Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/04 uku. 8
  • Onyesha Roho ya Upainia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Onyesha Roho ya Upainia
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari Zinazolingana
  • Filipo—Mweneza-Evanjeli Mwenye Bidii
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Kutangaza “Habari Njema Kumhusu Yesu”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
  • Baraka za Huduma ya Painia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Je! Wewe Una Roho ya Upainia?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1988
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 8/04 uku. 8

Onyesha Roho ya Upainia

1 Wahubiri wote wa Ufalme wanaweza kuonyesha roho ya upainia, iwe wanaweza kutumika wakati huu kama mapainia au la. Wanapenda sana kutii amri ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. (Mt. 28:19, 20; Mdo. 18:5) Wanawajali watu, nao hujitolea ili watimize huduma yao. (Mt. 9:36; Mdo. 20:24) Watumishi wa Yehova wako tayari kufanya yote yanayohitajiwa ili kuwasaidia wengine wajifunze kweli. (1 Kor. 9:19-23) Na tuchunguze mfano wa mtumishi mmoja aliyeonyesha roho hiyo, yule mweneza-injili Filipo.

2 Kuhubiri na Kufundisha: Filipo alishughulikia madaraka mazito katika kutaniko la karne ya kwanza. (Mdo. 6:1-6) Lakini, hasa alikuwa mhubiri mwenye bidii wa habari njema. (Mdo. 8:40) Vivyo hivyo leo, wazee na watumishi wa huduma wanaposhughulikia wajibu wao mbalimbali, wanaweza kuonyesha roho ya upainia kwa kuongoza katika huduma kwa uchangamfu. Hilo huchochea roho ya kutaniko kama nini!—Rom. 12:11.

3 Baada ya kifo cha Stefano, mateso ya ghafla yalisababisha msukosuko mkubwa katika maisha ya wanafunzi. Hata hivyo, Filipo aliendelea kuhubiri naye akatimiza sehemu muhimu ya kufungua njia kwa ajili ya Wasamaria. (Mdo. 8:1, 4-6, 12, 14-17) Tunaweza kumwiga kwa kuendelea kujulisha wengine habari njema tunapojaribiwa na kwa kuhubiria wote tunaokutana nao bila ubaguzi.—Yoh. 4:9.

4 Ustadi wa Filipo akiwa mwalimu wa Neno la Mungu unaweza kuonekana katika simulizi la kugeuka imani kwa towashi Mwethiopia. (Mdo. 8:26-38) Kusitawisha uwezo wa kutumia Biblia na ‘kujadiliana kwa kutumia Maandiko’ ni njia nyingine pia ya kuonyesha kwamba tuna roho ya upainia. (Mdo. 17:2, 3) Kama Filipo, tunajitahidi kuwahubiria watu habari njema popote pale tutakapowapata na wakati wowote ule unaofaa.

5 Familia na Kutaniko: Mtazamo wa Filipo na kielelezo chake bila shaka kiliwachochea binti zake. (Mdo. 21:9) Vivyo hivyo, wazazi Wakristo ambao wanafuatia zaidi mambo ya Ufalme, huwatia moyo watoto wao wafanye vivyo hivyo. Ajapokuwa amechoka mwishoni mwa juma, mzazi anayewahubiria wengine kwa bidii anaweza kumwekea mtoto wake mfano wenye kudumu.—Met. 22:6.

6 Filipo aliwaalika Paulo na Luka nyumbani kwake, ambao walikuwa Wakristo wenye juhudi waliofanya kazi kwa bidii katika utumishi wa Yehova. (Mdo. 21:8, 10) Tunaweza kuonyeshaje shukrani na kuwaunga mkono wale wenye bidii leo? Labda tunaweza kujitolea kuhubiri na mapainia asubuhi au alasiri moja katika siku ambayo watu wengi hawaendi kwenye huduma. (Flp. 2:4) Pia tunaweza kuwaalika nyumbani mwetu tuwe na ushirika wenye kutia moyo. Hata hali zetu ziwe zipi, sisi sote na tujitahidi kuonyesha roho ya upainia.

[Maswali ya Funzo]

1. Fafanua roho ya upainia.

2. Wazee na watumishi wa huduma wanaweza kuigaje bidii ya Filipo katika huduma?

3. Tunawezaje kuonyesha roho ya upainia tunapokabili majaribu?

4. Filipo aliweka kielelezo gani akiwa mwalimu?

5. Ni nini kinachoweza kuwasaidia wazazi Wakristo wawatie moyo watoto wao wawe na roho ya upainia?

6. Tunawezaje kuonyesha shukrani kwa mapainia katika kutaniko letu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki