Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g01 11/22 uku. 31
  • Mti Mkubwa Unaoitwa Tule

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mti Mkubwa Unaoitwa Tule
  • Amkeni!—2001
  • Habari Zinazolingana
  • Ukurasa wa Pili
    Amkeni!—2001
  • “Mti wa Uhai” Wenye Kushangaza wa Afrika
    Amkeni!—1995
  • Kutumikia kwa Moyo Wote Licha ya Majaribu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Waazteki wa Kisasa Wajifunza na Kuwa Wakristo wa Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Amkeni!—2001
g01 11/22 uku. 31

Mti Mkubwa Unaoitwa Tule

NA MWANDISHI WA AMKENI! NCHINI MEXICO

MITI mirefu kushinda miti mingine yote ulimwenguni ni miti aina ya mvinje iitwayo redwood huko California, inayoweza kufikia urefu wa meta 110 au zaidi. Hata hivyo, mti wa mvinje wa Mexico, wa jamii ya sequoia, una mzingo mkubwa kuliko miti mingine yote. Mti maarufu zaidi wa aina hiyo unakua umbali wa kilometa 13 mashariki ya jiji la Oaxaca, Mexico, katika mji uitwao Santa María del Tule. Mti huo unaitwa mti wa Tule. Sehemu ya chini ya shina lake ina mzingo wa meta 46. Angalau watu 30 walionyoosha kabisa mikono yao wangehitajika ili kuzunguka kabisa shina lake, na watu zaidi ya 500 wangeweza kupata kivuli chini ya matawi yake!

Inakadiriwa kwamba mti huo una umri wa zaidi ya miaka 2,000. Matawi makavu ya mti huo yaliyokatwa mwaka wa 1996 yalikuwa na uzito wa kilogramu 10,000. Wenyeji wanauita mti huo El Gigante (Jitu). Nchini Mexico jamii hiyo ya mti inaitwa ahuehuete, maana yake katika Kinahuatl ni “mzee wa maji,” kwa kuwa mara nyingi mti huo hukua karibu na maji au katika vinamasi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki