Sura ya 5
Wafu Wako Wapi?
1. Ni maswali gani ambayo kwa kawaida watu huuliza juu ya
LABDA wewe umepata kujiona upweke kwa sababu ya kupotelewa na mpenzi katika mauti. Katika vipindi vya namna hiyo watu wengi sana hawaoni huzuni tu bali pia hujiona dhaifu sana. Ni jambo la asili kutaka kujua: Jambo gani humpata mtu wakati anapokufa? Je! angali anayo fahamu mahali fulani? Je! liko tumaini la kweli kwamba wafu wataishi tena? Biblia ina jibu lenye kufariji kwa maswali haya.
2. Biblia husema jambo gani lilimpata mtu wa kwanza Adamu wakati wa kufa kwake, na hivyo mauti ni nini?
2 Kusema kwa urahisi, mauti ni kinyume cha uhai. Katika kumhukumu mtu wa kwanza Adamu kwa kutokutii kwake kwa makusudi, Mungu alisema: “[Utairudia] ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.” (Mwanzo 3:19) Fikiri sasa: Adamu alikuwa wapi kabla Mungu hajamwumba kutoka katika mavumbi na akampa uhai? Naam, yeye hakuwapo. Wakati wa kufa kwake Adamu aliirudia hali ile ile, isiyo na uhai na isiyo na fahamu. Yeye hakwenda wala kwenye jehanum ya moto wala kwenye furaha za mbinguni, bali alikufa—kama Mungu alivyosema kuwa angekufa.—Mwanzo 2:17.
3. Mhubiri 9:5, 10 husema nini juu ya hali ya wafu, na jambo gani hutukia kwa mawazo ya mwanadamu wakati wa kufa?
3 Biblia hufundisha waziwazi kwamba wafu wamo kaburini na hawana fahamu na hawana uhai. Angalia ambayo Mhubiri 9:5, 10 husema kwa habari ya hali ya wafu: “Kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote, wala ha-wana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahauliwa. Lo lote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; kwa kuwa hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, huko kuzimu uendako wewe.” Hii humaanisha kwamba wafu hawawezi kufanya jambo lo lote na hawawezi kusikia jambo lo lote mwilini. Mawazo yao yamekoma, kama Biblia isemavyo: “Msiwatumainie wakuu, wala binadamu ambaye hakuna wokovu kwake. Pumzi yake hutoka, huurudia udongo wake, siku hiyo mawazo yake yapotea.”—Zaburi 146:3, 4.
JE! MWANADAMU ANAYO NAFSI ISIYOWEZA KUFA?
4. Hesabu 31:28 hufunua nini juu ya neno “nafsi”?
4 Lakini namna gani juu ya nafsi? Je! si sehemu ya mwanadamu inayojitenga na mwili wake wakati wa kufa na huendelea kuishi? Ili kujibu hili sawasawa ni lazima tujue nafsi ni nini. Labda utashangaa kujua kwamba wanyama na wanadamu pia huitwa “nafsi” katika Maandiko yaliyoongozwa na roho ya Mungu. Kwa mfano, Hesabu 31:28, NW husema juu ya “nafsi moja [Kiebrania, neph’esh] kutoka katika mia tano, katika wanadamu na katika kundi la ng’ombe na katika punda na katika kundi la kondoo.”—Tazama pia Ufunuo 16:3, NW, mahali ambapo neno la Kigiriki kwa “nafsi,” psykhe huonekana.
5. Biblia husimuliaje nafsi?
5 Basi, nafsi, ni nini? Ebu tuone ambayo Neno lililoandikwa la Muumba mwenyewe liyasemayo juu yake. Katika Mwanzo 2:7 tunasoma: “[Yehova] Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.”
6. Ni mambo gani ya hakika juu ya nafsi ya kibinadamu huonyesha kwamba isingeweza kuwa kitu cha namna ya kivuli kiwezacho kuishi mbali na mtu? Basi nafsi ya kibinadamu ni nini?
6 Angalia, tafadhali, kwamba baada ya Mungu kumwanzisha mtu kupumua “mtu akawa nafsi hai.” Kwa hiyo mtu alikuwa ndiyo nafsi, kama vile mtu ambaye huwa daktari ndiye daktari. (1 Wakorintho 15:45) Kwa kuwa nafsi ya kibinadamu ni mtu mwenyewe, basi haiwezi ikawa kitu fulani cha namna ya kivuli ambacho hukaa tu katika mwili au kiwezacho kuishi mbali na mtu. Kupatana na jambo hili la hakika, Biblia hueleza waziwazi kwamba nafsi ya kibinadamu inazo sifa za kimwili. Kwa mfano, Biblia husema juu ya nafsi kutamani chakula cha kimwili, ikisema: “Nafsi yako inatamani kula nyama.” (Kumbukumbu la Torati 12:20; Mambo ya Walawi 17:12, NW) Inasema, pia, kwamba nafsi zinayo damu ikitembea katika mishipa yake, kwa maana husema juu ya “damu ya nafsi za maskini wasio na hatia.” (Yeremia 2:34, NW) Naam, nafsi yako kweli ndiyo wewe, pamoja na sifa zako zote za kimwili na za moyoni.—Mithali 2:10.
7. Wakati Biblia inapotumia usemi “nafsi yangu,” inamaanisha nini?
7 Namna gani, basi, maandiko yanayotumia maneno kama “nafsi yangu,” au yale yasemayo juu ya nafsi ya mtu kana kwamba imo ndani yake? Kwa kweli, maandiko haya lazima yapatane na maandiko tuliyokwisha kuyazungumza, kwa maana hapawezi pakawa kutopatana katika Neno la Mungu. Basi, inakuwa wazi kwamba neno “nafsi” laweza kutumiwa katika maana mbalimbali. Mara nyingine humtaja mtu mwenyewe kama nafsi. Hivyo kama vile mtu husema “mimi mwenyewe” aweza pia kusema “nafsi yangu,” kwa msingi maana yake ni jambo lile lile. Hivyo mtunga zaburi aliandika: “Nafsi yangu imekuwa haina usingizi kwa sababu ya huzuni.”—Zaburi 119:28, NW.
8. (a) Ni katika njia gani nyingine neno “nafsi” laweza kutumiwa? Basi mtu aliye hai aweza kusemwa kwa kufaa kwamba “anayo nafsi”? (b) Ni habari gani za Biblia husema juu ya mtu kupoteza uhai wake au nafsi?
8 “Nafsi” pia yaweza kuwa na maana ya maisha ambayo mtu huyafurahia kama nafsi iliyo hai au mtu. Basi, tunaweza kusema kwamba fulani yu hai, maana yake yeye ni mtu hai. Au twaweza kusema kwamba yeye anao uhai, maana yake yeye anao uhai kama mtu. Kwa jinsi iyo hiyo, mwanadamu, kupatana na Biblia, ndiye nafsi; lakini, wakati yeye yu hai, aweza kusemekana kwamba “anayo nafsi.” Hivyo, kama vile tusemavyo juu ya mtu kupoteza uhai wake, twaweza kusema juu ya kuipoteza nafsi yake. Yesu akasema: “Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake?” (Mathayo 16: 26) Wakati Raheli alipopata taabu katika kumzaa Benyamini, nafsi yake (au uhai kama nafsi) ilimtoka naye akafa. (Mwanzo 35:16-19, NW) Yeye alikoma kuwa mtu hai na akawa maiti. Na wakati nabii Elia alipofanya mwujiza kuhusu mtoto aliyekufa, nafsi ya mtoto (au uhai kama nafsi) ilirudi katika yeye “naye akawa hai.” Yeye alikuwa nafsi hai tena.—1 Wafalme 17:17-23, NW.
9. (a) Je! Biblia inasema kwamba nafsi ya kibinadamu haiwezi kufa? (b) Ni maandiko gani yaonyeshayo kwamba nafsi ya kibinadamu yaweza kufa?
9 Kwa kuwa nafsi ndiye mtu mwenyewe, jambo gani huipata nafsi wakati wa kufa? Biblia inaeleza waziwazi sana katika kusema kwamba nafsi hufa, ikisema: “Nafsi inayofanya dhambi—hiyo yenyewe itakufa.” (Ezekieli 18:4, 20, NW) Mtume Petro alitumia maneno kutoka kwa maandishi ya Musa kuhusu Yesu, akisema: “Kweli, nafsi yo yote isiyosikiliza kwa yule Nabii itaangamizwa kabisa kutoka miongoni mwa watu.” (Matendo 3:23, NW) Kupatana na kweli hii ya msingi, si mara moja Biblia husema katika yo yote ya mistari yake kwamba wala nafsi za kibinadamu wala za wanyama ni nafsi zisizoweza kufa, hazina mauti, haziwezi kuharibiwa au haziwezi kuangamia. Walakini, yako maandiko mengi yanayoonyesha kwamba nafsi yaweza kufa au kuuawa. (Mambo ya Walawi 23:30; Yakobo 5:20, NW) Hata kwa habari ya Yesu Kristo Biblia husema: “Alimwaga nafsi yake hata kufa.” (Isaya 53:12) Basi, tunaona, kwamba nafsi ya kibinadamu ndiye mtu mwenyewe, na mtu afapo, ni nafsi ya kibinadamu ndiyo inayokufa.
10. Mvurugo juu ya maneno gani mawili umeleta kutokuelewa sawasawa juu ya mauti?
10 Mengi ya kutokuelewa sawasawa juu ya mauti yamekuwa kwa sababu ya mvurugo katika akili za watu wengi kuhusu maana ya “nafsi” na “roho.” Bi-blia huonyesha kwamba si vitu vya namna moja, kama tutakavyoona.
ROHO NI NINI KATIKA VIUMBE VILIVYO HAI?
11. (a) Kupatana na Ayubu 34:14, 15, ni vitu gani viwili ambavyo lazima mwanadamu awe navyo ili adumu kuwa hai? (b) Eleza kila kimoja cha hivi kinamaanisha nini?
11 Kutokana na Ayubu 34:14, 15 tunajifunza kwamba kuna vitu viwili ambavyo ni lazima mwanadamu (au kiumbe kingine cho chote cha kidunia chenye fahamu) awe navyo ili adumu kuwa hai: roho na pumzi. Mle tunasoma: “Kama [Mungu] akimwekea mtu moyo wake, akijikusanyia roho [Kiebrania, ru’ahh] yake na pumzi [Kiebrania, neshamah’] zake; wenye mwili wote wataangamia pamoja, nao wanadamu watarejea tena kuwa mavumbi.” Tunajua kwamba mtu wa kwanza aliumbwa na Mungu kutoka katika “mavumbi ya ardhi,” yaani, vitu vya asili vilivyochukuliwa katika ardhi. Wakati wa kuumbwa kwa Adamu, Mungu alifanyiza mabilioni ya chembe katika mwili wake kuishi, kuwa na nguvu za uhai ndani yake. Hii nguvu ya uhai ya utendaji ndiyo inayomaanishwa ha-pa kwa neno la “roho (ru’ahh). Lakini ili nguvu ya uhai ipate kuendelea katika kila moja ya mabilioni ya chembe za Adamu, zilihitaji oksijeni, na hii ilipaswa kutolewa kwa njia ya kupumua. Basi, jambo lililofuata Mungu “akampulizia puani pumzi [neshamahl] ya uhai.” Ndipo mapafu ya Adamu yalipoanza kufanya kazi na hivyo kuendeleza nguvu ya uhai katika chembe za mwili wake kwa njia ya kupumua.—Mwanzo 2:7.
12. Onyesha mfano wa “pumzi ya uhai” kwa jambo liwezalo kutukia kwa kitoto kilichozaliwa hivi karibuni.
12 Jambo hili lilifanana na habari ya vitoto fulani vinavyozaliwa hivi karibuni. Ijapokuwa mna uhai katika kitoto wakati kinapozaliwa, mara nyingine hakianzi kupumua mara baada ya kuzaliwa. Daktari huona lazima kukipiga kofi kitoto ili kukianzisha kupumua, kwa maana pasipo pumzi mtoto angekufa upesi. Vivyo, pia, uhai katika chembe za mwili wa Adamu ulipaswa kuendelezwa kwa njia ya kupumua ili Adamu apate kutimiza kazi za mtu aliye hai.
13. (a) Je! roho ina hali ya utu? (b) Kutumia mfano wa motokaa, roho yaweza kulinganishwa na nini?
13 Kwa kuwa nafsi ya kibinadamu ndiye mtu mwenyewe aliye hai, roho ni nguvu tu ya uhai inayomwezesha mtu huyo kuwa hai. Roho haina hali ya utu, wala haiwezi kufanya mambo ambayo mtu aweza kufanya. Haiwezi kufikiri, kusema, kusikia, kuona au kugusa. Kwa sababu hiyo, inaweza kufananishwa na mkondo wa stimu ya beteri ya motokaa. Mkondo huo waweza kuwasha mafuta kufanya injini kutokeza nguvu, kufanya taa za mbele ya motokaa kung’aa, kufanya honi kulia, au kuifanya redio ya motokaa kutoa sauti na muziki. Lakini bila injini, taa za mbele ya motokaa, honi au redio, je! ule mkondo wa beteri ungeweza kufanya yo yote ya mambo haya kwa njia yake yenyewe? La, kwa maana ni nguvu tu inayouwezesha mtambo kufanya kazi na kufanya mambo ya namna hiyo.
14. Je! wanyama wanayo nguvu ya uhai au roho ile ile kama vile mwanadamu anayo?
14 Roho hii au nguvu za uhai hupatikana katika viumbe vyote vyenye uhai, ikipelekwa kutoka kwa wazazi kwenda kwa watoto wakati wa mtungo wa mimba. Hivyo, Mungu alimwambia Nuhu kwamba ye-ye angefanyizisha gharika ya maji “kuharibu mwili wote, ambao katika huo mna nguvu ya utendaji [ru’ahh, roho] ya uhai,” ya wanyama na wanadamu pia.—Mwanzo 6:17, NW, margin, chapa ya 1953; tazama pia 7:15, 22, AV, maneno ya pembeni.
15. Mhubiri 3:19, 20 huonyeshaje kwamba wanadamu na wanyama pia wanayo roho hii au nguvu ya uhai?
15 Kwa sababu vyote vina nguvu ile ile ya uhai au roho, wanadamu na wanyama hufa kwa jinsi ile ile. Kwa sababu hiyo, Mhubiri 3:19, 20 husema: “Linalowatukia wanadamu linawatukia wanyama; jambo moja lawatukia; anavyokufa huyu ndivyo anavyokufa huyu; naam, wote wanayo [roho] moja [ru’ahh] . . . Wote huendea mahali pamoja; wote hutoka katika mavumbi; na hata mavumbini hurudi tena.”
16. (a) Ni katika njia gani roho huuacha mwili wakati wa kufa? (b) Inarudije kwa Mungu?
16 Kwa kuwa Mungu ndiye Mpaji wa uhai, Neno lake husema kwamba wakati mtu afapo “mavumbi [huirudia] nchi kama yalivyokuwa, nayo roho [humrudia] Mungu aliyeitoa.” (Mhubiri 12:7) Wakati wa kufa nguvu ya uhai hatimaye huziacha chembe zote za mwili na mwili huanza kuoza. Mawazo ,yote ya fahamu na matendo hukoma. (Zaburi 104:29) Jinsi gani, basi, roho ‘humrudia Mungu aliyeitoa’? Je! nguvu ya uhai huiacha dunia kwa njia halisi na kusafiri katika anga mpaka panapo Mungu? La, humrudia Mungu katika maana ya kwamba sasa matumaini ya uzima wa wakati ujao wa mtu hubakia kabisa katika mikono ya Mungu. Mungu peke yake ndiye awezaye kuirudisha roho, kumfanya mtu aishi tena.
17. (a) Je! mtu aliyekufa anaweza kuwadhuru walio hai, au mtu aliye hai kumfaidi mtu aliyekufa? (b) Kujua kwetu kweli juu ya hali ya wafu hutulinda sisi na desturi gani ya kishetani?
17 Watu wengine huishi katika hofu ya wafu na hufanya matambiko ili kuwatuliza wazee waliokufa. Lakini tunaweza kupata faraja katika kujua kwamba, kwa kuwa wafu hawana fahamu, haiwezekani kwao kuwadhuru walio hai. Na ijapokuwa huenda mmoja alimpenda sana mtu fulani aliyekufa, Neno la Mungu huonyesha kwamba mmoja hawezi kumfaidi mtu aliyekufa kwa kumfanyia mtu wa namna hiyo matendo ya kidini au kawaida za ibada, labda kwa hasara kubwa kwa wale wabakio baada ya kufiwa. (2 Samweli 12:21-23) Kujua kwetu hali ya kweli ya wafu hutulinda sisi tena na desturi ya kujaribu kusema na wafu. Biblia huonya kwamba wale wajidaio kusema na wafu kwa kweli wao huzungumza na mashetani, viumbe vibaya vya kiroho vinavyosingizia uongo kuwa ndiye mtu aliyekufa.—Kumbukumbu la Torati 18: 10-12.
KUZIMU NI NINI
18. Dini nyingi hufundisha nini juu ya kuzimu, na kunazuka maswali gani juu yake?
18 Dini nyingi hufundisha kwamba watu wafapo huenda mahali pa mizimu paitwapo kuzimu. Lakini imani hii hufundishwa katika Neno la Mungu? Labda unajua maana ambayo dini yako mwenyewe hutoa kwa neno “kuzimu,” lakini je! umewahi kuchunguza kuona manna inayotolewa katika Maandiko? Kuzimu ni nini kupatana na Biblia?
19. (a) Neno “kuzimu” hutafsiriwa kutokana na neno gani la Kiebrania? Na neno hili la Kiebrania hutafsiriwaje katika Biblia ya Union Version katika Kiswahili? (b) Mara nyingine neno “kuzimu” hutafsiriwa kutokana na neno gani la Kigiriki?
19 Katika Maandiko ya Kiebrania ya Biblia neno “kuzimu” hutafsiriwa kutokana na neno la Kiebrania sheol’. Neno hili huonekana jumla ya mara 65. Walakini, Biblia ya Union Version katika Kiswahili, hutafsiri neno sheol’ mara 54 kama “kuzimu,” mara 6 kama “kaburi” au “kaburini,” mara 3 kama “ahera,” na mara mbili kama “shimo.” Katika Maandiko ya Kikristo ya Kigiriki neno “kuzimu” hutafsiriwa mara nyingine kutokana na neno la Kigiriki ha’des. Biblia ya Union Version hutafsiri neno ha’des kama “kuzimu” katika kila mahali pake kumi ambapo huonekana.
20. (a) Kwa nini kuzimu haimaanishi mahali ambapo wafu huendelea kuishi? (b) Je! Yesu alikuwamo katika kuzimu?
20 Je! kuzimu ni mahali pa mizimu? Je! sheol’ na ha’des humaanisha mahali fulani ambapo wafu huendelea kuishi? Ni wazi kwamba sivyo, kwa maana tumekwisha kuona kwamba wafu hawana fahamu na kwa hiyo hawawezi kuendelea kuishi. Biblia haijipingi yenyewe kuhusu hali ya wale waliomo katika kuzimu. Jambo hili huthibitishwa na uhakika wa kwamba Biblia husema kwamba Yesu alikuwamo katika kuzimu. (Matendo 2:31) Wakati mtume Petro aliposema jambo hili siku ya Pentekoste, kwa wazi alimaanisha kwamba Yesu alikuwa amekufa kaburini, si hai mahali fulani pa mizimu. (1 Wakorintho 15:3, 4; Isaya 53:12) Katika kusema hivi mtume alitumia maneno kutoka Zaburi 16: 10. Neno la Kiebrania sheol’ lilitumiwa hapa, na katika Matendo 2:31 neno hili linatafsiriwa na neno in Kigiriki ha’des. Hii huonyesha kwamba sheol’ na ha’des humaanisha jambo lile lile. “Kuzimu” ya Biblia kwa kweli ni kaburi la wanadamu.
21. (a) Je! Lazaro, ndugu ya Mariamu na Martha, alikwenda mahali pa mizimu, na twajuaje hili? (b) Je! wale waliomo katika kuzimu wako hai?
21 Iwapo mtu ye yote angeweza kujua kama wafu wako na fahamu au hawana fahamu, kwa hakika angekuwa mmoja ambaye amerudi kutoka kwa wafu. Lazaro, ndugu ya Mariamu na Martha, alikuwa mmojawapo wa wale waliorudi kutoka “kuzimu” ya Biblia. Hata hivyo Lazaro hakusema neno moja juu ya lo lote lililotukia wakati alipokuwa kule. (Yohana 11:1114, 38-44) Kwa nini sivyo? Kwa sababu, kama tulivyokwisha kujifunza, “wafu hawajui neno lo lote.” (Mhubiri 9:5) Kama uthibitisho zaidi wa hili Ufunuo sura ya 20, mstari wa 13 hutuambia kwamba “Mauti na Kuzimu [ha’des] zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake.” Kwa wazi “kuzimu” ya Biblia ni kaburi la kawaida la wanadamu wote, mahali pasipo na uhai.
TAJIRI NA LAZARO
22. Twajuaje kwamba maneno ya Yesu juu ya tajiri na Lazaro ni mfano?
22 Walakini, pana mahali pamoja ambapo kuzimu [hades] huonekana, ambapo pamewafanya watu wengine kusadiki kwamba kuzimu ya Biblia ni mahali pa mateso ya kimwili. Hapo ni mahali ambapo Yesu alisema juu ya tajiri na Lazaro, na akasema kwamba tajiri alikufa, na katika kuzimu [ha’des] akapatwa na mateso. (Luka 16:22-31) Kwa nini matumizi ya kuzimu[ha’des] hapa ni tofauti sana na matumizi yake katika mahali pengine? Kwa sababu Yesu alikuwa akitoa mfano naye alikuwa hasemi habari ya mahali halisi ya mateso. (Mathayo 13:34) Angalia: Je! ni jambo la akili au la Maandiko kusadiki kwamba mtu huteswa kwa sababu tu yeye ni tajiri, huvaa nguo nzuri na ana chakula tele cha kula? Je! ni jambo la Maandiko kusadiki kwamba mmoja hubarikiwa na maisha ya mbinguni kwa sababu tu yeye ni mwenye kuomba-omba? Angalia hili pia: Je! kuzimu iko katika kiasi cha umbali ulio karibu na mbingu hata kwamba ingewezekana kuwa na mazungumzo halisi? Tena, kama tajiri alikuwa katika ziwa halisi liwakalo moto, jinsi gani Ibrahimu angeweza kumtuma Lazaro kwenda kupooza ulimi wake kwa tone tu la maji penye ncha ya kidole chake? Ni nini, basi, Yesu alikuwa akionyesha mfano?
23. Ni nini maana ya mfano kwa habari ya (a) tajiri? (b) Lazaro? (c) mauti ya kila mmoja? (d) mateso ya tajiri?
23 Katika mfano huu tajiri alifananisha jamii ya viongozi wa kidini waliomkataa na hatimaye wakamwua Yesu. Lazaro hufananisha watu wa kawaida waliomkubali Mwana wa Mungu. Biblia huonyesha kwamba mauti yaweza kutumiwa kama mfano, ikionyesha badiliko kubwa katika maisha ya mtu au mwendo wa tendo. (Linganisha Warumi 6:2, 11-13; 7:4-6.) Mauti, au badiliko kutoka katika hali za zamani, ilitokea wakati Yesu alipoilisha jamii ya Lazaro kwa kiroho, na hivyo nao wakaja katika kibali cha Ibrahimu mkubwa zaidi, Yehova Mungu. Wakati uo huo, viongozi wa uongo wa kidini ‘wakafa’ kwa habari ya kuwa na kibali cha Mungu. Wakikataliwa mbali, walipata mateso wakati wafuasi wa Kristo baada ya Pentekoste walipofunua waziwazi kwa nguvu matendo yao mabaya. (Matendo 7:51-57) Kwa hiyo mfano huu haufundishi kwamba watu fulani waliokufa huteswa katika kuzimu yenye moto halisi.
JEHANUM NA PURGATORI (MATOHARA)
24. (a) Wakati tafsiri fulani za Biblia zisemapo juu ya “jehanum ya moto,” ni kutoka katika neno gani la awali la Kigiriki neno “jehanum” hutafsiriwa? (b) Jehanum ilitumiwaje wakati Yesu alipokuwa duniani?
24 Labda mtu fulani atapinga na kusema kwamba Biblia husema juu ya “jehanum ya moto.” (Mathayo 5:22) Kweli, tafsiri fulani hutumia usemi huu, lakini katika habari za namna hiyo neno la awali la Kigiriki lililotumiwa hapa kwa “jehanum” ni Ge’enna, silo ha’des. Jehanum huonekana mara kumi na mbili katika Maandiko ya Kikristo ya Kigiriki, na humaanisha bonde la Hinomu nje ya kuta za Yerusalemu. Yesu alipokuwa duniani bonde hili lilitumiwa kama jaa kubwa ya taka mahali ambapo moto uliendelezwa kuwaka kwa kuongeza kiberiti (sulfur) kwa kuchoma takataka. Smith’s Dictionary of the Bible, Volume ya I, hueleza: “Pakawa mahali pa kawaida pa taka ya mji, ambapo maiti za waasi, na mizoga ya wanyama, na kila aina nyingine ya taka ilipotupwa.”
25. (a) Jehanum ni mfano unaofaa wa nini? (b) Ni maneno gani katika kitabu cha Biblia cha Ufunuo ni mfano wa jambo lile lile?
25 Basi wakati Yesu aliposema kwamba watu wangetupwa katika Jehanum kwa matendo yao mabaya, alikuwa na maana gani? Si kwamba wangeteswa milele. Yesu alitumia bonde hilo (Jehanum) la moto na kiberiti kama mfano unaofaa wa uharibifu wa milele. Ndivyo wasikilizaji wake wa karne ya kwanza walivyoelewa kuwa ndiyo maana yake. “Ziwa la moto” linalotajwa katika kitabu cha Ufunuo lina maana ile ile, si mateso katika hali ya kufahamu, bali ni “mauti ya pili,” mauti ya milele au uharibifu. Ni wazi kwamba “ziwa” hili ni mfano, kwa sababu mauti na kuzimu (ha’des) hutupwa ndani yake. Vitu vya namna hiyo haviwezi kuteketezwa kwa njia halisi, bali vyaweza kuondolewa kabisa, au kuharibiwa.—Ufunuo 20: 14; 21:8.
26. Je! Biblia hutaja mahali kama purgatori?
26 Basi, purgatori, ni nini? Hii husemwa kuwa mahali ambapo roho za kibinadamu huwa na fahamu na hutakaswa katika moto baada ya kufa. Kwa kuwa Biblia huonyesha waziwazi kwamba wafu hawana fahamu, Mungu angewezaje kumtesa mtu ye yote katika mahali pa namna hiyo? (Zaburi 146:4) Kwa kweli, wala neno “purgatori” wala wazo la “purgatori” halionekani katika Biblia.
JE! WAFU WATAISHI TENA?
27. Kuna tumaini gani kwa wafu?
27 Kufundisha kwa Biblia juu ya hali ya kweli ya wafu huondoa hofu na mashaka mengi yasiyo ya lazima katika akili za mtu kuhusu wale ambao wamekufa. Kujua kwamba watu hawa hawateswi hutusaidia sisi kuthamini zaidi sana upendo wa Mungu, na haki. yake. Hata hivyo, bado labda mtu atataka kujua, Ikiwa mtu anakufa na anakwenda tu kaburini, kuna tumaini gani kwa wafu? Biblia hufunua kwamba kuna tumaini la ajabu, tumaini la kuishi tena.
28. (a) Kufufua kwa Yesu kwa watu kutoka kwa wafu kulitoa mfano gani wa mbele? (b) Umati mkubwa zaidi wa wanadamu watafufuliwa kwenye nini?
28 Wakati wa huduma yake ya kidunia Yesu Kristo alionyesha uwezo wake juu ya mauti, akiwarudisha kweli watu waliokufa kwenye uhai wa kibinadamu. (Luka 7:11-16; Yohana 11:39-44) Yeye alitoa mfano wa mbele wa jambo atakalofanya kwa kiasi kikubwa sana katika taratibu mpya ya mambo ya Mungu .Tumaini lenye kuchangamsha moyo ni la kwamba wakati huo kuzimu, kaburi la kawaida la wanadamu, itakuwa tupu kwa kuondolewa wafu wake wasio na fahamu. (Ufunuo 20:13) Wengine hupokea ufufuo kwenye utukufu wa mbinguni kama viumbe vya kiroho, hata kama vile Yesu Kristo alivyopokea. (Warumi 6:5) Walakini, umati mkubwa zaidi wa wanadamu watarudishwa ili wafurahie uzima katika paradiso ya kidunia itakayorudishwa. —Matendo 24:15; Luka 23: 43, NW.
29. Mipango ya ajabu ya Yehova kwa kuwabariki wanadamu hutoa maana ya kutosha itutie moyo sisi kufanya nini?
29 Katika taratibu mpya ya Mungu wafu watakaofufuliwa, ikiwa wanatimiza sheria za haki za Mungu, haitakuwa lazima kamwe wafe tena. (Isaya 25:8) Kwa hakika mpango huu wa ajabu kwa kubariki wanadamu ndiyo sababu kwetu sisi kuyatwaa maarifa zaidi ya Yehova na ya Mwanawe, Yesu Kristo. Kufanya hivyo kwaweza kuongoza kwenye uzima wetu wa milele na baraka zetu za milele.
wafu?