Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 1/11 uku. 6
  • Kwa Nini Dini Haijawaunganisha Wanadamu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Dini Haijawaunganisha Wanadamu?
  • Amkeni!—2011
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kugawanywa na Dini
  • Dini Imejiingiza Katika Siasa
  • Mchanganyiko Unaoweza Kutokeza Madhara
  • Nani Anayependezwa na Dini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Je! Dini Yoyote Ni Nzuri vya Kutosha?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Je, Dini Itawahi Kuleta Amani?
    Amkeni!—2011
  • Jinsi Dini za Uwongo Zinavyopotosha Ukweli Kumhusu Mungu
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2011
g 1/11 uku. 6

Kwa Nini Dini Haijawaunganisha Wanadamu?

IKIWA tungesema kwamba dini ndiyo chanzo cha mizozo yote ingemaanisha kwamba iwapo hakungekuwa na dini hakungekuwa na vita vingi. Je, wazo hilo linapatana na akili? Je, tunaweza kumaliza vita kwa kuondoa dini zote? Vyovyote vile utakavyojibu, jambo moja ni hakika: Dini haijawaunganisha wanadamu. Fikiria sababu fulani kwa nini hilo ni kweli.

Kugawanywa na Dini

Wanadamu wamegawanywa na dini, kwa kuwa dini nyingi kuu zimekuwa na chuki ya muda mrefu. Je, kuna sababu ya kuamini kwamba Wabudha, Wahindu, Waislamu, Wakristo, na Wayahudi watawahi kuishi pamoja kwa amani?

Jambo lingine lenye kusikitisha ni kwamba dini hizo kuu zimegawanyika katika vikundi vidogo-vidogo. Kwa mfano, kulingana na kadirio moja, dini zinazodai kuwa za Kikristo zimegawanyika katika vikundi zaidi ya 30,000. Dini ya Kiislamu pia imegawanywa na mafundisho yanayopingana. Kulingana na shirika moja la habari la Mashariki ya Kati, msomi Mwislamu, Mohsen Hojjat hivi majuzi alikiri kwamba “ukosefu wa umoja kati ya Waislamu ndio unaosababisha matatizo yanayowakabili Waislamu kwa ujumla.” Dini nyingine maarufu kama zile za Wabudha, Wahindu, na Wayahudi zimegawanyika katika madhehebu mengi yanayopingana.

Dini Imejiingiza Katika Siasa

Inaonekana kwamba dini ina uvutano katika karibu kila sehemu ya maisha. Gazeti la habari The Economist linasema kwamba “watu wa kidini wanaeleza waziwazi imani yao katika nyanja zote kutia ndani nyanja ya biashara. Dini pia inaathiri maamuzi ya watu hata katika mambo ya kifedha.” Jambo hilo limewagawanya watu badala ya kuwaunganisha. Lakini uvutano mkubwa zaidi unaoleta madhara unahusiana na historia ndefu ya dini kujiingiza katika siasa.

Katika ripoti ya hivi majuzi iliyotajwa katika habari iliyotangulia, kikundi cha wanahistoria kilisema kwamba “yaelekea dini inaweza kusababisha vita ikiwa dini na serikali zitashirikiana kwa ukaribu au kuungana.” Ukweli wa mambo ni: Dini imekuwa ikijiingiza, na hata sasa bado inajiingiza, katika mashirika ya kisiasa na kijeshi.

Mchanganyiko Unaoweza Kutokeza Madhara

Katika nchi nyingi, dini kubwa zimekuwa njia ya kutambulisha uzalendo au rangi ya mtu. Kwa sababu hiyo, si rahisi kutofautisha chuki ya kitaifa, ubaguzi wa rangi, mizozo ya kikabila, na chuki ya kidini. Mchanganyiko huo unaweza kuharibu kabisa mambo ya ulimwengu huu.

Jambo lenye kupingana ni kwamba dini nyingi hudai kumwakilisha yule Mungu wa Biblia, Muumba. Je, inapatana na akili kwamba Muumba mweza-yote, mwenye hekima yote, na mwenye upendo anaweza kujihusisha kwa njia yoyote na dini zenye kutokeza mgawanyiko na umwagaji wa damu?

[Picha katika ukurasa wa 6]

Maelfu ya Mashahidi wa Yehova wamefungwa kwa sababu ya kuchagua kutounga mkono upande wowote wa kisiasa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki