Msamaha wa Mkubwa wa Polisi
Tom Will Lane alikuwa ndiye mkubwa wa polisi ambaye Edward Michalec alisimulia juu yake katika makala ya “Amkeni!” ya Desemba 22, 1996, yenye kichwa “Niliimarishwa Kukabili Majaribu Yaliyokuwa Mbele.” Katika masimulizi hayo, Michalec asimulia:
“Mkubwa wa polisi wa Wharton, Texas, Marekani, alikuwa mwenye ghadhabu sana. Akinipeleka jela kwa mara ya nne, alisema kwa sauti kubwa: ‘Kwa nini hutii amri?’
“‘Nina haki kabisa ya kufanya jambo hili,’ nikajibu mara moja. Kusema hivyo kulimghadhabisha mkuu huyo hata zaidi, akaanza kunipiga kwa fimbo. Polisi wengine wakajiunga naye, wakinipiga kwa sehemu za nyuma za bastola zao.”
Hivi majuzi Mary Perez, mwanamke mmoja aliyemfanyia kazi huyo Mkubwa wa Polisi, Lane, katika miaka ya mapema ya 1960, aliandika hivi: “Alijua kwamba mimi ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Aliniambia jinsi alivyomnyanyasa Ed Michalec. Aliniambia niwaeleze Mashahidi wengine kwamba anaomba radhi kwa matendo yake. Anasema yeye hakujua kwamba Mashahidi walikuwa watu wema wenye kutii sheria. Alisikitika kwelikweli.”
Mary aliongezea: “Ingawa mkubwa huyo wa polisi alikufa miaka kadhaa iliyopita, natumaini kwamba barua hii itawasilisha radhi yake.”
Kisha akasimulia jinsi alivyopata kuwa Shahidi: “Mnyanyaso wa Ndugu Michalec ulianza katika miaka ya mapema ya 1940. Kwa sababu hii niliazimia kusikiliza Mashahidi walipobisha mlango wangu. Upesi tulianza kujifunza Biblia. Tukabatizwa na mume wangu mnamo 1949.”
Huu ni mfano mwingine tu ambao unaonyesha matokeo makubwa kwa maisha za wengine wakati mtu anaposimama imara kutetea kanuni za Kikristo. Kwa mfano, ni wangapi wamevutiwa sana na msimamo wenye moyo mkuu wa Petro na mitume wengine katika karne ya kwanza?—Matendo 5:17-29.
[Picha katika ukurasa wa 31]
Ed Michalec na Mary Perez, miaka ya 1940