Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 1
  • Mungu Aanza Kuumba Vitu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mungu Aanza Kuumba Vitu
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Mungu Aliumba Mbingu na Dunia
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Mfumo Wetu wa Pekee wa Jua—Jinsi Ulivyotokea
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Mungu Alianza Lini Kuumba Ulimwengu?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Ni Nani Aliyeviumba Vitu Vyote?
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
Pata Habari Zaidi
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 1
Sayari ya dunia ya zamani iliyofunikwa na bahari, mawe na volkano

HADITHI YA 1

Mungu Aanza Kuumba Vitu

VITU vizuri vyote tulivyo navyo vimetoka kwa Mungu. Aliumba jua litupe mwangaza mchana, mwezi na nyota usiku. Tena Mungu akaumba dunia tukae ndani yake.

Lakini kwanza Mungu hakuumba jua, mwezi, nyota na dunia. Unajua alivyoumba kwanza? Mungu aliumba watu walio kama yeye. Hatuwezi kuona watu hao, kama vile hatuwezi kumwona Mungu. Biblia inawaita watu hao malaika. Mungu aliumba malaika wakae na yeye mbinguni.

Malaika ambaye Mungu aliumba kwanza alikuwa wa pekee sana. Alikuwa Mwana wa kwanza wa Mungu, akafanya kazi pamoja na Baba yake. Alimsaidia Mungu kuumba vitu vingine vyote. Tena alimsaidia Mungu kuumba jua, mwezi, nyota na dunia yetu.

Wakati huo dunia ilikuwa namna gani? Mwanzoni mtu hangeweza kukaa duniani. Nchi yote ilikuwa bahari kubwa. Lakini Mungu alitaka watu wakae duniani. Akaanza kutayarisha makao yetu. Alifanya nini?

Kwanza dunia ilitaka nuru. Basi Mungu akaifanya nuru ya jua iangazie dunia. Alifanya hivyo ili kuwe usiku na mchana. Kisha Mungu akatokeza nchi kavu juu ya maji ya bahari.

Kwanza nchi haikuwa na kitu. Ilikuwa kama picha unayoona hapa. Maua hayakuwapo, wala miti wala wanyama. Hata samaki hawakuwamo baharini. Mungu alikuwa na kazi zaidi ili dunia iwe makao yanayofaa sana ya wanyama na watu.

Yeremia 10:12; Wakolosai 1:15-17; Mwanzo 1:1-10.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki