Roho Inayoendesha Taratibu ya Zamani Iliyopo
(Funzo la Kitabu)
1. Ni ulizo gani linalotokea juu ya roho ambayo imeenea katika taratibu ya mambo ya zamani iliyopo, na yatupasa tuazimieje?
TARATIBU ya mambo iliyopo ni ya zamani—ilianza maelfu ya miaka yaliyopita. Katika maelfu hayo yote ya miaka roho moja imeenea katika taratibu ya mambo ya kibinadamu. Je! imekuwa roho takatifu? Hakuna mtu atakayepinga mambo ya hakika ya historia kwa kudai kwamba roho takatifu itokayo kwa Yehova Mungu ndiyo imekuwa nguvu isiyoonekana yenye kutendesha jamii yote ya kibinadamu katika shughuli (kazi) zake, au katika mtindo wake wa maisha. Kama roho takatifu ndiyo ingalikuwa imeendesha taratibu hii ya zamani ya mambo wakati wote huo, matokeo yangalikuwa tofauti kabisa na hali ya mambo ya ulimwengu leo.
2. (a) Watu wanaofuatana na taratibu hii ya zamani wanaongozwa na sheria za namna gani? (b) “Kazi za mwili” ni nini, nayo “matunda ya roho” ni nini?
2 Roho takatifu itokayo kwa Yehova Mungu, ifanyapo kazi katika maisha za watu, inatokeza matunda yenye kuitambulisha. Tukiamua kutokana na matunda ambayo taratibu hii ya zamani imekuwa na wakati tele wa kutokeza, twaweza kusema haiongozwi na roho takatifu ya Mungu. Umati mkubwa wa wanadamu wanaofuatana na taratibu hii ya zamani wanajionyesha kuwa watu wanaohitaji kuzuiwa na sheria zinazofanywa kwa ajili ya watu wenye kutaka uvunjaji wa sheria, zinazowaamuru waepuke mabaya ya namna zote. Miaka mia kumi na tisa iliyopita alikuwako mwanamume mmoja aliyetoka katika orodha kama hiyo ya sheria. Aliandika barua kuonyesha kwamba twahitaji uongozi bora, nguvu bora yenye kufanya kazi katika maisha zetu, ikiwa twataka kuwa tofauti na taratibu ya zamani iliyopo. Twahitaji ile roho, nguvu ya utendaji isiyoonekana itokayo kwa Yeye aliye na adili bora zaidi kuliko taratibu hii ya ulimwengu ya zamani, aliye bora zaidi kuliko mpaji ye yote wa sheria katika jamii ya kibinadamu. Mwandikaji wa barua hiyo alionyesha nguvu hiyo takatifu inayoweza kututendesha kazi zinazofaa, akisema:
“Endeleeni kutembea kwa roho nanyi hamtaendesha tamaa yo yote ya kimwili. Kwa maana mwili unapinga roho katika tamaa yake, nayo roho inaupinga mwili; kwa maana hivyo viwili vinapingana, hata mambo yale mngependa kuyafanya hamyafanyi. Zaidi ya hilo ikiwa mnaongozwa na roho, hamko chini ya sheria.
“Sasa kazi za mwili ni dhahiri, nazo ni uasherati, uchafu, mwenendo mpotovu, ibada ya sanamu, kuzoea uchawi, uadui, ugomvi, wivu, vipindi vya ulevi, karamu za ulafi, na mambo kama hayo. Kwa habari ya mambo hayo natangulia kuwaonya, jinsi ile ile nilivyotangulia kuwaonya, kwamba wale wanaozoea mambo hayo hawataurithi ufalme wa Mungu.
“Kwa upande mwingine, matunda ya roho ni upendo, furaha, amani, ustahimilivu, fadhili, wema, imani. upole, kujiweza. Juu ya mambo hayo hakuna sheria.”—Gal. 5:16-23, NW; angalia 1 Timotheo 1:8-11 pia.
3. Wale wanaotazamia kurithi haraka za ufalme wa Mungu hawazoei kazi gani?
3 Hiyo ni orodha ya mambo tofauti, sivyo? Bila shaka wale wanaozaa matunda ya roho ya Mungu hawazoei mambo yanayoitwa “kazi za mwili.” Wanautazamia ufalme wa Mungu wakiwa na tamaa nyofu ya kurithi baraka zake.
4. Kwa sababu gani sisi wenyewe hatuna haja ya kuonyesha makosa ya taratibu ya zamani, na kwa sababu gani taratibu hiyo ya zamani haitasaidia watu warithi ufalme wa Mangu?
4 Hata hivyo, namna gani juu ya taratibu ya zamani iliyopo? Hatuna lazima ya kuonyesha makosa yake. Ripoti za magazeti, makala za magazeti, maandishi ya polisi, ukosefu wa usalama ulio mahali pote kwa sababu ya kuongezeka kwa uvunjaji wa sheria, hospitali zenye bei za juu za kuponyea magonjwa ya akili na vilevile kaswende na kisonono yenye kutisha, wasiwasi wa kisiasa pamoja na tisho (ogopesho) linaloongezeka la vita ya dunia nzima na kutumia makombora ya atomiki, zinatuonyesha makosa yake. Yako mambo mengi yasiyohesabika ambayo yangeweza kutajwa kuonyesha taratibu ya zamani imejawa na “kazi za mwili.” Taratibu hii ya zamani haitasaidia watu ‘waurithi ufalme wa Mungu.’ Haina uhusiano na ufalme wa Mungu. Haikuenewa, haikuongozwa wala kusaidiwa na roho takatifu itokayo kwa Mungu. Si takatifu hata kidogo, hata ile sehemu yake inayoitwa Jumuiya ya Wakristo.
5, 6. Kwa sababu gani tamaa ya asili ya mwili ya kufanya mambo yanayopinga roho ya Muumba haikusababishwa na Mungu?
5 Imekuwaje kwamba roho ya Mungu haiendeshi sehemu yo yote ya taratibu hii ya zamani? Mwili wa kibinadamu uliingiaje katika hali ya kutaka kwa urahisi kufanya kazi zinazopinga roho ya Mungu? Mwili wa kibinadamu haukuwa hivyo ulipoumbwa. Wakati huo uliongozwa na roho ya Muumba wake. Mungu asingaliweza kutia ndani ya mwili alioumba wakati huo tu kitu kibaya cha kumpinga yeye. Yeye siye Chanzo cha ubaya. Mteteaji wa chanzo cha mambo ya haki, nabii Musa alimwondolea Yehova Mungu malawama yote ya maelekeo mabaya yaliyomo katika mwili wa mwanadamu. Musa alisema: “Kazi yake ni kamilifu; maana, njia zake zote ni haki. Mungu wa uaminifu, asiye na uovu, yeye ndiye mwenye haki na adili. Wametenda mambo ya uharibifu, hawawi watoto wake, hii ndiyo ila yao.”—Kum. 32:4, 5.
6 Kasoro iliyomo ndani ya wanadamu haikuletwa na Mungu. Yeye alifanya mwanadamu wa kwanza akiwa mkamilifu, akwa sifa kwa uwezo Wake wa kuumba. Mungu hana kasoro. Mungu alisaidiwa na Mwanawe pekee akamfanya mwanadamu wa kwanza “kwa mfano wetu kwa sura yetu.” Mwanadamu wa kwanza, Adamu, alikuwa mfano wa ukamilifu wa kimungu na kwa hiyo ili awe mfano halisi alipaswa kuwa mkamilifu.—Mwa. 1:26-28; 2:7, 8
7. Wakati Adamu alipokuwa Edeni, kulikuwa na hali gani kati ya mbingu na dunia kumfurahisha Mungu?
7 Katika Bustani ya Edeni iliyokuwa paradiso mwanadamu wa kwanza alitembea kulingana na roho takatifu ya Mungu. Mara kwa mara alizungumza na Mungu. Mungu alitembea katika Bustani ya Edeni yenye kupendeza, naye Adamu alijua hivyo ingawa hakumwona. Huo ulikuwa umoja kati ya Mungu na mwanadamu. Wakati huo kulikuwa na umoja kati ya vitu vya mbinguni na vya duniani. Kwa sababu gani? Kwa sababu roho ya Mungu ilikuwa ikienea pote. Hilo lilimfurahisha Yehova Mungu. Yeye “ndiye Mungu wa furaha.”—1 Tim. 1:11, NW.
8. Ni kwa sababu ya dhambi ya namna gani hatuna taratibu ya mambo makamilifu duniani leo, nayo dhambi hiyo ilitendwa na nani?
8 Hapa, sasa, ulikuwako msingi wa kuendelea kwa utaratibu mzuri kabisa wa mambo ambao usingezeeka wala kukaribia kutoweka. Lakini leo hatuna taratibu ya mambo safi, yenye haki wala kamilifu. Kwa sababu gani? Ni kwa sababu dhambi imetendwa juu ya roho takatifu. Ikatendwa na nani? Ikatendwa na yule ambaye Yesu Kristo alimtambua wakati alipokuwa akiongea na wanaume waliotaka sana kumwua yeye kwa sababu ya kusema kweli ya Mungu. Yesu aliwaambia hao ambao wangekuwa wauaji hivi: “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; Wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye, ni mwongo, na baba ya huo.”—Yohana 8:44.
9. Ni nani baba wa kiroho wa mtu mwenye kuzoea dhambi, sababu gani?
9 Mtu wa kwanza kutenda dhambi juu ya roho takatifu atambulishwa pia na mwanafunzi wa Yesu aitwaye Yohana, aandikaye hivi: “Atendaye dhambi ni wa Ibilisi, kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo.” (1Yohana 3:8) Mtu huyo mwenye kuzoea dhambi hawezi kuwa na baba mwingine wa kiroho, bali aliyemfanya aanze mwendo huo ndiye baba yake.
10. Mwongo wa kwanza alijifanyaje mwenycwe kuwa Ibilisi?
10 Mtajo huu wa mwongo wa kwanza katika kuumba kote kuwa Ibilisi waonyesha kwamba uongo wake ulimpinga Mungu, kwa maana jina Ibilisi lamaanisha Mchongeaji. Aliiacha kweli akasitawisha ndani yake mwenyewe nia ya kusema uongo. Ibilisi alipinga yale ambayo Mungu alikuwa amemwambia Adamu, akamwambia Hawa, mke wa Adamu, kwamba adhabu ya kula katika mti uliokatazwa isingekuwa kifo: “Hakika hamtakufa, kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.” (Mwa. 3:1-5) Mwongo huyo alijifanya mwenyewe Ibilisi, kwanza kuhusu Mungu.
11. Pengine Ibilisi alitumia mpango gani wa hila kuzuia Mungu asitimize neno lake Adamu na Hawa wakitenda dhambi?
11 Mchongeaji huyo wa Mungu asingeweza kuhakikisha kabisa kwamba Adamu na Hawa wasingekufa hakika wakila tunda lililokatazwa la mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Neno lake halikuwa lenye nguvu zaidi kuliko la Mungu. (Ebr. 4:12; Mwa. 2:16, 17) Lakini inaelekea kwamba Ibilisi alidhani angeweza kumweka Yehova Mungu katika hali yenye aibu ambayo ingefanya isipatane na uamuzi wake wa kuwaua Adamu na Hawa, hasa Ibilisi akifanya wanadamu hao wawili wenye dhambi wale katika “mtu wa uzima” kabla hawajatangaziwa hukumu yao na Mungu.—Mwa. 2:9; 3:22, 23.
12. Ibilisi akawaje mwuaji, na ni nini kinachomngojea sasa?
12 Ijapokuwa Ibilisi alitumia ujanja wote huo, akawa bado mwongo. Mateka wake walikufa kama nafsi za kibinadamu, kwa maana Yehova Mungu aliye Mwamuzi aliwahukumu wafe akaendelea kuwazuia wasiufikie “mtu wa uzima” kwa kuwafukuza katika Bustani ya Edeni iliyokuwa paradiso. (Mwa. 3:17-24) Kwa sababu ya kusababisha kifo cha mwanamume wa kwanza na mke wake bila upendo, Ibilisi akawa “mwuaji.” Alistahili kuuawa kulingana na sheria inayotajwa na Mwanzishi wa Ukristo: “Ye yote atakayemkosesha mmojawapo wa hawa waniaminio, afadhali afungiwe jiwe la kusagia shingoni mwake, na kutupwa baharini.” (Marko 9:42) Ndivyo ilivyo, uharibifu wa milele unamngojea mwuaji huyo, Ibilisi.
13. Yehova alimfananisha Ibilisi na nani, na kabla hajauawa anaruhusiwa kutokeza nini?
13 Mwisho huo wa Ibilisi ulionyeshwa wakati Mwamuzi wa wote, Yehova, alipomfananisha na nyoka aliyetumiwa kumdanganya mwanamke Hawa ale tunda lililokatazwa na Mungu. Akimwaambia Nyoka wa mfano, Yehova alisema: “Kwa sababu umefanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako; nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, naye utamyonda kisigino.” (Mwa. 3:14, 15) Hivyo Ibilisi ndiye aliyelaaniwa na Mungu. Kwa hiyo ni juu ya Mungu kumwua mlaaniwa huyo. Lakini hilo lisingetukia kabla ya Nyoka aliyelaaniwa kupata nafasi ya kuwa na “uzao,” wazao wa kiroho. Kwa kuwa Ibilisi ni roho, yeye hakurithi nguvu za uzazi kama mwanadamu.
14. Kutambaa kwa tumbo kwa njia ya mfano kulimaanisha nini kwa Ibilisi kama Nyoka Mkuu, naye aliungwa na nani katika cheo chake cha kushushwa?
14 Yehova alimfananisha Ibilisi na nyoka atambaaye kwa tumbo lake na kula chakula chenye mavumbi ya visehemu vya udongo. Hivyo alionyesha vile ambavyo Ibilisi aliyelaaniwa sasa alivyoshushwa sana. Kwa kuwa alishushwa kwenye cheo cha chini zaidi kinachoweza kupatikana, kililinganishwa na mahali palipokuja kuitwa Tartaro. Baadaye roho wengine walijiunga na Ibilisi katika mahali hapo, malaika wengine waliokana Ubaba wa Mungu wakachagua kuwa wa Ibilisi. Roho hao wakawa “uzao” wake.
15. Petro na Yuda wanasema nini juu ya malaika waliojiunga na Nyoka Mkuu katika kutenda dhambi?
15 Akitaja uzao huo wa kiroho wa Nyoka wa asili, mtume Mkristo Petro aliandika hivi: “Mungu hakukosa kuadhibu malaika waliofanya dhambi, bali, kwa kuwatupa katika Tartaro, aliwapeleka kwenye mashimo yenye giza zito mno wawekwe akiba kwa hukumu.” (2 Pet. 2:4, NW) Mwanafunzi Mkristo Yuda anataja “uzao” uo huo wa malaika wa Nyoka, anapoandika hivi: “Malaika wasiolinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu.”—Yuda 6.
16. Kwa sababu gani Ibilisi alimdanganya Hawa atende dhambi akiwa peke yake, na kwa sababu gani wengine wanadhani alikuwa amekuwa kerubi?
16 Wakati ambao Ibilisi alimdanganya Hawa, mke wa Adamu, amwasi Mungu Baba yake wa mbinguni, Nyoka Mkuu hakuwa na “uzao.” Ibilisi alichukua hatua akiwa peke yake. Yeye hakuchagua kuwa na mwenzi-malaika ambaye angeweza kuwa mshindani wake katika kudai utawala juu ya wazao wa Adamu na Hawa. Alitamani sana yeye peke yake ndiye atawale wanadamu wote. Hatujui kabisa cheo alichokuwa nacho katika tengenezo la asili la Mungu. Wanafunzi wengi wa Biblia wameufahamu unabii wa Ezekieli 28:11-19 kuhusu mfalme wa Tiro wa kale kuwa wahusu Shetani Ibilisi pia, na hivyo wanawaza kwamba Ibilisi aliyejifanya mwenyewe alikuwa “kerubi” kati ya “wana wa Mungu” wa mbinguni. Ikiwa ndivyo, basi hiyo yaongeza uzito wa kushushwa kwake kama Nyoka Mkuu.
17. Ni kwa njia gani malaika waasi wanakuwa katika giza moja la Tartaro pamoja ,na Ibilisi?
17 Wale malaika wengine waliomwasi Mungu, ambao wakawa “uzao” wa Nyoka, wamo pamoja naye katika giza la Tartaro, wakiwa kama nyoka waliolaaniwa. Hawana tena nuru ya upendeleo wa mashauri ya Mungu. Walipoasi Mungu aliondoa roho takatifu yake ndani yao.
18. (a) Kwa sababu gani wakati ujao una giza tititi kwa Ibilisi na mashetani wake? (b) Ulizo la fumbo lililotokezwa sasa lilikuwa ulizo gani?
18 Wakati ujao ni wenye giza tititi kwa Nyoka Mkuu na “uzao” wake wa malaika. Siku ya hukumu ya Mungu yawangojea, nao wana taraja la ‘kupondwa katika kichwa.’ Mungu atatumia “uzao” wa “mwanamke” wake kuwaponda hivyo. (Mwa. 3:15) Jeraha watakalotiwa si kidonda cha ngozi ya kichwa tu. Ni kupondwa kwa kichwa chenyewe, kutakakomwua Nyoka Mkuu na “uzao” wake. Huo ndio ufahamu wa kweli kabisa, kwa maana katika Warumi 16:20, imeandikwa juu ya wanafunzi wa Kristo hivi: “Mungu wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi.” Hiyo ni sababu ya kutosha kumfanya Shetani na “uzao” wake wawe adui za “uzao” wa “mwanamke” wa Mungu. Mungu alipotaja “uzao” wa “mwanamke” wake, kulitokea fumbo katika mbingu na dunia. Fumbo hilo au siri takatifu ambalo sasa ulimwengu wote ulitaka kujua maana yake lilikuwa, Uzao huu wa mwanamke ni nani?
—Kutoka Holy Spirit the Force Behind the Coming New Order, Sura ya 3.