwako tena watu ‘wazee,’ kwa kuwa ujuzi ambao utaruhusu kushindwa kwa kifo utaleta pia ujana wa milele.”
Hivi karibuni zaidi, makala katika The New York Times Magazine la Septemba 28, 1997, iliripoti kuhusu “upanuzi wa uhai” msimamo wa kutegemea mazuri unaoshirikiwa na idadi fulani ya watu wenye kujali afya ambao wana shauku kuhusu uwezo wa tekinolojia ya leo. “Kwa kweli naamini kuwa huenda tukawa kizazi cha kwanza ambacho kitaishi milele,” akasema mtu mmoja mwenye shauku. Mwingine alisemekana kuwa “mwenye furaha na mwenye uhakika . . . kwamba kuongezwa kwa mbinu za kijeni kutapatikana karibuni ili kuokoa [kizazi hiki] kwa kukomesha kuzeeka, labda kurudisha uzee nyuma.” Je, kutumaini mema kama huku kwa kushangaza?
Je, waamini kuwa mwanadamu kupitia tekinolojia yake atashinda kifo? Au kuna njia nyingine ya kuishi milele? Mamilioni ya watu kote ulimwenguni wanaamini kuwa uhai udumuo milele waweza kufikiwa kwa hakika. Jifunze jinsi gani kwa kukubali mwaliko wa kusikiliza hotuba ya watu wote yenye kusisimua “Njia ya Pekee Iongozayo Kwenye Uhai Udumuo Milele,” ambayo itatolewa katika “Njia ya Mungu ya Maisha,” Mkusanyiko wa Wilaya wa Mashahidi wa Yehova. Waweza kuisikiliza katika eneo lililoko karibu na nyumbani kwako, kwani kuanzia mwanzo wa mwezi huu, itatolewa katika mamia ya mikusanyiko kote ulimwenguni.
Wasiliana na Mashahidi wa Yehova wa kwenu au uwaandikie wachapishaji wa gazeti hili wakueleze mahali pa mkusanyiko palipo karibu zaidi nawe.