Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g20 Na. 3 kur. 10-11
  • Anzisha Urafiki na Watu Mbalimbali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Anzisha Urafiki na Watu Mbalimbali
  • Amkeni!—2020
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Tatizo
  • Kanuni ya Biblia
  • Faida za Kufanya Urafiki na Watu Mbalimbali
  • Mambo Unayoweza Kufanya
  • Walifaulu Kuushinda Ubaguzi
    Amkeni!—2020
  • Uwe na Upendo
    Amkeni!—2020
  • Je, Niongeze Idadi ya Marafiki Wangu?
    Vijana Huuliza
  • Kutosheleza Tamaa Yetu ya Kuwa na Marafiki
    Amkeni!—2004
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2020
g20 Na. 3 kur. 10-11
Wanawake wanne wanaotoka katika mataifa mbalimbali wakizungumza na kucheka huku watoto wao wakicheza pamoja kwenye bustani.

Anzisha Urafiki na Watu Mbalimbali

Tatizo

Tukijitenga na watu ambao tunahisi ni tofauti na sisi, tutachochea hisia za ubaguzi. Na tukichagua marafiki ambao wana mtazamo kama wetu, huenda tukawa na maoni kwamba wengine wanapaswa kufikiri, kuhisi na kutenda kama sisi.

Kanuni ya Biblia

“Fungueni kabisa mioyo yenu.”​—2 WAKORINTHO 6:13.

Kanuni hiyo inamaanisha nini? Moyo unaweza kumaanisha hisia zetu kutia ndani upendo tulionao kuelekea watu wengine. Ikiwa watu tunaowapenda ni wale tu walio na hali, sifa na mtazamo kama wetu, tutakuwa tumefunga moyo wetu. Ili kuepuka tatizo hilo, ni lazima tuwe tayari kufanya urafiki na watu walio tofauti na sisi.

Faida za Kufanya Urafiki na Watu Mbalimbali

Tunapowajua watu kibinafsi, tunaanza kuelewa ni kwa nini wanafanya mambo kwa njia tofauti. Na kadiri urafiki wetu unavyokuwa wa karibu zaidi, tunaacha kukazia tofauti tulizonazo. Tunaanza kuwathamini zaidi, wanapokuwa na shangwe, tunashangilia nao, na wanapokuwa na huzuni tunahuzunika nao.

Mfikirie mwanamke anayeitwa Nazaré. Wakati fulani alikuwa akiwabagua wahamiaji. Anaeleza jambo lililomsaidia. Anasema: “Nilishirikiana nao na kufanya kazi pamoja nao. Watu hao walikuwa tofauti kabisa na mambo ambayo watu wengine walisema kuwahusu. Unapofanya urafiki na watu wa jamii tofauti, unaanza kuwapenda, kuwathamini na kuelewa kwamba kila mmoja wao ana sifa tofauti na mwenzake.”

Tahadhari

Baadhi ya watu huamua kuishi maisha ambayo huwadhuru wao wenyewe na watu wengine pia. Hivyo, tunapaswa kuwa waangalifu tunapochagua rafiki zetu. Kuwaepuka watu wasio wanyofu na wanaoishi maisha mapotovu si ubaguzi. Ingawa hutapambana na watu ambao hawaishi kulingana na viwango vyako vya maadili au kuwanyima haki zao, ni jambo la busara usiwachague wawe rafiki zako. —Methali 13:20.

Mambo Unayoweza Kufanya

Tafuta fursa za kuzungumza na watu kutoka nchi, kabila au lugha nyingine. Unaweza:

  • Kuwaomba wakueleze kuhusu maisha yao.

  • Kuwakaribisha kwa ajili ya chakula.

  • Kusikiliza kwa makini wanapokusimulia kuhusu maisha yao na kutambua mambo wanayoona kuwa muhimu.

Ukielewa jinsi mambo waliyopitia maishani yalivyowaathiri, huenda ukawa na mtazamo mzuri.

Simulizi: Kandasamy na Sookammah (Kanada)

“Tulilelewa nchini Afrika Kusini, wakati ambapo kulikuwa na ubaguzi wa rangi. Watu wa jamii moja walilazimishwa kujitenga na jamii nyingine kwa sababu ya rangi yao, na hilo lilichochea zaidi hisia za ubaguzi. Sisi si wazungu na tuliwachukia wazungu kwa sababu walituona kuwa duni. Wakati huo, hatukuhisi tuna ubaguzi. Badala yake tulihisi sisi ndio tunaobaguliwa.

“Ili kubadili mtazamo wetu, tulichukua hatua ya kwanza kwa kufungua mioyo yetu na kuwa tayari kufanya urafiki na watu kutoka tamaduni mbalimbali. Tulipoanza kushirikiana na wazungu, tulitambua kwamba kuna mambo mengi tunayofanana nao. Sisi sote tunakabili hali na changamoto zinazofanana maishani.

“Tuliwakaribisha wenzi wa ndoa ambao ni wazungu waishi nasi nyumbani kwetu kwa muda mrefu. Tulipata nafasi ya kuwajua vizuri. Hatua kwa hatua tukawa marafiki na kujiona tuko sawa. Hatimaye tulianza kuwa na mtazamo unaofaa kuelekea wazungu.”

Ndugu wa kweli

Johny na Gideon wakiwasalimia watoto nje ya Jumba la Ufalme la Mashahidi wa Yehova.

Ingawa Johny na Gideon walitoka kwenye jamii mbili tofauti na maoni yao ya kisiasa yalitofautiana, walisitawisha urafiki wa karibu.

Tazama video Johny na Gideon: Walikuwa Maadui, Sasa ni Ndugu. Tafuta video hiyo kwenye tovuti ya jw.org/sw.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki