Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g99 4/8 kur. 5-7
  • Mashaka Yako Ulimwenguni Kote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mashaka Yako Ulimwenguni Kote
  • Amkeni!—1999
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Tumaini Lao Lavunjwa na Wale Waliowaitibari
  • Matokeo Mabaya Sana
  • Kuzuia Nyumbani
    Amkeni!—1993
  • Jinsi ya Kuwalinda Watoto Wako
    Amkeni!—2007
  • Upendo na Haki Katika Ulimwengu Mwovu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Mawazo Yasiyo ya Kweli Ambayo Ni ya Kawaida
    Amkeni!—1993
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1999
g99 4/8 kur. 5-7

Mashaka Yako Ulimwenguni Kote

MAUJI ya kinyama ya watoto wanaoishi barabarani katika Brazili bado ni mfano mwingine unaoonyesha ukosefu wa usalama wa watoto wasiotakikana. Ripoti kutoka nchi hiyo zilisema kwamba mamia kadhaa ya watoto walikuwa wakiuawa kila mwaka.

Watoto wameshambuliwa kikatili katika Dunblane, Scotland, na Wolverhampton, Uingereza, na sehemu nyinginezo. Kwa kielelezo, wazia kuteseka kwa Maria mwenye umri wa miaka 12, ambaye ni yatima kutoka Angola aliyebakwa na kupata mimba. Baadaye alilazimishwa kutembea kilometa 320 hivi, ambapo baadaye alijifungua mtoto kabla ya wakati wake aliyeishi majuma mawili tu. Maria alikufa baada ya juma moja, akiwa mgonjwa na aliyekosa kulishwa chakula cha kutosha.

Mwaka wa 1992 ripoti moja ya Hazina ya Watoto ya Umoja wa Mataifa (UNICEF) ilisema kwamba “‘vita dhidi ya watoto’ ni jambo lililobuniwa katika karne ya 20.” Kulingana na ripoti moja ya 1996 ya shirika la UNICEF, maoni ya watu fulani ni kwamba ‘vizazi vijavyo vya adui, yaani, watoto wa adui, lazima pia viondolewe.’ Mwelezaji wa kisiasa alifafanua jambo hili kwa njia hii: “Ili kuua panya wakubwa, ni lazima uue panya wadogo.”

Hivi karibuni watoto milioni mbili wameuawa kijeuri katika kipindi cha miaka kumi. Wengine milioni nne wamelemazwa, wakapofushwa, au wakaharibiwa akili na mabomu yanayotegwa chini ya ardhi, wakijitahidi kupambana na maisha kadiri wawezavyo pamoja na mamilioni wengi waliopoteza makao yao wakati wa vita. Haishangazi kwamba ripoti moja ilikuwa na kichwa hiki cha habari: “Majinamizi Yenye Kuogofya ya Ukatili wa Vita kwa Watoto.”

Ukatili huu ambao umefanywa dhidi ya watoto ni tatizo kwa jamii ya kibinadamu, ithibati hakika kwamba watoto wana matatizo, si katika nchi chache tu bali ulimwenguni pote. Na watoto wengi ambao wametendwa vibaya wamevunjiwa tumaini pia.

Tumaini Lao Lavunjwa na Wale Waliowaitibari

Mtoto anapovunjiwa tumaini makovu mabaya sana ya kihisia-moyo yaweza kutokea. Huwa hivyo hasa mtu anayevunja tumaini la mtoto anapokuwa ni mzazi, rafiki, au mshauri. Mweneo wa tatizo hili la wazazi kuwatenda watoto vibaya unaonyeshwa na simu nyingi zilizopokewa kwenye laini ya simu ya moja kwa moja baada ya kutangazwa kwa kipindi cha mazungumzo kilichoitwa “Kutishwa Kimyakimya: Kufichua na Kukomesha Kutenda Watoto Vibaya,” kilicholetwa na Oprah Winfrey katika Marekani. “Simu zenye kuogofya zaidi zilitoka kwa watoto wachanga, waliosema kwa hofu, wanataka kutoroka wasipatwe na maumivu ya kimwili au kutendwa vibaya kingono,” akasema msimamizi wa kipindi hicho Arnold Shapiro, kama alivyonukuliwa katika jarida Children Today.

Tukio hili lilichangia sehemu kubwa ya kukanusha wazo la kwamba watu wanaowatenda watoto vibaya ni wageni wakubwa wenye kutisha. Uhakika ni kwamba “wengi wanaowatenda watoto vibaya ni wazazi na jamaa wengine wa karibu,” amalizia Shapiro. Uchunguzi mwingine unathibitisha jambo hili na pia unaonyesha kwamba nyakati nyingine rafiki za familia wanaotumainiwa walimtayarisha mtoto na familia kwa kisa cha kumtenda mtoto huyo vibaya baadaye. Ngono ya maharimu ni uvunjaji wa tumaini wenye kushtua zaidi.

Kutendwa vibaya kingono na watu wanaovutiwa kingono na watoto ni tisho jingine linalowakabili watoto ulimwenguni pote. Kijarida Trends & Issues in Crime and Criminal Justice chatoa fasiri hii: “Kuvutiwa kingono na watoto kwarejezea uvutio wa kingono kuelekea mtoto aliye mchanga sana. . . . Sikuzote kuvutiwa kingono na watoto huhusisha kutenda uhalifu kama vile kushambulia kingono, mambo ya aibu na makosa yanayohusisha ponografia ya watoto.”

Ripoti zenye kusikitisha za vikundi vya watu wenye kuvutiwa kingono na watoto, ambao huwatumia watoto vibaya kwa pupa, zinazidi kupokewa kutoka sehemu zote za ulimwengu. (Ona sanduku kwenye ukurasa wa 7.) Wenye kutendwa vibaya ni wavulana na wasichana wachanga. Wakishawishwa na wanaume wasio na adili, wanatendwa vibaya kingono na kisha wanatishwa au kudekezwa kupita kiasi ili kuwachochea wabaki katika “kikundi” hiki. Wanaume ambao hupanga na kufanya matendo haya maovu mara nyingi huwa ni viongozi mashuhuri wa jumuiya na nyakati nyingine hufanya hivyo huku polisi na idara ya mahakama wakiwa na habari za kutosha na kuwalinda.

Jambo lenye kufedhehesha pia linasababishwa na makasisi wanaowatenda watoto vibaya kingono. Habari kutoka ulimwenguni pote zafunua kiwango kikubwa cha watoto wanaotendwa vibaya kingono na makasisi, nyakati nyingine hata kwa jina la Mungu. Kwa kielelezo, kasisi Mwanglikana aliyethibitishwa kuwa na hatia alimwambia mvulana mwenye umri wa miaka kumi kwamba “Mungu alikuwa akinena kupitia kwake [kasisi huyo], na kitu chochote alichofanya au kitu chochote [mvulana huyo] alichofanya kilimpendeza Mungu na kwa hiyo kilifaa.”

Katika Australia pitio la kitabu The Battle and the Backlash: The Child Sexual Abuse War lilisema juu ya kutendwa vibaya kwa watoto na makasisi na watu wengine wenye nyadhifa zenye kuitibariwa. Lilisema kwamba mashirika yaliyohusika yalijali zaidi kulinda jinsi ambavyo yangeonekana na kujikinga yenyewe badala ya kuwalinda watoto wanaoweza kudhurika kwa urahisi.

Matokeo Mabaya Sana

Kwa kawaida tumaini la mtoto huwa kamili. Hivyo, tumaini hilo linapovunjwa, kunakuwa na matokeo mabaya sana kwa mtoto mchanga asiyeshuku hatari yoyote. Kichapo Child Abuse & Neglect chasema hivi: “Watu na mahali ambapo awali palikuwa penye kuandaa usalama au tegemezo pamehusianishwa na hatari na hofu. Maisha ya mtoto yanazidi kuwa yasiyotabirika na yasiyoweza kudhibitiwa.”

Tokeo la kutendwa vibaya namna hiyo, ambapo visa vingi vimeendelea kwa miaka mingi, ni kwamba watoto fulani wamepatwa na matatizo ya kijamii na ya kiakili baadaye maishani, mpaka wanapokuwa watu wazima. Kuvunjwa huku kwa tumaini ni jambo baya sana kwa sababu mtoto ametumiwa kwa kujinufaisha kwa sababu tu ni mtoto. Lakini watoto wengi wanaotendwa vibaya hawasemi habari hizo kamwe—jambo ambalo hutumainiwa na watu wenye kuwatenda watoto vibaya.

Katika miaka ya karibuni, uthibitisho kutoka ulimwenguni pote wa kuwatenda watoto vibaya unazidi kuongezeka, hivi kwamba leo umekuwa mwingi sana kutoweza kukanushwa au kupuuzwa tena. Lakini wengi wanakubali kwamba kukomeshwa kabisa kwa zoea la kuwatenda watoto vibaya ni kazi yenye kutisha. Hivyo kunatokea maswali haya: Je, kuna mtu yeyote anayeweza kuwalinda kikweli watoto wetu? Wale ambao ni wazazi miongoni mwetu wanaweza kulindaje urithi kutoka kwa Mungu na kutunza maisha yanayoweza kudhurika kwa urahisi ya watoto wetu wachanga? Wazazi wanaweza kupata wapi msaada?

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 7]

Utendaji wa Internet Unaofanywa kwa Uangalifu

Miezi michache iliyopita, katika mojawapo ya jitihada kubwa zaidi iliyopata kufanywa ya utendaji wa siri dhidi ya ponografia ya watoto inayopitishwa kwenye Internet, polisi katika nchi 12 walivamia nyumba za washukiwa zaidi ya 100 wenye kuvutiwa kingono na watoto. Kutoka kikundi kimoja tu cha wanaume wenye kuvutiwa kingono na watoto huko Marekani, walitwaa picha za kiponografia za watoto zaidi ya 100,000.

Mpelelezi wa Uingereza aliyeratibu uchunguzi huo wa Internet wa miezi mitano alisema hivi: “Mambo yaliyomo yangemfanya mtu yeyote mwenye akili timamu ashikwe na kichefuchefu.” Kulikuwa na watoto wa jinsia zote mbili, wengine wakiwa na umri wa miaka miwili. Polisi wa Ubelgiji walisema kwamba picha za Internet ndizo zilizokuwa “zenye kunyarafisha zaidi kati ya ponografia ya watoto. . . . Zilikuwa mbaya sana hivi kwamba watu walifikia kiwango cha kuwatenda vibaya watoto wao wenyewe ili waweze kutokeza picha zenye kutazamisha zaidi.” Mtu mmoja alipiga picha zake mwenyewe akimbaka mpwa wake wa kike na kuingiza picha hizi ndani ya kompyuta.

Washukiwa walitia ndani walimu, mwanasayansi, mwanafunzi wa sheria, kiongozi wa maskauti, mhasibu, na profesa wa chuo kikuu.

[Picha katika ukurasa wa 6]

Kitu chenye kulipuka kililemaza mkono wa kuume wa mvulana huyu

[Hisani]

UN/DPI Photo by Armineh Johannes

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 7]

Photo ILO/J. Maillard

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki