Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g99 2/8 kur. 16-19
  • Aina ya Mavazi Tunayovalia—Je, Yapasa Kufikiriwa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Aina ya Mavazi Tunayovalia—Je, Yapasa Kufikiriwa?
  • Amkeni!—1999
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mtindo Hueleza Nini?
  • Ni Nini Kinachozipata Kanuni za Mavazi?
  • Kwa Nini Kujifikiria Kupita Kiasi na Kutaka Kujitambulisha?
  • Je, Nimevalia Ifaavyo?
  • Valia kwa “Utimamu wa Akili”
  • Je, Mtindo Wako wa Mavazi Unamtukuza Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Naweza Kuboreshaje Jumla ya Mavazi Yangu?
    Amkeni!—1995
  • Kwa Nini Mavazi na Mwonekano Wetu Ni Muhimu?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Kuvaa na Kujipamba kwa Kiasi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1999
g99 2/8 kur. 16-19

Aina ya Mavazi Tunayovalia—Je, Yapasa Kufikiriwa?

“SIJUI nivalie nini!” Je, ombi hili la kutaka msaada lasikika kuwa la kawaida? Bila shaka, viwanda vya leo vya mitindo ya mavazi, sikuzote vinakuwa na hamu ya kukusaidia—au kukutatanisha hata zaidi—na mitindo yao ya karibuni.

Linalofanya maamuzi yawe magumu hata zaidi ni kwamba siku hizi waweza kutiwa moyo uvalie, si kirasmi, bali kikawaida. Kuhusu mwelekeo huu ulio kinyume cha mambo wa miaka ya 1990, tahariri moja ya mitindo ya mavazi yasema: “Inaweza kutuliza kufahamu kwamba si jambo lenye kukubalika tu kuonekana umeumbuka kidogo, umezeeka, umevalia mavazi ya kawaida na yaliyochujuka, bali ni jambo linalotamanika.”

Naam, katika miaka ya karibuni matangazo ya biashara yanayofanywa kwa juhudi nyingi, vigezo vya kuigwa vya televisheni, marika, kujitutumua, na pia kutamani kutambuliwa yamechangia uvutano mkubwa kuhusu mavazi ambayo watu wanavaa, hasa wachanga. Wengine wao hata huiba ili waonekane kuwa wa kimtindo.

Mitindo mingi inayopendwa na wengi ya miaka ya 1990 inatokana na tamaduni za miaka ya karibuni zinazoshikilia maoni yanayopita kiasi kama vile harakati za hipi katika jumuiya ya Magharibi ya miaka ya 1960. Ndevu, nywele ndefu zisizochanwa, na mavazi yenye kukunjana na machafu yalidhihirisha kupuuzwa kwa kanuni za kitamaduni. Lakini mavazi ya uasi pia yalianzisha desturi mpya, msongo mpya wa marika.

Mavazi yamekuwa njia ya kawaida ya kujitambulisha na kujieleza zaidi. Mavazi, hasa T-shati, yamekuwa bango za matangazo, yakitangaza kwa njia isiyo waziwazi michezo inayopendwa na wachezaji mashujaa, vichekesho, kupoteza imani, uchokozi, adili—au ukosefu wake—na bidhaa za biashara. Au yanaweza kutisha. Fikiria kichwa cha habari cha hivi karibuni katika gazeti Newsweek: “Unyama Ukiwa Kauli ya Mtindo wa Vijana.” Makala hiyo yamnukuu kijana mwenye umri wa miaka 21 akiongea kuhusu T-shati yake: “Mimi huivalia kwa sababu inaeleza watu niko katika hali gani. Sitaruhusu mtu yeyote aniambie jambo la kufanya na sitaki kusumbuliwa.”

Mambo yanayoonyeshwa kwenye T-shati yaweza kutofautiana kwa watu mbalimbali. Lakini kukubaliana—na kitu kinachotambulisha kikundi fulani au na roho ya kawaida ya uasi, mtazamo wa mimi kwanza, utundu, au ujeuri—ni mambo dhahiri. Msanii mmoja hutoboa mashimo kwenye nguo kupatana na anavyoelezwa na mteja. “Wanaweza kuchagua mashimo ya bastola, ya bunduki, au ya bombomu,” asema. “Ni kauli ya mtindo tu.”

Mtindo Hueleza Nini?

“Kwa kawaida mavazi ni njia moja ya kujitambulisha kuwa wa kikundi fulani katika jamii,” asema Jane de Teliga, ofisa msimamizi wa mitindo kwenye Jumba la Makumbusho la Powerhouse, Sydney, Australia. Aongezea hivi: “Unachagua kikundi unachotaka kushirikishwa nacho na kuvalia kulingana nacho.” Dakt. Dianna Kenny, mhadhiri wa saikolojia katika Chuo Kikuu cha Sydney, alisema kwamba yakiwa namna ya kuainisha watu mavazi ni ya maana kama vile dini, utajiri, kazi ya kuajiriwa, kabila, elimu, na anwani ya nyumbani. Kulingana na gazeti Jet, karibu mgongano wa tofauti za kirangi utukie katika shule moja ya Wazungu peke yao katika Marekani “kuhusu wasichana Wazungu wenye kusuka nywele, wenye kuvalia mavazi makubwa-makubwa, na mitindo mingine ya ‘hipu-hopu’ kwa sababu inahusishwa na Weusi.”

Pia kuna tofauti za vikundi katika tamaduni ndogo fulani, kama vile ulimwengu wa muziki: “Katika visa vingi,” lasema gazeti Maclean’s, “mavazi hufaana na mapendezi ya muziki: mashabiki wa rege huvalia rangi nyangavu na chepeo za Jamaika, huku wenye kupendelea roki aina ya granji wakivalia chepeo zilizofumwa kwa uzi na mashati yenye mistari.” Lakini hata yawe ya namna gani, ya kizembe, ya kawaida, mwonekano wa kuwa bila makao na wa kimaskini, unaoitwa granji, waweza kugharimu kiasi kikubwa cha fedha.

Ni Nini Kinachozipata Kanuni za Mavazi?

“Kila kitu ni kinyume cha kile unachoweza kufikiri,” asema mwandishi wa safu za gazeti Woody Hochswender. “Mitindo ya wanaume ambayo, wakati mmoja iliongozwa na kanuni kali, inazidi kuwa yenye ufidhuli . . . Kila kitu chapaswa kuonekana kana kwamba kimewekwa ovyoovyo.” Hata hivyo, mwelekeo huu, katika vikao fulani waweza kuonyesha mtazamo wa kutojali. Au waweza kudhihirisha ukosefu wa kujistahi au kukosa kuwastahi wengine.

Katika makala kuhusu maoni ya wanafunzi kuelekea walimu, jarida Perceptual and Motor Skills laeleza kwamba “ingawa mwalimu aliyevalia jinzi alionwa kuwa mwenye kuleta mzaha darasani, maoni yake hayakustahiwa sana na mara nyingi alichaguliwa kuwa mwalimu asiyejua kitu chochote.” Jarida hilohilo laeleza kwamba “mwalimu wa kike aliyevalia jinzi alionwa kuwa mwenye mzaha, mwenye kufikika, lakini si mwenye ujuzi hasa, asiyestahiwa sana, asiye kama mwalimu, na kwa ujumla anayependelewa.”

Wakati huohuo, katika sehemu ya kazini, bado tuna kauli ya kimtindo: kuvalia kwa njia yenye kuvutia uangalifu. Katika miaka ya karibuni wanawake zaidi wametaka kujipatia madaraka kazini. “Mimi huvalia ili kuvutia,” asema Marie, meneja wa kiwanda cha uchapishaji. “Nataka kuwa mashuhuri. Nataka kuonekana kama kitu cha kutisha,” aongezea. Marie ni mwenye kufuatia haki katika kufunua kwamba anajielekezea fikira.

Mitindo inayopendwa inaonekana makanisani pia. Watu fulani wanaopenda sana mitindo wametumia kanisa lao kutangaza mitindo yao ya karibuni. Na bado, leo, makasisi, huku wakipambwa kwa kanzu zao zenye kuning’inia, mara nyingi wakiwa kwenye mimbari huangalia kwa dharau kutaniko lililovaa jinzi na raba au katika mavazi ya kimtindo.

Kwa Nini Kujifikiria Kupita Kiasi na Kutaka Kujitambulisha?

Wanasaikolojia wanasema kwamba mavazi ya kimtindo—hasa miongoni mwa vijana—ni namna ya ubinafsi, katika maana ya kwamba yanadhihirisha tamaa ya kuelekezewa uangalifu. Wanayafafanua kuwa “mwelekeo wenye kudumu kwa upande wa vijana wa kujiona kuwa kitu cha kuelekezewa uangalifu na wengine.” Kwa kweli anasema: “Nafikiri unanifikiria kupita kiasi kama ninavyojifikiria mwenyewe.”—American Journal of Orthopsychiatry.

Falsafa zinazokazia umaana wa mwanadamu na kumpuuza Mungu pia zimeendeleza maoni (mara nyingi yanaenezwa na mfumo wa biashara) kwamba wewe, ndiwe mtu wa maana zaidi katika ulimwengu wote mzima. Tatizo ni kwamba, sasa kuna watu wapatao bilioni sita ‘walio wa maana zaidi.’ Mamilioni ya watu katika dini za Jumuiya ya Wakristo wamejiunga katika kufuatia kupita kiasi vitu vya kimwili, wakijitahidi kufikia “kiwango cha juu cha maisha, ya wakati uliopo.” (Linganisha 2 Timotheo 3:1-5.) Kwa kuongezea kuna kuzorota kwa kizio cha familia na upendo wa kweli, na haishangazi kwamba wengi, hasa vijana, wako tayari kufanya jambo lolote ili kujipatia utambulisho wa aina fulani na usalama.

Hata hivyo, kwa kawaida wale wanaohangaikia mavazi na msimamo wao mbele za Mungu hujiuliza: Napaswa kujipatanisha na kanuni za mavazi zinazobadilika kwa kadiri gani? Nitajuaje ikiwa mavazi yangu yanafaa? Je, yanatoa ishara zenye kutatanisha au hata zisizo za kweli kunihusu?

Je, Nimevalia Ifaavyo?

Kwa msingi, mavazi tunayovalia ni jambo la uchaguzi wa kibinafsi. Mapendezi yetu hutofautiana, kama vile mapato yetu ya kifedha. Na desturi hutofautiana katika mahali mbalimbali, katika nchi mbalimbali, na katika maeneo mbalimbali yenye tabia ya nchi inayotofautiana. Lakini bila kujali hali yako, kumbuka kanuni hii: “Kwa kila jambo kuna majira yake, na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.” (Mhubiri 3:1) Yaani, valia kulingana na hali. Na pili, “kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako.”—Mika 6:8.

Hilo halimaanishi kuvalia kwa adabu bali, kwa njia ambayo ni “yenye mpangilio mzuri” na inayodhihirisha “utimamu wa akili.” (1 Timotheo 2:9, 10) Mara nyingi, hili humaanisha kwa usahili kujizuia, sifa ambayo gazeti Working Woman huiambatanisha na kupambanua mazuri na adabu nzuri. Likiwa jambo la kawaida, usiruhusu kamwe mavazi yako yawe kitu cha kwanza kutambuliwa unapoingia ndani ya chumba, ili kuwashinda wengine. Kichapo Working Woman chasema: “Valia . . . katika njia ambayo watu hawatakengeushwa fikira na mavazi yako lakini waweze kuona wema wako.”

Jarida Perceptual and Motor Skills lasema kwamba: “Mkusanyo wa fasihi zinazochunguza wazo ambalo hutolewa na mwenye kuvalia mavazi na fungu linalotimizwa kuwapa wengine ujumbe fulani huonyesha kwamba mavazi ni kidokezi cha maana kinachotumiwa kuwahukumu wengine tuwaonapo mara ya kwanza.” Katika wazo hilihili mwanamke mmoja akiwa katika umri wa miaka 40, ambaye awali alifurahia uwezo wake wa kuvutia watu kwa namna alivyovalia, asema hivi: “Kulinisababishia matatizo makubwa sana kwa sababu kulifanya iwe vigumu kutofautisha maisha yangu ya kikazi na ya kibinafsi. Sikuzote nilifikiwa na wanaume wakitaka kunikaribisha kwa chakula kikuu cha siku.” Mhasibu mmoja wa kike, akifafanua mtindo unaotofautiana na huo, asimulia hivi: “Nimeona jinsi ambavyo wanaume wanajiendesha kuelekea wanawake wanaovalia kikawaida, au wanaovalia kwa kufuatia sana mtindo wa kiume. Wanadhaniwa kuwa wanawake wachokozi na wanaonyeshwa ufikirio kidogo na wanaume katika shughuli za kikazi.”

Mwanamke mmoja kijana anayeitwa Jeffie alitambua kwamba alikuwa akitoa ishara zenye kutatanisha aliponyolewa kwa njia ya kimtindo. “Nilifikiri tu ilionekana kuwa ‘tofauti,’” akumbuka. “Lakini watu walianza kuniuliza, ‘Je, kwa kweli wewe ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova?’ na hilo liliniaibisha.” Jeffie alihitaji kujiuliza maswali ya kujichanganua. Je, si kweli kwamba “kutoka katika wingi wa moyo” si kinywa chetu hunena tu bali pia mavazi na mapambo yetu? (Mathayo 12:34) Mavazi yako hufunua nini—moyo wenye nia ya kuelekeza uangalifu kwa Muumba au kwako mwenyewe?

Valia kwa “Utimamu wa Akili”

Fikiria, pia, jinsi ambavyo mavazi yako hukuathiri wewe. Mavazi ya kutaka uangalifu na kuvalia kupita kiasi kwaweza kukufanya uwe mwenye ubinafsi sana, mavazi yasiyo nadhifu yaweza kuimarisha mawazo yasiyofaa uliyo nayo kujielekea, na T-shati zinazotangaza bingwa umpendaye wa sinema au wa michezo au shujaa mwingine zaweza kukuchochea uabudu mashujaa—ibada ya sanamu. Naam, mavazi yako hunena na wengine—na kuwaambia jinsi ulivyo.

Mavazi yako yanasema nini kukuhusu ikiwa unavalia ili utambuliwe au unavalia ili kusisimua? Je, unaimarisha vitabia vya utu ambavyo kwa kweli unapaswa kuwa uking’ang’ana kuvishinda? Zaidi ya hilo, unajaribu kuvutia mtu wa aina gani? Shauri lililorekodiwa katika Waroma 12:3 laweza kutusaidia tushinde ubinafsi, ubatili, na mawazo yasiyofaa. Hapo mtume Paulo atushauri ‘tusijifikirie [wenyewe] zaidi kuliko ilivyo lazima kufikiri; bali tufikiri ili tuwe na akili timamu.’ Kuwa na “akili timamu” kwamaanisha kuwa na busara.

Jambo hili ni la maana hasa kwa wale walio na nyadhifa za madaraka na waliokabidhiwa amana. Kielelezo chao kinaathiri sana wengine. Sikuzote, wale wanaojitahidi kufikia mapendeleo ya utumishi katika Kutaniko la Kikristo na wake zao Wakristo hali kadhalika wangeonyesha mtazamo wenye kiasi na wenye kustahiwa katika mavazi na mapambo yao. Hatungependa kamwe kuwa kama mtu anayetajwa katika kielezi cha Yesu cha karamu ya ndoa: “Mfalme alipoingia kuwakagua wageni-waalikwa aliona mara hiyo hapo mtu asiyevishwa vazi la ndoa.” Baada ya kufahamu kwamba mwanamume huyu hakuwa na sababu halali ya kuvalia vazi la namna hiyo lisilo na heshima, “mfalme akasema kwa watumishi wake, ‘Mfungeni mikono na miguu na kumtupa ndani ya giza kule nje.’”—Mathayo 22:11-13.

Hivyo, ni muhimu wazazi wasitawishe ndani ya watoto wao mtazamo na upendezi unaofaa kuhusu mavazi kupitia kwa neno na kwa kielelezo. Nyakati nyingine huenda hili likamaanisha kwamba wazazi watahitaji kuwa thabiti wanaposababu na mwana au binti yao. Lakini inatia moyo kama nini tunaposifiwa bila kutarajia kuhusu kiwango cha juu cha mavazi na mwenendo wa vijana wetu na wetu pia!

Naam, watumishi wa Yehova wamewekwa huru na ubatili, mitindo ghali, na kujifikiria kupita kiasi. Wao wanaongozwa na kanuni za kimungu, si na roho ya ulimwengu. (1 Wakorintho 2:12) Ikiwa unaishi kupatana na kanuni hizi, kuchagua mavazi yako hakupaswi kuwa jambo gumu sana. Zaidi ya hilo, kama vile fremu ya picha iliyochaguliwa vizuri, mavazi yako hayatafunika kupita kiasi utu wako wala kuufedhehesha. Na kadiri ujitahidivyo kuwa kama Mungu, ndivyo utakavyositawisha urembo wa kiroho ambao hauamuliwi na mavazi uliyo nayo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki