Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g03 8/22 uku. 16
  • Maelezo Mafupi Kuhusu Kikundi cha Kidini

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maelezo Mafupi Kuhusu Kikundi cha Kidini
  • Amkeni!—2003
  • Habari Zinazolingana
  • Filipo—Mweneza-Evanjeli Mwenye Bidii
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Kutangaza “Habari Njema Kumhusu Yesu”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
  • Onyesha Roho ya Upainia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Kuzungumza kwa Njia ya Kawaida
    Wapende Watu—Fanya Wanafunzi
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2003
g03 8/22 uku. 16

Maelezo Mafupi Kuhusu Kikundi cha Kidini

Philip mwenye umri wa miaka 15, alipewa mgawo wa kuchunguza na kutoa ripoti juu ya michezo, siasa, utamaduni, au vikundi vya kidini katika Sydney, jiji lake la nyumbani, nchini Australia. Mgawo huo ulikuwa sehemu ya somo lake la jiografia katika shule ya sekondari. Philip aliamua kuandika ripoti kuhusu kutaniko la Mashahidi wa Yehova, ambapo yeye na familia yake hushiriki. Wanafunzi hao waliagizwa wazungumze na washiriki 20 wa kikundi walichochagua ili kupata, miongoni mwa mambo mengine, habari fupi kuhusu “sifa mbalimbali za kikundi hicho.”

Baada ya kukusanya matokeo ya uchunguzi wake, Philip aliandika hivi: “Kutaniko la Mashahidi wa Yehova ni tengenezo la kidini linalokutana hasa kwa kusudi la kujifunza Biblia. Wakati wa mikutano hiyo, maandiko ya Biblia husomwa kisha hufafanuliwa. Mikutano hiyo pia hukusudia kutufundisha njia bora zaidi ya kuwafundisha wengine kuhusu Biblia. Jambo hilo hufanywa kwa kuwatembelea watu nyumbani kwao ambapo wao huwa wamestarehe. Washiriki wote wa kikundi hicho hushiriki katika kazi hiyo kwa kawaida, kwa viwango mbalimbali, kulingana na hali zao. Zaidi ya kujifunza Biblia wenyewe na kuwafundisha wengine, kikundi hicho pia husaidia kugawia watu majarida ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!, ambayo huwa na makala zenye kupendeza kuhusu mambo ya asili, historia, na masuala ya ulimwengu na yale yanayotuhusu. Pia sisi hujitahidi kuwategemeza watu walioshuka moyo baada ya misiba mibaya ya ulimwengu, kama vile msiba wa Septemba 11, nasi huwapa vichapo vya kuwasaidia vinavyozungumzia mambo kama vile ndoa, maisha ya familia, na vijana.”

Kwa sababu ya kiwango cha uchunguzi wake na jinsi alivyotoa ripoti yake, Philip alipata alama ya juu zaidi. Ikiwa ungependa kujifunza mengi zaidi kuhusu kazi ambayo hufanywa na Mashahidi wa Yehova, zungumza nao wakati ujao watakapokutembelea au uwasiliane nao kwa kutumia anwani iliyo karibu nawe iliyoorodheshwa katika ukurasa wa 5.

[Picha katika ukurasa wa 16]

Philip

[Picha katika ukurasa wa 16]

Italia

[Picha katika ukurasa wa 16]

Australia

[Picha katika ukurasa wa 16]

Brazili

[Picha katika ukurasa wa 16]

Uholanzi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki