Utangulizi
Kila mmoja wetu ameathiriwa kwa kadiri fulani na matatizo makubwa kama vile ugonjwa, aksidenti, majanga ya asili au kutendewa kwa jeuri.
Watu wanahangaika kutafuta majibu.
Baadhi ya watu wanaamini kwamba kuteseka ni mipango ya Mungu au wanahisi hatuwezi kuzuia mambo yanayotupata.
Wengine wanaamini tunateseka kwa sababu ya mambo tuliyofanya zamani kabla ya kuzaliwa upya.
Matatizo makubwa yanapotokea, watu hujiuliza maswali mengi sana.