Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g99 4/8 kur. 8-11
  • Ni Nani Atakayewalinda Watoto Wetu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nani Atakayewalinda Watoto Wetu?
  • Amkeni!—1999
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Wazazi Wanaweza Kufanya Mengi
  • Utatuzi Halisi Pekee
  • Jinsi ya Kuwalinda Watoto Wako
    Amkeni!—2007
  • Kulea Watoto tangu Uchanga
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Zoeza Mtoto Wako Tangu Utoto Mchanga Sana
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Wazazi, Ulindeni Urithi Wenu Wenye Thamani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1999
g99 4/8 kur. 8-11

Ni Nani Atakayewalinda Watoto Wetu?

NI JAMBO lenye kutia moyo kujua kwamba sasa kutenda watoto vibaya ni tatizo linalokubaliwa ulimwenguni pote. Mashirika kama vile Mkutano wa Stockholm Dhidi ya Biashara ya Kutumia Watoto Vibaya Kingono, uliohudhuriwa na wawakilishi kutoka nchi 130, yamekazia uangalifu tatizo hili.

Kwa kuongezea, nchi fulani sasa zinatunga sheria zinazoharamisha utalii wa ngono na ponografia ya watoto. Wengine hata wanatengeneza orodha ya watu wanaojulikana kuwa wanavutiwa kingono na watoto, wakiwazuia wasiweze kuwapata watoto.

Kisha kuna wale wanaowatafutia watoto maisha bora kwa kutunga sheria za kuwalinda. Na nchi kadhaa zaidi na watu mmoja mmoja wanakataa kununua bidhaa zilizotengenezwa kwa kazi ngumu ya watoto.

Ingawa bila shaka sote husifu jitihada hizo za kukomesha zoea la kutenda watoto vibaya katika jamii, lazima tuone mambo kihalisi na kukiri kwamba kutenda watoto vibaya kumeenea sana ndani ya jamii ya kibinadamu. Lingekuwa jambo la ujinga kufikiri kwamba utatuzi sahili kama vile kutunga sheria ungewalinda watoto wetu kabisa. Tayari sheria nyingi zimepitishwa, na bado tatizo lingaliko. Uhalifu wa watu wazima ulimwenguni unafunuliwa waziwazi na mambo hakika yenye kusikitisha kwamba lazima sheria nyingi zitungwe ili kulinda haki za asili za mtoto.

Sheria si kinga ya mwisho kwa watoto. Tunahitaji tu kutazama matokeo ya sheria zilizotungwa zenye kutisha kama za azimio la Mkataba wa Haki za Mtoto wa UM, ambalo limetiwa sahihi na nchi nyingi. Imethibitishwa vya kutosha kwamba hata nyingi za serikali hizi, ambazo zimesongwa sana na hali za kiuchumi, hazifanyi jitihada za kutosha kukomesha kutumiwa vibaya kwa watoto wao. Kutenda watoto vibaya kwazidi kuwa tatizo kubwa la kimataifa.

Wazazi Wanaweza Kufanya Mengi

Kuwa mzazi mwenye mafanikio ni kazi inayohitaji jitihada nyingi. Inahitaji kujidhabihu. Lakini wazazi wanaojali wanahitaji kuhakikisha kwamba hawatawadhabihu watoto wao. Gazeti Maclean’s lasema kwamba mara nyingi “hali ya kuwa mzazi huonwa kuwa kama shughuli ya kujifurahisha.” Kitu cha kuchezea cha mtoto au shughuli ya kujifurahisha yaweza kukatishwa, lakini kuwa mzazi ni daraka kutoka kwa Mungu.

Kuwa mzazi mzuri ni mojawapo ya zawadi zenye thamani sana unazoweza kumpa mtoto wako, kwa kuwa zitamsaidia afurahie hali ya utotoni yenye usalama. Usalama huo hautegemei hadhi ya kijamii au ya kiuchumi maishani. Mtoto wako anakuhitaji—anahitaji upendo na shauku yako, uhakikishio wako anapohisi kuwa ametishwa, na anahitaji wakati wako. Mtoto wako anahitaji kusikia sauti yako ukimsimulia hadithi, anataka uwe kiolezo chake cha kuigwa, na anahitaji nidhamu yako yenye upendo.

Kuhusu habari ya adili za kingono—wazazi, mwe na uhusiano wa familia wenye kiasi na mheshimu akili na miili ya watoto wenu. Watoto hujifunza kwa wepesi sana mambo ambayo huvuka mipaka ya kiadili ambayo wazazi huwawekea. Wanahitaji kufundishwa namna ya kujiendesha wenyewe wanapokuwa nyumbani na wanapokuwa nje. Ukikosa kufanya hivyo, mtu fulani atafanya hivyo kwa niaba yako, na huenda usipendezwe na matokeo yake. Wafundishe watoto namna wanavyoweza kufanya ikiwa hali yao ya kiadili itapata kutishwa. Wajulishe sehemu zao za siri ni za kazi gani, na uwafundishe kwamba hazipasi kutumiwa vibaya. Waambie namna wanavyopaswa kutenda ikiwa mtu fulani anawajia na kutaka kuwatumia kwa kujinufaisha.

Nyakati zote jua mahali walipo watoto wako na ujue mtu aliye pamoja nao. Marafiki wa karibu wa mtoto wako ni akina nani? Ni nani ambao hutunza mtoto wako wakati haupo? Je, wanaweza kutumainiwa? Bila shaka, hilo halimaanishi kwamba mzazi apaswa kushuku kila mtu. Wachunguze ifaavyo watu wazima wanaoshughulika na mtoto wako, ukitazama zaidi ya sura ya nje.

Fikiria mvunjiko-moyo unaopata wazazi ambao wamegundua wakiwa wamechelewa mno kwamba watoto wao wametendwa vibaya na makasisi, walimu, au hata washiriki wa karibu wa familia waliowatumaini. Ingefaa kujiuliza hivi ukiwa mzazi, ‘Je, kanisa langu huvumilia au huficha zoea la kutenda watoto vibaya? Je, dini yangu inashikilia kwa imara kanuni za juu za kiadili?’ Majibu ya maswali haya yangeweza kukusaidia ufanye uchaguzi wa hekima katika kuwalinda watoto wako.

Zaidi ya yote, wasaidie wajue na kupenda kanuni za Muumba, zitakazowalinda wasipatwe na madhara. Watoto waonapo wazazi wao wakistahi kanuni za juu za adili, watakuwa tayari kufuata kielelezo hiki kizuri.

Utatuzi Halisi Pekee

Bila shaka, wala sheria wala vifungo vya muda mrefu havitaweza kuwalinda watoto wetu. Muumba kupitia Neno lake lililopuliziwa, Biblia, aweza kufanikiwa kutokeza mwenendo safi kiadili, kwa kubadili kufikiri kwa watu walio kama hayawani wawe kama washiriki wa jumuiya yoyote wenye upendo na wenye kufuatia adili.

Jambo hili limewezekana kama ambavyo imeonyeshwa tayari. Kuna wengi ambao wameacha mitindo-maisha ya kale ya uzinifu. Sasa wanatoa ithibati kubwa sana ya nguvu za Neno la Mungu. Lakini ingawa hii ni hatua inayofaa, wakosaji wengi waliopotoka hawatabadilika. Hii ndiyo sababu Yehova Mungu ameahidi kwamba wote wanaowatumia watoto wetu kwa faida yao karibuni wataondolewa duniani—pamoja na falsafa zao, tamaa zao, na pupa yao.—1 Yohana 2:15-17.

Kisha, katika ulimwengu mpya wa Mungu, wakati umaskini hautakuwapo tena, watoto wote watafurahia hali ya utoto wao bila kuharakishwa na bila kusumbuliwa, ambayo ni haki yao kutoka kwa Mungu. Hii haitamaanisha tu mwisho wa kutenda watoto vibaya bali pia mwisho wa mambo yote yenye kuhuzunisha yanayoharibu maisha ya watu leo: “Mambo ya kwanza hayatakumbukwa, wala hayataingia moyoni.”—Isaya 65:17.

Hivyo, katika ulimwengu mpya wa Mungu, maneno ya Yesu Kristo yatatimizwa kwa kiwango kikubwa zaidi: “Waacheni watoto wachanga, na komeni kuwazuia kunijia, kwa maana ufalme wa mbingu [ukitawala juu ya dunia, makao ya wanadamu ya Paradiso] ni wa walio kama hao.”—Mathayo 19:14.

[Picha katika ukurasa wa 9]

Wasaidie watoto wako wajifunze makusudi na kanuni za Muumba

[Picha katika ukurasa wa 9]

Wafundishe watoto wako kwa busara namna wanavyopaswa kutenda wanapotishwa kingono

[Picha katika ukurasa wa 9]

Unakuwa zawadi yenye thamani kwa watoto wako unapokuwa mzazi mwema

[Picha katika ukurasa wa 10]

Katika ulimwengu mpya wa Mungu, watoto wote watafurahia utoto wao kikamilifu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki