Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 8/09 uku. 29
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
  • Amkeni!—2009
  • Habari Zinazolingana
  • Kuna ubaya gani kutumia matusi?
    Amkeni!—2008
  • Yaliyomo
    Amkeni!—2008
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—1994
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—2005
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2009
g 8/09 uku. 29

Kutoka kwa Wasomaji Wetu

Vijana Huuliza . . . Kuna Ubaya Gani Kutumia Matusi? (Machi 2008) Nililelewa na wazazi Wakristo, lakini nilianza kuwa na mazoea ya kutumia matusi. Nilijaribu sana kuacha bila mafanikio. Hata hivyo, makala hii ilinisaidia kujizuia. Kama ilivyotajwa katika makala hiyo, sitaki kutumia vibaya zawadi ya usemi. Kwa hiyo sasa ninafikiria maneno yangu kwa uangalifu kabla ya kuzungumza. Asanteni sana.

C. P., Brazili

Nina umri wa miaka 12. Ninazungukwa na watu wanaotumia matusi shuleni, na ninaogopa kwamba siku moja nitamtukana mtu bila kutarajia. Nilikuwa karibu kuwaandikia nikiomba mwandike makala ya “Vijana Huuliza” kuhusu jambo hilo ndipo makala hiyo ikachapishwa katika Amkeni! Makala hiyo ilinikumbusha kwa nini ni vibaya kutukana, na iliniimarisha. Endeleeni kuandika makala kama hizo!

A. P., Marekani

Mimi na mume wangu hujiruzuku kwa kusafisha nyumba za watu, na mmoja wa wateja wetu alituambia kwamba “azimio [lake] la mwaka mpya” lilikuwa kuacha kutumia matusi. Alisema kwamba anasali kila siku, akimwomba Mungu amsaidie aache mazoea yake mabaya. Pia aliniambia nimpe kichapo chochote kinachozungumzia jambo hilo. Nilisali kuhusu jambo hilo na kisha, kama kawaida, nilitoa magazeti ya karibuni kutoka kituo chetu cha Intaneti www.jw.org na kuyaweka katika kifaa cha MP3. Unaweza kuwazia jinsi siku iliyofuata nilivyofurahi niliposikiliza ukurasa wa pili na kujua mambo yaliyo katika wa gazeti hilo. Nilisisimuka sana! Ingawa makala hiyo iliandikwa kwa ajili ya vijana, nilijua kwamba mteja huyo angepata mashauri yanayofaa. Nilitamani sana kumpa gazeti hilo.

S. C., Marekani

Kuongoza Ndege Kunakulindaje? (Aprili 2008) Nilisema kwamba sasa “niko salama na tayari kwa safari” baada ya kusoma makala hiyo. Nilitiwa moyo na kuhisi salama zaidi kwa sababu gazeti Amkeni! lilinionyesha kwamba waongozaji wa ndege wanapendezwa sana na usalama wetu. Asanteni.

T. S., Brazili

Ungejibuje? Nina umri wa miaka 12 na ninaishi kusini mwa Ireland. Ningependa kuwashukuru kwamba maswali ya pekee kwa ajili ya watoto kurasa za nyuma za Amkeni! Makala hizo zinapendeza. Zinafanya watoto wafurahie gazeti. Tafadhali endeleeni kuziandika. Asanteni tena.

A. C., Ireland

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki