Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g20 Na. 3 kur. 6-7
  • Uwe na Huruma

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uwe na Huruma
  • Amkeni!—2020
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Tatizo
  • Kanuni ya Biblia
  • Kuwa na Huruma Kunaweza Kutusaidiaje?
  • Mambo Unayoweza Kufanya
  • Hisia-Mwenzi—Hutusaidia Kudhihirisha Fadhili na Huruma
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
  • Onyesha Hisia-Mwenzi
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2021
  • Je, Mungu Huhisi Maumivu Yako?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2018
  • Kuboresha Uhusiano wa Familia na Marafiki
    Amkeni!—2019
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2020
g20 Na. 3 kur. 6-7
Mwanamume Mzungu na Mkalasinga wakiwa wameketi pamoja ndani ya ndege. Wanazungumza kwa furaha.

Uwe Na Huruma

Tatizo

Tukikazia sana jinsi wengine walivyo tofauti na sisi, huenda tukaona tofauti hizo kuwa udhaifu au mapungufu. Kwa sababu ya tofauti hizo, tunaweza kuanza kuwaona wengine kuwa duni. Tunapositawisha mtazamo huo mbaya, inaweza kuwa vigumu kuwaonyesha wengine huruma. Kutokuwa na huruma kunaweza kuwa dalili ya tatizo kubwa zaidi, yaani, ubaguzi.

Kanuni ya Biblia

“Shangilieni na wale wanaoshangilia; lieni na wale wanaolia.”—WAROMA 12:15.

Kanuni hiyo inamaanisha nini? Kwa maneno machache, kanuni hii inamaanisha, uwe na huruma. Kuwa na huruma ni kujiweka katika hali ya mtu mwingine na kuhisi jinsi anavyohisi.

Kuwa na Huruma Kunaweza Kutusaidiaje?

Tunapomhurumia mtu tunatambua kwamba hakuna tofauti kati yetu na yeye. Anaweza kuhisi kama tunavyohisi na akatenda kama tunavyotenda. Sifa ya huruma inatusaidia kuwaona watu wote kuwa ni ndugu zetu hata iwe wanatokea wapi. Kadiri tunavyotambua kwamba wengine hawana tofauti na sisi, ndivyo mtazamo wetu kuwaelekea unavyokuwa bora zaidi.

Sifa ya huruma itatusaidia kuwaheshimu wengine. Wakati fulani, Anne-Marie kutoka Senegal aliwadharau maskini. Anaeleza jinsi sifa ya huruma ilivyomsaidia. Anasema hivi: “Nilipoona watu hao wakiteseka, nilijiuliza ‘Mimi ningehisije ikiwa ningekuwa na hali kama yao?’ Nilitambua kwamba mimi si bora kuliko wao kwa sababu sina jambo lolote linalofanya niwe bora.” Tukijitahidi kujua hali ngumu ambazo wengine wanapitia, itakuwa rahisi kuwahurumia badala ya kuwakosoa.

Mambo Unayoweza Kufanya

Ikiwa una mtazamo usiofaa kuelekea watu fulani, jaribu kuwazia mambo ambayo hautofautiani nao. Kwa mfano, fikiria jinsi wanavyohisi

Sifa ya huruma inatusaidia kuwaona watu wote kuwa ni ndugu zetu

  • wanapokula chakula pamoja na familia yao

  • wanapotimiza malengo fulani

  • wanapotumia muda pamoja na rafiki zao, au

  • wanaposikiliza muziki mzuri wanaoupenda

Jaribu kujiweka katika hali yao. Kisha jiulize:

  • ‘Ningetendaje ikiwa mtu fulani angefanya nihisi sina thamani yoyote?’

  • ‘Ningehisije ikiwa watu wengine wangenihukumu hata kabla ya kunijua vizuri?’

  • ‘Ikiwa ningezaliwa katika jamii hiyo, ningependa watu wengine wanitendeaje?’

Wanaume haohao, Mzungu na Mkalasinga, wakionyeshana picha za mambo ambayo hawatofautiani kama vile familia zao, michezo wanayopenda, na kazi.

Simulizi: Robert (Singapore)

“Zamani nilifikiri kwamba viziwi ni watu wa ajabu, wenye uwezo mdogo wa kufikiri, na hukasirika haraka. Hivyo niliwaepuka. Hata hivyo, sikufikiri kuwa huo ni ubaguzi kwa sababu maoni yangu hayakumdhuru mtu yeyote.

“Sifa ya huruma ilinisaidia kuondoa hisia za ubaguzi. Kwa mfano, nilifikiri viziwi hawana uwezo mkubwa wa kufikiri kwa sababu, kila nikizungumza nao wananitazama tu. Hivyo nilijiuliza, ‘Mimi ningehisije ikiwa mtu fulani angezungumza nami lakini siwezi kumsikia?’ Bila shaka ningemtazama tu! Hata ningekuwa na vifaa vya kunisaidia kusikia, huenda ishara zangu za uso zingeonyesha ninajaribu kumwelewa lakini kumbe ninajitahidi kumsikia vizuri.

“Kadiri nilivyojitahidi kutambua jinsi viziwi wanavyohisi, ndivyo nilivyoendelea kuushinda ubaguzi.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki