Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yy sura 5 kur. 35-42
  • Punyeto na Ngono za Wanaume kwa Wanaume na Wanawake kwa Wanawake

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Punyeto na Ngono za Wanaume kwa Wanaume na Wanawake kwa Wanawake
  • Kupata Faida Zote za Ujana Wako
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MAONI JUU YA CHANZO CHA JUU ZAIDI
  • MAZOEA YA NGONO ZA WANAUME KWA WANAUME NA WANAWAKE KWA WANAWAKE
  • KUSHINDA KWA KUJIWEZA
  • Kuacha Kupiga Punyeto—Kwa Sababu Gani? kwa Njia Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1974
  • Ninaweza Kushinda Jinsi Gani Mazoea ya Kupiga Punyeto?
    Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 1
  • Shinda Zoea la Kupiga Punyeto
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
  • Kuendelea Kuwa na Maoni ya Mungu Juu ya Ngono
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
Pata Habari Zaidi
Kupata Faida Zote za Ujana Wako
yy sura 5 kur. 35-42

Sura ya 5

Punyeto na Ngono za Wanaume kwa Wanaume na Wanawake kwa Wanawake

1-4. (a) Kupiga punyeto ni nini? (b) Kwa sababu gani si vizuri kuwa na mazoea mabaya hata ikiwa watu wengi wanayo? (c) Sababu gani tupendezwe na vile Mungu anavyoona jambo hili?

JE! NAMNA miili ya wavulana na wasichana inavyokua wakati wa kubalehe hata wanaweza kuzaa watoto si jambo la kustaajabisha? Kwa kawaida maoni yako juu ya wanaume na wanawake yanageuka wakati mwili wako unapopata mageuzo hayo. Uvutano unaongezeka, na mara nyingi wavulana wanapendezwa sana na wasichana, nao wasichana wanapendezwa na wavulana. Lakini labda unatamani na kutaka sana kujua vilevile juu ya mwili wako mwenyewe unaogeuka haraka. Je! utajuaje? Je! ujaribu kutumia viungo vyako vya ngono ? Je! kuna ubaya wo wote wa kusugua viungo vya uzazi kwa njia fulani mpaka viamke sana?

2 Mazoea haya yanaitwa kupiga punyeto. Ni mazoea ya kawaida sana. Mwandikaji mmoja anasema hivi juu ya kupiga punyeto: “Kila uchunguzi wetu wa uangalifu wa habari za hesabu unaonyesha waziwazi kwamba . . . kadiri isiyopungua 95 kwa mia ya wavulana na vijana wanaume wenye umri wa miaka kati ya kumi na mitatu na 25 wanazoea kupiga punyeto kwa muda ulio tofauti-tofauti.” Kwa habari ya wasichana, mwandikaji uyu huyu anasema kwamba “kadiri ya 40 mpaka 50 kwa mia wanapatikana wakipiga punyeto.” Watu wengine wanasema kwamba hesabu hizo zahakikisha wenye kupiga punyeto wana afya na kwamba “inasikitisha sana ikiwa kijana mwenye afya hapigi punyeto.”

3 Basi, wewe waonaje? Unakubali kwamba kupiga punyeto ndiyo kawaida ya mwili kwa sababu kumekuwa ndiyo mazoea ya ulimwengu leo? Kusema uongo na wivi ni mambo ya kawaida leo vile-vile. Hata hivyo, je! ungedhani inafaa kusema uongo na kuiba? Ile homa ya mafua imeenea mahali pote, lakini je! wataka homa ya mafua kwa sababu imeenea mahali pote? Basi namna gani vile wanavyodai kwamba kupiga punyeto si kubaya?

4 Kwa habari ya mwili, madaktari wengi wanasema kwamba si vibaya kupiga punyeto mara chache. Wanasema kama madaktari wa magonjwa ya akili, kwamba ni vibaya tu wakati mpiga punyeto anapokuwa na maoni yenye hatia, hatia inayosumbua akili na moyo kisha kuchafua afya ya mwili. Lakini madaktari ni wanadamu wenye makosa, wanakosea, na maoni yao yanageuka. Hata hivyo, kuna mahali imara pasina makosa wala uamuzi mbaya ambapo vijana wanaweza kupata shauri. Hapo ni Neno la Mungu. Na ikiwa twataka uzima wa milele kwa kupendelewa na Mungu, kuliko kutaka maisha nyingi tu, imetupasa tutafute hekima na shauri lake. Yeye aweza kutufanyia wasiyoweza kutufanyia wanadamu ili tuwe na furaha.

MAONI JUU YA CHANZO CHA JUU ZAIDI

5, 6. (a) Lile shauri lililo katika Wakolosai 3:5 linapasaje kupiga punyeto? (b) Ni kwa sababu gani Biblia inashirikisha mazoea haya na “kutamani”?

5 Basi, jambo lenyewe si kadiri kupiga punyeto kunavyoweza kuumiza mwili, bali ni kama kunaumiza kiroho. Kweli, maneno haya “kupiga punyeto” na “kujichua” hayaonekani katika Biblia. Lakini wafahamu nini kutokana na shauri lililoongozwa na Mungu ambalo mtume Paulo alitoa katika Wakolosai 3:5, NW? Anawaambia wale wasiotaka kupoteza kibali ya Mungu hivi: “Kwa hiyo, vitulizeni [Msiamshe] viungo vyenu vya mwili vilivyopo duniani kwa habari ya uasherati, uchafu, nyege, tamaa zenye kudhuru, na kutamani.” Tofauti na uasherati, kupiga punyeto ni jambo ambalo mwanamume au mwanamke anaweza kufanya peke yake. Lakini maana yake ndiyo kusema kupiga punyeto si kuchafu? Je! maana yake si kutawalwa na “nyege”?

6 Tena, mtume anaandika juu ya wale ambao “wanajitia katika mambo ya ufisadi wapate kufanyiza kila namna ya uchafu kwa kutamani.” (Waefeso 4:19) Katika barua yake aliyoandikia Wakolosai ambayo maneno yake yametumiwa katika fungu lililotangulia, Paulo alitaja “kutamani” na vilevile katika fungu hili la maneno. Kwa kweli, kupiga punyeto kwaonyesha tabia hizo mbaya. Namna gani? Kwani ni kutamani kitu kisicho mali yako. Mungu amefanya mpango wa ndoa ili kutoshelezea nyege. Lakini kwa kweli mpiga punyeto anataka kuona raha hiyo pasipo malipo. Malipo ni kutwaa na kutimiza madaraka yanayofuatana na ndoa. Fahamu katika neno hili kwamba mtume aliposhauri watu ‘waliowashwa tamaa,’ hakuwaambia watafute kutuliza tamaa hiyo kwa kupiga punyeto, bali kupitia kwa ndoa, ambao ni mpango wa Mungu.—1 Wakorintho 7:2, 9.

7, 8. (a) Kama kupiga punyeto ni mazoea, kunawezaje kumharibia mtu asiwe na matumaini ya ndoa yenye furaha? (b) Sababu gani lingekuwa kosa kudhani kwamba kupiga punyeto ni njia inayofaa ili kuepuka kuvunja vibaya sheria ya Mungu?

7 Kwa kweli, kupiga punyeto kwaweza kukufanya usifurahie ndoa wakati ujao. Ikiwa mwanamume au mwanamke amezoea kutuliza nyege zake kwa kupiga punyeto, anasitawisha mazoea ya kufikiria raha yake mwenyewe. Lakini katika ndoa kuna lazima, hasa upande wa mwanamume, kufikiria vilevile raha na furaha ya mwenzake. Bila kufanya hivyo, hali ya ndoa inaharibika polepole kisha uchungu na hali ya kukata tamaa inatokea. Hali hii ndiyo mojawapo la magumu makubwa kuliko yote yanayotokea katika ndoa, yaani, waume kufikiria furaha yao wenyewe wasifikirie mahitaji ya wake zao. Mengi kati ya hayo yanatokana na mazoea ya kupiga punyeto kabla ya ndoa.

8 Pengine watu watauliza hivi: “Lakini namna gani kama mtu ni mdogo sana asistahili kuoa au kuolewa? Je! kupiga punyeto kusingemzuia asivunje vibaya zaidi sheria ya Mungu, kama kufanya uasherati au ngono za wanaume kwa wanaume na wanawake kwa wanawake, anapongojea ndoa baadaye?” Huenda ikaelekea kuwa hivyo. Lakini je! huko ni kuwaza kuzuri? Hapana. Kupiga punyeto kunaifanya dhamiri njema izoee mabaya na kushindwa kumwonya mtu juu ya hayo. Kupiga punyeto kunaweza kuwa mazoea ambayo mwanamume au mwanamke anafanya kila anapoona mkazo wa namna yo yote kama vile dawa za kulevya, hata akose uwezo wa kufanya bidii ashinde magumu yanayoleta wasiwasi huo. Kwa hiyo kunaweza kutokeza mabaya juu ya mabaya na mwishowe kumfanya mtu awe mtumwa wake. Lakini Mungu anatuambia tuitawale miili, tusiiruhusu itutawale sisi.

MAZOEA YA NGONO ZA WANAUME KWA WANAUME NA WANAWAKE KWA WANAWAKE

9-13. (a) Mara nyingine kupiga punyeto kunamwelekezaje mtu kwenye ngono za wanaume kwa wanaume na wanawake kwa wanawake? Je! ye yote anayefanya ngono na mwanamume mwenzake au na mwanamke mwenzake alizaliwa hivyo? (b) Mungu anaonaje, mazoea hayo? (c) Je! yawezekana kujitenga nayo? (Warumi 1:24-27; Mambo ya Walawi 18:22, 23; 1 Wakorintho 6:9-11)

9 Bila shaka kujiacha ushindwe na nyege kwa kupiga punyeto hakutakupa nguvu za kushinda kishawishi cha kufanya uasherati au hata ngono za wanaume kwa wanaume na wanawake kwa wanawake (homosexuality). Mahali pake, kunasitawisha fikira mbaya na tamaa mbaya. Kwa kweli, kupiga punyeto kwaweza kuongoza wanaume na wanawake wafanye ngono wao kwa wao. Wakati mtu anaona hatosheki na ngono anayofanya peke yake, anatafuta mwenziwe wapate kuchocheana nyege.

10 Tendo hili linatokea mara nyingi zaidi kuliko unavyojua. Tofauti na vile watu wengi wanavyowaza, wanaume na wanawake wanaofanya ngono wao kwa wao hawazaliwi wakiwa na tabia hiyo, ila wanajifunza. Mara nyingi mtu anaanza tabia hiyo akiwa mchanga sana kwa kushikashika viungo vya uzazi vya mwenzake, kisha anaanza ngono na mwanamume mwenzake au mwanamke mwanzake. Kijana mmoja wa kiume anasimulia hivi:

11 “Nilipokuwa mchanga, sikuongozwa sana na wazazi. Niliruhusiwa kujiongoza na kufanya nilivyotaka tu. Ni wakati nilipopata umri wa miaka minane binamu zangu wakubwa waliponielekeza kwenye ngono za wanaume kwa wanaume. Nikaona kuna raha ya kufanya hivyo, basi nikaendelea kufanya ngono hizo pamoja nao kisha na wengine. Muda si muda ikawa kazi ya karibu kila siku. Kwanza sikujua ikiwa ninafanya jambo lo lote baya. Wazazi wangu hawakuwa wamenifunza juu ya mwenendo mwema, nami sikuwatumaini hata kidogo.

12 “Wakati huu tulikuwa tukiishi katika nchi moja ya Amerika ya Kati. Mwisho tukahamia mjini New York, nilikomalizia masomo ya juu. Niliendelea vilevile na ngono za wanaume kwa wanaume. Shule na mji zilijaa tele wanaume na wanawake wenye kufanya ngono wao kwa wao, kwa hiyo zilikuwako nafasi tele. Nilipoendelea kukua niwe mtu mzima nikajua kwamba yale niliyokuwa nikifanya si mambo ya akili, na hayakuwa mazuri. Lakini nikaendelea kufanya hivyo kwa sababu nilitaka hivyo. Ngono hizi zikawa zimenivuta sana.”

13 Kijana huyo alivutwa sana na mazoea hayo, na aliweza kuyashinda kwa kujitahidi sana tu. Ni nini kilichomwongoza ageuke? Ni kutaka kumpendeza Yehova Mungu. Alipofahamu kwamba Mungu aona ngono za wanaume kwa wanaume na wanawake kwa wanawake kuwa “si mambo ya akili,” na kwamba anayakataa kabisa, kijana huyo aliyapinga sana mazoea hayo mpaka akayashinda. Neno la Mungu linasema waziwazi sana juu ya jambo hili hivi: “Msikosee: mwasherati wala mwabudu sanamu, wala wenye hatia ya uzinzi wala wenye hatia ya ngono za wanaume kwa wanaume na wanawake kwa wanawake . . . hawataumiliki ufalme wa Mungu.”—1 Wakorintho 6:9, 10, The New English Bible.

KUSHINDA KWA KUJIWEZA

14-16. (a) Ni nini linaloweza kufanywa ili kuzuia nyege? (Wafilipi 4:8; 1 Wathesalonike 4:3-5) (b) Ukiona unazidiwa na nyege unaweza kufanya nini ili zitulie? (Zaburi 1:1, 2; 63:6, 7)

14 Fikira zako zinapasa maoni yako na mambo unayofanya. Kwa hiyo wataka nini hasa ? Je! wataka kuwa na maoni ya kusumbuliwa na nyege wakati wote, ukizoea kupiga punyeto, labda hata kuanza ngono za wanaume kwa wanaume na wanawake kwa wanawake? Ukijiacha ufikirie sana mambo ya ngono, hili laweza kukupata. Lakini kama wataka uzuie nyege hizo zisiharibu furaha yako ya maisha na kutimiza mambo yanayofaa, basi jiweze uanze kufikiria mambo mengine.

15 Usikubali kutazama picha na kusoma habari au mambo mengine yanayoamsha nyege. Ukijiacha uyafikirie mambo hayo au kuongea juu yake, utapata taabu na kusumbuliwa sana ndani ya mwili wako. Kwa sababu vile unavyozidi kutazama au kuzungumza mambo hayo ndivyo moyo wako utakavyovutwa zaidi. Na moyo wako ndio unaokuongoza sana utende.

16 Lakini kama unashikwa sana na nyege hata wakati wa hali za kawaida, hapo itakuwaje? Unaweza kuzituliza namna gani? Si kwa kupiga punyeto, bali kwa kugeuza akili, moyo na mwili wako ufikirie mambo mengine. Unaweza kufanya kazi, kufanya mazoezi ya mwili, kucheza au kwenda kutembea. Inafaa kutafuta mtu wa kuzungumza naye, mtu unayeheshimu, hata unaweza kumpigia simu mtu huyo ikiwa lazima. Kusoma Biblia au vitabu vinavyoeleza mambo ya Biblia kwa sauti kuu ni mmojawapo wa misaada bora sana. Na zaidi ya yote, mwambie Baba yako wa kimbinguni Yehova Mungu, gumu hilo katika sala.”

17-20. (a) Kugeuza mazoea ya kulala, ya kula na ya usafi kunawezaje kumsaidia mtu? (b) Hata ikiwa mtu anaona anajitahidi sana ili afanye mema, sababu gani asidhani ni kazi bure? (Zaburi 103:13, 14)

17 Kwa kweli, yako mambo mengine mengi ambayo ni mepesi na ya busara anayoweza mtu kufanya yamsaidie aepuke au apunguze nyege. Kuwa pamoja na wengine ambao ni watu wenye tabia nzuri ni ulinzi. Ikiwa unalala chumbani peke yako na unaona unasumbuliwa sana usiku na nyege, unaweza kufanya mpango wa kushiriki chumba kimoja na mtu mwingine wa jamaa yako. Labda utaona inafaa vilevile kulala kibavu kuliko kulala mgongoni au kifudifudi.

18 Jambo jingine linaloweza kusaidia ni kuhakikisha kwamba mavazi yako hayasugui sana viungo vya uzazi. Jaribu kuhakikisha kwamba kabla ya kulala mambo unayosoma na kuzungumza yanatuliza nyege kuliko kuziamsha. Jambo hili ni kutia vilevile cho chote unachokula wakati huu. Wengine wameona kwamba wanalala usingizi mzuri zaidi na hawaamshwi nyege ikiwa wanakula na kunywa kidogo kabla ya kulala. Na jambo lenye maana sana kwa wanaume na wanawake ni kuwa safi. Uchafu unaweza kufanya viungo vya uzazi kuwasha na kumfanya mtu aanze kuvisugua. Unaweza kuwauliza wazazi wako wakueleze habari za usafi wako.

19 Inafaa mara nyingine kusafisha viungo vya uzazi na, pengine kwa kufanya hivyo, mtu atadhani angeshawishwa avitumie vibaya. Lakini pengine utaona kwamba utunzaji huo utakusaidia kuwa na maoni mazuri zaidi juu ya viungo hivi kwa sababu una kusudi zuri, kusudi la kuepuka nyege. Utafahamu kwamba viungo hivi havikukusudiwa vikutawale wewe na maisha yako yote.

20 Kama unayapinga sasa mazoea ya kupiga punyeto, kumbuka: Bila shaka wewe si mtu wa kwanza kupatwa na ugumu huu. Usidhani hata kidogo kwamba Yehova Mungu na Mwanawe Yesu Kristo wamekuacha, hata ijapokuwa unaona unajitahidi sana uache mazoea ya kupiga punyeto. Ukiendelea kujitahidi sana uyashinde, watakusaidia kwa njia nzuri na kwa uvumilivu uongeze nguvu zinazohitajiwa upate kushinda.

[Blabu katika ukurasa wa 39]

Je! wanaume na wanawake wanaofanya ngono wao kwa wao wanazaliwa hivyo, au wanajifunza tabia hiyo?

[Picha katika ukurasa wa 41]

DJe! ni sawa kusoma habari yo yote?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki