Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g21 Na. 2 kur. 13-15
  • Teknolojia Inaathirije Uwezo Wako wa Kujifunza?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Teknolojia Inaathirije Uwezo Wako wa Kujifunza?
  • Amkeni!—2021
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UNACHOPASWA KUJUA
  • UNACHOWEZA KUFANYA
  • Ninapaswa Kujua Nini Kuhusu Kufanya Mambo Mengi kwa Wakati Mmoja?
    Vijana Huuliza
  • Jinsi ya Kutumia Teknolojia kwa Usawaziko
    Msaada kwa Ajili ya Familia
  • Thamani ya Faragha
    Amkeni!—1998
  • Teknolojia—Fikiria Wengine na Gharama
    Amkeni!—2009
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2021
g21 Na. 2 kur. 13-15
Mwanamume akitazama video inayoonyesha jinsi ya kupika chakula fulani.

Teknolojia Inaathirije Uwezo Wako Wa Kujifunza?

Kila siku watu hujifunza mambo mapya​—iwe ni shuleni, kazini au kwa sababu nyingine. Teknolojia inaweza kutusaidia. Leo, ni rahisi kupata taarifa bila hata kuondoka nyumbani wala kuinuka kwenye kiti chako.

Hata hivyo, watu wengi wanaotumia teknolojia kupita kiasi wametambua kwamba . . .

  • si rahisi kukaza fikira wanaposoma.

  • si rahisi kufanya jambo moja bila kukengeushwa.

  • wanachoka upesi wanapokuwa peke yao.

UNACHOPASWA KUJUA

Msichana akifanya mambo mengi kwa wakati mmoja. Anaandika ujumbe mfupi kwenye simu yake, anazungumza na rafiki yake kwa njia ya video, na anatumia kompyuta na kitabu kusoma.

KUSOMA

Baadhi ya watu wanaotumia vifaa vyao vya kielektroni kupita kiasi hawawezi kusoma kwa makini kitabu au makala fulani na kuimaliza yote, badala yake wanapitia juujuu ili kupata mambo makuu.

Unaweza kupitia kitabu au makala kijuu-juu ikiwa unahitaji kupata jibu la swali fulani haraka. Lakini, kufanya hivyo kutapunguza uwezo wako wa kujifunza mambo kwa kina.

JAMBO LA KUFIKIRIA: Je, unaweza kusoma vifungu virefu vya maneno bila kuchoka? Kusoma kwa makini kunaweza kukusaidiaje kujifunza mambo kwa kina?​—METHALI 18:15.

KUKAZA FIKIRA

Baadhi ya watu wanahisi kwamba teknolojia inawapa uwezo wa kufanya mambo mawili kwa wakati mmoja​—kwa mfano, wanaweza kutuma ujumbe huku wakiwa wanasoma. Lakini wanakengeushwa na mwishowe wanashindwa kufanya jambo lolote vizuri, hasa ikiwa mambo yote mawili yanahitaji kufanywa kwa umakini.

Unahitaji kujidhibiti ili ukazie fikira jambo unalofanya, lakini kuna faida kubwa ya kufanya hivyo. Msichana anayeitwa Grace anasema hivi: “Utafanya makosa machache na hutakuwa na mkazo mwingi. Nimejifunza kwamba ni bora kufanya kazi moja kwa makini kuliko kukengeushwa kwa kufanya kazi nyingi kwa wakati mmoja.”

JAMBO LA KUFIKIRIA: Je, kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja kunakuzuia usikazie fikira jambo unalojifunza au hata kulisahau kabisa?​—METHALI 17:24.

UNAPOKUWA PEKE YAKO

Baadhi ya watu hawapendi kuwa peke yao, hivyo wanatumia teknolojia zaidi ili wasiwe wapweke. Mwanamke anayeitwa Olivia anakiri hivi: “Ninachoka ninapokaa kwa dakika 15 tu bila kuangalia simu, kifaa cha kielektroni (tablet), au kuangalia TV.”

Hata hivyo, kipindi cha kuwa peke yako ni muhimu sana ili ufikirie mambo kwa kina​—hilo ni muhimu kwa watoto na watu wazima hasa wanapotaka kujifunza jambo fulani.

JAMBO LA KUFIKIRIA: Je, unaweza kutumia vizuri wakati wa kuwa peke yako ili ujifunze jambo fulani?​—1 TIMOTHEO 4:15.

UNACHOWEZA KUFANYA

CHUNGUZA JINSI UNAVYOTUMIA TEKNOLOJIA

Ni kwa njia gani unaweza kutumia teknolojia kuboresha uwezo wako wa kujifunza? Teknolojia inaweza kukuzuiaje usikaze fikira na kujifunza kikamili?

KANUNI YA BIBLIA: “Ilinde hekima inayotumika na uwezo wa kufikiri.”​—METHALI 3:21.

JIULIZE . . .

  • Je, ni vigumu kwangu kukaza fikira ninaposoma makala ndefu kwenye kifaa cha kielektroni? Ikiwa ndivyo, ni mambo gani hasa yanayonikengeusha?

  • Ninaweza kuchukua hatua gani ili kupunguza au hata kuondoa kabisa mambo hayo?

Dokezo: Anza kwa kusoma habari fupifupi na kisha hatua kwa hatua ongeza kiwango cha habari unachosoma. Soma kwa sauti, taratibu, ili ukazie fikira mambo unayosoma.

  • Ninaweza kufanya mabadiliko gani ili niwe na muda wa kutosha wa kufikiria na kutafakari mambo niliyosoma?

Dokezo: Tumia dakika kumi kabla ya kumaliza kusoma kupitia mambo uliyosoma.

  • Ni katika hali gani ninalazimika kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja?

  • Ninaweza kufanya mabadiliko gani ili nifanye kikamili kazi moja kabla ya kuanza kazi nyingine?

Dokezo: Unapojifunza, weka mbali vitu vinavyoweza kukukengeusha ili uweze kukaza fikira.

KANUNI YA BIBLIA: “Jipatie hekima, jipatie uelewaji.”​—METHALI 4:5.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki