Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/88 kur. 1-2
  • Je! Wewe Una Roho ya Upainia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Wewe Una Roho ya Upainia?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • JINSI YA KUSITAWISHA ROHO YA UPAINIA
  • MATOKEO CHANYA
  • Kutembea kwa Nafsi Yote katika Njia ya Uzima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1975
  • Baraka za Huduma ya Painia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Je! Waweza Kumtumikia Yehova Ukiwa Painia?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Painia Ni Nani?
    Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 7/88 kur. 1-2

Je! Wewe Una Roho ya Upainia?

1 “Roho ya upainia” ni nini? Huenda ikafasiliwa kuwa na mwelekeo chanya kuelekea amri ya kuhubiri na kufanya wanafunzi, kujitia kabisa katika kuonyesha upendo na hangaikio kwa watu, kuwa mwenye kujidhabihu, kupata shangwe katika kufuata Bwana-Mkubwa kwa ukaribu, na kupendezwa si na vitu vya kimwili, bali vya kiroho.

2 Kwa uhakika watu wa Yehova kwa ujumla wanadhihirisha roho hii leo. Hata wanapokabili minyanyaso mikali na maafa mengine, kwa shangwe wanasonga mbele katika kutangaza habari njema za Ufalme wa Mungu. Ile shangwe inayotokana na kuhubiri habari njema kwa bidii inaonekana na kuhisiwa hasa tunapohudhuria mikusanyiko ya wilaya na makusanyiko mengine makubwa ya watu wa Mungu. Roho inayodhihirishwa katika pindi hizo inatujaza bidii kubwa zaidi, tuwe sisi ni wahubiri au mapainia.

3 Hata hivyo, kuishi kama tunavyoishi ndani kabisa ya wakati wa mwisho, wasiwasi na mikazo ya maisha ya kila siku inaweza kuathiri mtu katika njia fulani, labda ikipunguza bidii na idili yetu kwa mambo ya kiroho. Kila mtu anaweza kujiuliza mwenyewe, ‘Je! mimi nina roho ya upainia? Je! mimi ninaruhusu mfumo huu wa mambo uninyanganye hiyo? Je! mimi nina bidii kwa ajili ya ukweli, nikiwa na hamu nyingi ya kuwaambia wengine juu ya Ufalme wa Mungu? Je! mimi ninaendeleza roho ya upainia katika kundi na kuwatia moyo wengine kujihusisha kikamili katika kufanya penzi la Mungu? Ninaweza kufanya nini ili nishinde mwelekeo hasi au ubaridi?

JINSI YA KUSITAWISHA ROHO YA UPAINIA

4 Roho ya upainia kwa kawaida inategemea hali ya moyoni, na ni lazima tuisitawishe. Kwa kuwa tunalisha moyo mambo tunayosoma na kusikiliza, funzo la kibinafsi la Biblia lina sehemu ya maana sana katika kusitawisha kwetu roho ya upainia. Paulo alimsihi Timotheo: “Uyatafakari hayo . . . ili kuendelea kwako kuwe dhahiri kwa watu wote. . . . Dumu katika mambo hayo; maana kwa kufanya hivyo utajiokoa nafsi yako na wale wakusikiao pia.” (1 Tim. 4:15, 16) Basi, inahitajiwa sana kwetu sisi kutafakari juu ya mambo ya kiroho ili kuyaingiza ndani ya moyo wetu, ulio kao la msukumo. Kwa kufanya hivyo tutasitawisha hamu ya kutaka kufanya mapenzi ya Mungu. Kuthamini kwetu mambo ya kiroho kutakuwa kwenye kina kirefu, nasi tutatafuta njia za kupanua huduma yetu.

5 Mambo tunayozungumza yanaweza kuvunja ndugu zetu au kuwajenga. (Efe. 4:29) Kwa kushiriki mambo yaliyoonwa shambani na mambo tuliyofurahia mikutanoni au katika funzo la kibinafsi, tunaingiza mawazo ambayo ni chanya na yenye kutia moyo. Kwa kuongezea, tunapokuwa na pindi ya kuzungumza pamoja na watu katika kawaida ya maisha yetu ya kila siku je! sisi tunatafuta fursa za kuwatolea ushuhuda wa vivi hivi? Tukifanya hivyo, tunafuata nyayo za Kiolezo chetu, Yesu.—Yn. 4:7-10.

6 Kusitawisha upendo kwa jirani kunatusaidia kusitawisha roho ya upainia. (Mt. 22:39) Yesu alionyesha upendo wa aina hii alipokuwa duniani. Yeye alihisi huruma kwa ajili ya watu na alitaka kufanya yote ambayo angeweza ili awasaidie, ijapokuwa hiyo ilimaanisha kujidhabihu sana. (Mt. 9:36; Rum. 5:6) Tukionyesha mwelekeo kama wa Kristo, tutasukumwa na huruma na kufanya yote tuwezayo ili kusaidia jirani zetu kiroho, hata wengine wakitukataa.—Linganisha Mathayo 23:37.

MATOKEO CHANYA

7 Kuna baraka na manufaa nyingi zinazotokana na kudhihirisha roho ya upainia katika maisha zetu. Tunapoongeza utendaji wetu katika huduma, tunakuwa walimu wenye matokeo zaidi, na jambo hilo linaweza kutuletea shangwe kubwa. Roho ya upainia inapoendelea kuongezeka katika kundi, ndivyo na uchangamshi na hali ya kiroho ya akina ndugu. Kuhusu matokeo yenye kujenga ambayo utumishi wa painia umekuwa nayo kwa kundi lake, mzee mmoja alisema hivi: “Ulitokeza tofauti kubwa sana! Mwendo wa kundi ulibadilika. Maelekeo sasa ni kuongeza ushirika wetu zaidi na zaidi katika utumishi wa Yehova.”—Ona Mnara wa Mlinzi, Septemba 15, 1985, ukurasa 21, fungu 1.

8 Mwaka wa utumishi wa 1989 unapokaribia, azimia kusitawisha roho ya upainia katika kundi. Angalia-angalia njia za kupanua huduma yako. Panga kimbele ili ufanye upainia msaidizi iwezekanapo, au labda ufikie utumishi wa painia wa kawaida. Wawe mapainia au wahubiri, wote kundini wanaweza kuwa na roho ya upainia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki