Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g99 9/8 kur. 9-10
  • Uhai Ulianzaje?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uhai Ulianzaje?
  • Amkeni!—1999
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Tumeumbwa kwa Njia ya Ajabu
  • Ushirikiano wa Molekuli Wenye Kuendeleza Uhai
    Je, Kuna Muumba Anayekujali?
  • Maagizo Yalitoka Wapi?
    Maswali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai
  • Kuchunguza Chembe kwa Hadubini
    Amkeni!—1999
  • Chunguza Uthibitisho
    Amkeni!—2011
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1999
g99 9/8 kur. 9-10

Uhai Ulianzaje?

MOLEKULI ya DNA hutekeleza mambo ya kustaajabisha. DNA hutimiza mambo mawili yanayohitajiwa na chembe zako katika kufanyiza visehemu vya urithi. Kwanza, DNA hunakiliwa sawasawa ili habari iweze kupitishwa kutoka kwa chembe moja hadi nyingine. Pili, mfuatano wa DNA husaidia chembe kujua aina ya protini itakayofanyiza, na hivyo kuamua chembe hiyo itakuwa ya aina gani na kazi itakayofanya. Hata hivyo, DNA haitekelezi kazi hizi bila msaada. Protini nyingi za kipekee huhusika.

DNA peke yake haiwezi kutokeza uhai. Ina maagizo yote yanayohitajiwa ili kufanyiza protini zote zinazohitajiwa na chembe hai, kutia ndani zile zinazonakili DNA kwa ajili ya kizazi kingine cha chembe na zile zinazosaidia DNA kufanyiza protini mpya. Ingawa hivyo, habari chungu nzima iliyohifadhiwa katika chembe za urithi za DNA ni bure pasipo RNA na protini za kipekee, zinazotia ndani ribosomu, zinazohitajiwa ili “kusoma” na kutumia habari hiyo.

Wala protini peke yake haziwezi hutokeza uhai. Protini iliyo peke yake haiwezi kutokeza chembe ya urithi iliyo na maagizo ya kufanyiza protini za aina ileile.

Kwa hiyo, kufumbua fumbo la uhai kumeonyesha nini? Elimu ya kisasa ya chembe za urithi na biolojia ya molekuli imetoa uthibitisho wa kutosha wa uhusiano ulio tata sana wenye kutegemeana kati ya DNA, RNA, na protini. Matokeo haya yanaonyesha kwamba uhai hutegemea kuwapo kwa elementi hizi zote kwa wakati mmoja. Hivyo, uhai haungeweza kamwe kutokea tu ghafula kwa nasibu.

Maelezo pekee yanayopatana na akili ni kuwa Muumba mwenye akili sana aliweka maagizo katika DNA na wakati uleule akifanyiza protini zilizo kamili. Utendeano huo ulibuniwa kwa njia bora hivi kwamba mara tu baada ya kubuniwa, utendaji huu ungehakikisha kwamba protini zingeendelea kunakili DNA na kutokeza chembe zaidi za urithi, huku protini nyingine zikifasiri chembe hizi za urithi ili kufanyiza protini zaidi.

Kwa wazi, utaratibu huu wa uhai wenye kustaajabisha ulianzishwa na Mbuni Mkuu, Yehova Mungu.

Tumeumbwa kwa Njia ya Ajabu

Ijapokuwa Biblia si kitabu cha kisayansi, inafunua mambo fulani kuhusu fungu la Muumba, aliyebuni maagizo ya uhai. Miaka elfu tatu hivi iliyopita, Mfalme Daudi wa Israeli, asiyejua lolote juu ya maendeleo ya kisasa katika utafiti wa urithi, alimwimbia hivi Muumba wake kwa lugha ya kishairi: “Ni wewe ndiwe uliyeumba mtima wangu, na kuniunganisha pamoja tumboni mwa mama yangu; ninakushukuru kwa sababu ya maajabu haya yote: kwa sababu ya umbo langu la ajabu, kwa sababu ya maajabu ya kazi zako. Unanijua kabisa, kwa kuwa uliona mifupa yangu ikiumbika nilipokuwa nikiumbwa kwa siri, nikishikanishwa pamoja ndani ya tumbo la uzazi.”—Zaburi 139:13-15, Jerusalem Bible.

Hebu jiangalie sana katika kioo kwa muda tena. Angalia rangi ya macho yako, umbile la nywele zako, rangi ya uso wako, na umbo la ujumla la mwili wako. Fikiria jinsi mambo hayo yalivyorithiwa kutoka kwa vizazi vilivyopita na jinsi yanavyopitishwa kwa uzao wako. Sasa, fikiria Yule aliyepanga utaratibu huu wa kustaajabisha. Huenda ukasukumwa kurudia maneno yaliyoandikwa na mtume Yohana: “Wewe wastahili, Yehova, naam, Mungu wetu, kupokea utukufu na heshima na nguvu, kwa sababu uliumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako na vikaumbwa.”—Ufunuo 4:11.

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 10]

Je, Ilitokana na Nasibu Tu?

Uchunguzi uliofanywa hivi karibuni na wanasayansi wawili Waingereza unathibitisha kwamba msimbo wa urithi haukutokana na nasibu bila utaratibu maalum. “Uchunguzi wao umeonyesha kwamba [msimbo wa chembe za urithi] ni mojawapo ya misimbo bora kati ya mabilioni ya misimbo inayoweza kuwapo,” lasema gazeti New Scientist. Ni msimbo mmoja tu kati ya misimbo ya chembe za urithi takriban 1020 (1 ikifuatwa na sufuri 20) inayoweza kuwapo, uliochaguliwa mapema sana katika historia ya uhai. Mbona huu msimbo mahususi ukachaguliwa? Kwa sababu unapunguza kasoro zinazozuka wakati wa utengenezaji wa protini au kasoro zinazosababishwa na mabadiliko ya chembe za urithi. Yaani, msimbo huu hususa wa chembe za urithi unahakikisha kwamba sheria za urithi zinafuatwa kabisa. Ijapokuwa watu fulani hudai kwamba kuchaguliwa kwa msimbo huu kulitokana na “misongo yenye nguvu ya kuchagua,” watafiti hao wawili wamekata kauli kwamba “ni jambo lisilowezekana kabisa kwamba msimbo huu bora ulitokana na nasibu.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki