Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g18 Na. 2 uku. 11
  • 8 Kielelezo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • 8 Kielelezo
  • Amkeni!—2018
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MAANA YAKE
  • KWA NINI NI MUHIMU
  • MAMBO YA KUFANYA
  • Kulea Watoto Wenye Furaha Katika Ulimwengu Wenye Mchafuko Mwingi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Je, Biblia Inaweza Kukusaidia Kulea Watoto Wako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Wazazi—Wasaidieni Watoto Wenu Wampende Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Je! Wewe Unafundisha Watoto Wako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2018
g18 Na. 2 uku. 11

KWA WAZAZI

8 Kielelezo

MAANA YAKE

Wazazi huweka kielelezo kwa kuishi kulingana na yale wanayofundisha. Kwa mfano, huwezi kutarajia mtoto wako awe msema kweli ikiwa amekusikia ukisema, “Mwambie sipo,” wakati ambapo hutaki kuongea na mgeni aliye mlangoni.

“Wazazi hawapaswi kutarajia watoto wafanye kile wanachowaambia ikiwa wao wenyewe wanatenda kinyume. Watoto hufyonza kila kitu tunachosema au kufanya, nao watatuambia ikiwa matendo yetu hayaendani na kile tunachowafundisha.”—David.

KANUNI YA BIBLIA: “Wewe unayehubiri, ‘Usiibe,’ je, wewe huiba?”​—Waroma 2:21.

KWA NINI NI MUHIMU

Kielelezo cha wazazi kwa watoto wao na hata vijana kina nguvu sana kuliko maneno au matendo ya mtu mwingine yeyote, kutia ndani watoto au vijana wenzao. Hilo linamaanisha kwamba unachangia sehemu kubwa sana katika kuwaongoza watoto wako kwenye njia inayofaa, na bila shaka hiyo itawezekana ikiwa tu unatenda kulingana na yale unayofundisha.

“Huenda ukamwambia mtoto jambo fulani mara nyingi na usiwe na uhakika ikiwa kweli anakuelewa, lakini ukitenda kinyume na ulichosema hata mara moja tu, mtoto atakuambia. Watoto huona kila kitu tunachofanya, hata tunapohisi hawaelewi.”—Nicole.

KANUNI YA BIBLIA: “Hekima inayotoka juu . . . si ya kinafiki.”​—Yakobo 3:17.

MAMBO YA KUFANYA

Jichunguze. Wewe hutazama sinema au miziki ya aina gani? Unamtendeaje mwenzi wako na watoto wako? Rafiki zako ni watu wa aina gani? Je, unawajali wengine? Kwa ufupi, ukifikiria jinsi unavyotaka watoto wako wawe, je, hivyo ndivyo wewe ulivyo?

“Mimi na mume wangu hatuwalazimishi watoto wetu kuishi kupatana na kanuni ambazo sisi wenyewe hatufuati.”—Christine.

Omba msamaha unapokosea. Watoto wako wanajua kwamba wewe si mkamilifu. Ukikosea na kumwambia mwenzi wako na watoto “samahani,” utakuwa ukiwafundisha kuwa wanyoofu na wanyenyekevu—sifa muhimu sana maishani.

“Watoto wetu wanahitaji kusikia tukikubali makosa yetu na kuomba msamaha. Tusipofanya hivyo, hawatajifunza kukubali wanapokosea.”—Robin.

“Tukiwa wazazi, tunachangia sehemu kubwa sana kuhusiana na jinsi watoto wetu watakavyokuwa, na mfano wetu ndio kifaa kikuu tulicho nacho kwa sababu wanauona muda wote. Ni kana kwamba wanafundishwa kila wakati kutokana na jinsi sisi wazazi tunavyoishi.”—Wendell.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki