Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g99 8/8 kur. 9-10
  • Unaweza Kuchagua Wakati Wako Ujao

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Unaweza Kuchagua Wakati Wako Ujao
  • Amkeni!—1999
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Tukio Lisiloepukika na Hiari
  • Kisababishi na Matokeo
  • Utakuwa na Wakati Ujao wa Aina Gani?
  • Kutafuta Mambo Yaliyokusudiwa Kimbele ya Mwanadamu
    Amkeni!—1999
  • Je! Ajali Huongoza Wakati Wako Ujao?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Je! Wakati Ujao Wako Unaamuliwa na Ajali?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Wakati Wako Ujao, Upo Mikononi Mwako!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2018
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1999
g99 8/8 kur. 9-10

Unaweza Kuchagua Wakati Wako Ujao

IJAPOKUWA uaguzi ulionwa kuwa “utimizo mkubwa sana wa kielimu katika ulimwengu wa kale,” ulikuwa “ustadi uliodharauliwa na manabii Waebrania,” asema mwakiolojia Joan Oates. Kwa nini?

Licha ya kuzungukwa na mataifa yaliyoitikadi kwamba maisha huamuliwa kimbele, Waisraeli wa kale walikataa wazo la kwamba kani isiyojulikana iliongoza maisha yao. Katika maagizo yake kwa taifa hilo, Mungu aliwaambia: “Asionekane kwako . . . mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri, wala . . . [“mpiga-ramli,” NW].”—Kumbukumbu la Torati 18:10, 11.

Bila kufuata wazo la kuamuliwa kimbele kwa maisha na bila kutegemea wapiga ramli, Waisraeli wangeweza kuwa na uhakika juu ya wakati ujao. Ikieleza sababu, ensaiklopedia ya Kikatoliki ya Kifaransa Théo inataarifu kwamba taifa hilo liliitikadi kwamba “mwanadamu na ulimwengu haukuwa unaongozwa na kani fulani isiyojulikana. Mungu alikuwa na kusudi kwa mwanadamu.” Kusudi gani hilo?

Tukio Lisiloepukika na Hiari

Mungu aliwaahidi Waisraeli amani na ufanisi iwapo wangetii sheria zake. (Mambo ya Walawi 26:3-6) Kwa kuongezea, walimtazamia Mesiya ambaye angeleta hali za uadilifu duniani. (Isaya, sura ya 11) Hata hivyo, uhakika wa kwamba Mungu alikuwa ametoa ahadi hizi haukumaanisha kwamba mtu mmoja-mmoja angeketi tu kitako na kusubiri mambo yatukie. Kinyume cha hilo, waliambiwa: “Lo lote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako.”—Mhubiri 9:10.

Wazo hili lilitegemea hiari. Waisraeli walikuwa huru kumtumikia Mungu na kuchagua wakati wao ujao. Mungu aliwaahidi hivi: “Tena itakuwa, mtakaposikiza kwa bidii maagizo yangu niwaagizayo leo, kwa kumpenda BWANA, Mungu wenu, na kumtumikia kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote, ndipo nitakapowapa mvua ya nchi yenu kwa wakati wake, mvua ya masika, na mvua ya vuli, upate kuvuna nafaka yako, na divai yako, na mafuta yako.” (Kumbukumbu la Torati 11:13, 14) Waisraeli walipokea baraka za Mungu walipokuwa watiifu.

Kabla tu ya kuingia katika nchi iliyoahidiwa, Mungu alilipa taifa la Israeli uchaguzi: “Angalia, nimekuwekea mbele yako uzima na mema, na mauti na mabaya.” (Kumbukumbu la Torati 30:15) Wakati ujao wa kila mtu ulitegemea matendo yake na uamuzi wake. Kumtumikia Mungu kungetokeza uzima na baraka, ilhali kukataa kufanya hivyo kungeleta shida. Lakini namna gani leo?

Kisababishi na Matokeo

Tumewekewa mipaka na sheria kadhaa za kiasili ambazo zipo kwa faida yetu. Mojawapo ya sheria hizi ni sheria ya kisababishi na matokeo au, kama vile Biblia inavyosema, “Lolote lile mtu analopanda, hilo atavuna pia.” (Wagalatia 6:7) Tunapotambua kanuni hii, inawezekana kuzingatia uwezekano wa kutukia kwa matukio fulani ya wakati ujao.

Tukiendesha gari kwa kasi bila hadhari, tutaelekea kupata aksidenti kuliko tunapoendesha kwa hadhari. Tukivuta sigareti, tutaelekea sana kushikwa na kansa kuliko tusipovuta. Kwa kweli, matukio kama lile shambulio la magaidi lililotajwa katika makala ya kwanza ya mfululizo huu yaelekea kwamba hayawezi kutupata sisi, na kukisia uwezekano lingekuwa jambo bure. Hata hivyo, kushikilia wazo la kuamuliwa kimbele kwa maisha hakutatunufaisha. Hakutuelimishi juu ya wakati wa sasa wala wakati ujao. Kuitikadi jambo lisilo la kweli hakutuhakikishii wakati ujao. Wala kufikiri kwamba Mungu ndiye anayeamua matokeo katika kila tukio.

Utakuwa na Wakati Ujao wa Aina Gani?

Wakati wetu ujao haukutangulia kuandikwa lakini unaamuliwa na wakati wa sasa. Hata ingawa uhai ni zawadi kutoka kwa Mungu, Biblia husema waziwazi kwamba tuna fungu muhimu la kutimiza katika kuamua wakati wetu wa sasa na wa wakati ujao. Uhakika wa kwamba tuna uchaguzi wa ama kumfurahisha Mungu ama kumhuzunisha, unaonyesha kwamba Mungu ameturuhusu tuchague kwa kiasi fulani maisha tunayotaka.—Mwanzo 6:6; Zaburi 78:40; Mithali 27:11.

Kwa kuongezea, Maandiko Matakatifu yanakazia tena na tena kwamba wakati wetu ujao unahusiana na uvumilivu wetu na mwendo wetu wa maisha, mambo ambayo hayangekuwa na maana ikiwa yale yatakayompata mtu yameshaamuliwa kimbele. (Mathayo 24:13; Luka 10:25-28) Hivyo basi, ikiwa tutachagua kuwa watiifu na waaminifu kwa Mungu, tunaweza kutarajia wakati ujao wa aina gani?

Biblia hufunua kwamba wanadamu wana wakati ujao mwangavu sana. Dunia itageuzwa iwe paradiso itakayokuwa na amani na usalama. (Zaburi 37:9-11; 46:8, 9) Wakati ujao huo ni hakika kwa sababu Muumba mweza-yote atatimiza ahadi zake. (Isaya 55:11) Lakini kupokea kwetu baraka ya uhai katika Paradiso hakujaamuliwa kimbele: kunategemea kufanya kwetu mapenzi ya Mungu kwa utii sasa. (2 Wathesalonike 1:6-8; Ufunuo 7:14, 15) Mungu ametupa hiari naye anatutia moyo hivi: “Chagua uzima, ili uwe hai.” (Kumbukumbu la Torati 30:19) Wewe utachagua nini? Ni juu yako kuchagua wakati wako ujao wala hautegemei kuamuliwa kimbele.

[Picha katika ukurasa wa 10]

Mungu amekusudia wakati ujao ajabu kwa wanadamu watiifu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki