Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 7/10 kur. 26-27
  • “Viziwi Wanafaidika kwa Kujifunza Biblia”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Viziwi Wanafaidika kwa Kujifunza Biblia”
  • Amkeni!—2010
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Yehova Ameufanya Uso Wake Ung’ae Kuwaelekea’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Wathamini Ndugu na Dada Zako Viziwi!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Uwe Macho Kutafuta Viziwi Katika Eneo Lenu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Kusikiliza kwa Macho Yako
    Amkeni!—1998
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2010
g 7/10 kur. 26-27

“Viziwi Wanafaidika kwa Kujifunza Biblia”

HABARI iliyokuwa na kichwa hicho ilichapishwa katika gazeti moja la viziwi katika Jamhuri ya Cheki. Zdeněk Straka, aliyeandika habari hiyo, aliwasifu Mashahidi wa Yehova ambao wamejifunza lugha ya ishara ili wawasaidie viziwi.

Ni nini kilichomchochea Bw. Straka kuandika habari hiyo? Katika mwaka wa 2006, alihudhuria kusanyiko la Mashahidi wa Yehova huko Prague, ambako programu ilitafsiriwa katika lugha ya ishara kwa ajili ya viziwi 70 hivi waliohudhuria. Kila mwaka, Mashahidi wa Yehova huwa na makusanyiko ulimwenguni pote ili kutoa elimu ya Biblia na ushirika wenye kujenga. Viziwi hawasahauliwi. Mwaka mmoja hivi karibuni, makusanyiko 96 yalifanywa katika lugha ya ishara ulimwenguni pote na programu hiyo ilitafsiriwa kwa ajili ya viziwi katika maeneo mengine 95.

Wakati wa kusanyiko hilo huko Prague, kutaniko la lugha ya ishara katika jiji hilo lilikuwa likiwafundisha viziwi 30 hivi Biblia. Wale wanaojifunza Biblia wanafaidika kama kisa kifuatacho kinavyoonyesha.

Markéta husafiri zaidi ya kilomita 100 kila juma ili ajifunze Biblia na mwanamke kiziwi kutoka Mongolia. Lugha ya ishara ya Kicheki na ya Kimongolia zinatofautiana, kwa hiyo, Markéta anahitaji kuwa mbunifu ili mwanafunzi wake aelewe kile anachofundishwa. Hata hivyo, jitihada za Markéta hazijaambulia patupu. Kwa kuwa mwanafunzi huyo alikuwa mjamzito kwa mara ya pili, alikuwa akifikiria kutoa mimba lakini akabadili maoni yake. Markéta anasema hivi, “Nilipomwuliza kwa nini alibadili maoni yake, alinijibu hivi kwa lugha ya ishara, ‘Yehova huchukizwa watu wanapotoa mimba.’ Nilifurahi kuona kwamba alielewa maoni ya Mungu kuhusu uhai!”a

Ulimwenguni pote, viziwi wengi wanapata ujuzi sahihi kumhusu Mungu kwa kujifunza Neno lake. Wanapomkaribia Mungu wao na kupata shangwe zaidi maishani, maisha yao yanakuwa bora zaidi.—Isaya 48:17, 18.

[Maelezo ya Chini]

a Ili upate habari zaidi kuhusu maoni ya Biblia juu ya utoaji-mimba, ona gazeti Amkeni! la Juni (Mwezi wa 6) 2009, ukurasa wa 3-9.

[Sanduku katika ukurasa wa 26, 27]

JE, WAJUA?

● Mashahidi wa Yehova hutokeza DVD katika lugha 43 za ishara. Habari kwa ajili ya viziwi inaweza pia kupakuliwa kwenye Tovuti ya www.jw.org.

● Ili kutokeza vichapo zaidi kwa ajili ya viziwi, Mashahidi wa Yehova wamepanga vikundi 59 vya kutafsiri katika lugha ya ishara ulimwenguni pote.

● Ulimwenguni pote, kuna zaidi ya makutaniko 1,200 ya Mashahidi wa Yehova ya lugha ya ishara.

[Mchoro katika ukurasa wa 26]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

www.jw.org

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki