Misaada Mingine kwa Ajili ya Jamaa Yako
Je! ungependa misaada mingine yenye thamani kwa ajili ya jamaa yako? Waweza kupata chochote cha vifuatavyo au vyote kwa kuandikia I.B.S.A., ukitumia anwani ifaayo katika ukurasa ufuatao.
Kumsikiliza Mwalimu Mkuu. Kitabu hiki pia kimetungwa kwa ajili ya watoto wachanga. Chatumia njia za kufundisha ambazo huvuta watoto na wazazi waungane pamoja na kufanya kujifunza kuwe raha. Lengo kuu la kitabu hiki ni kufundisha watoto viwango vya maadili bora ya Biblia. Kwa kuagiza wachanga katika kanuni zifaazo za maisha, wewe utaweza kuwasaidia kweli kweli wakabiliane na matatizo ya kisasa. Ni chenye vielezi vya kupendeza, herufi kubwa, mpangilio wa maneno yenye kueleweka kwa urahisi, jalada gumu, ukubwa wa mfukoni, kurasa 192.
Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi. Kitabu hiki kitasaidia matineja wakinze mavutano ya ukosefu wa adili ya ulimwengu wa leo. Kutofuata haki, utumizi mbaya wa vileo na dawa za kulevya, maadili ya ngono, kufanya urafiki na mtu wa jinsia tofauti na utafutaji wa mapenzi ni baadhi ya habari zenye kuzungumzwa. Ni chenye jalada gumu, kurasa 320.