Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 1 uku. 8-uku. 9 fu. 4
  • Mungu Aliumba Mbingu na Dunia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mungu Aliumba Mbingu na Dunia
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Mungu Aanza Kuumba Vitu
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Wanyama
    Amkeni!—2015
  • Bustani Nzuri
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Ni Nani Aliyeviumba Vitu Vyote?
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 1 uku. 8-uku. 9 fu. 4
Bustani ya Edeni

SOMO LA 1

Mungu Aliumba Mbingu na Dunia

Yehova Mungu ndiye Muumba wetu. Yeye aliumba vitu vyote, vinavyoonekana na visivyoonekana. Kabla ya kuumba vitu tunavyoona, aliumba malaika wengi sana. Je, unajua malaika ni nani? Malaika ni viumbe ambao waliumbwa na Yehova, walio kama yeye. Hatuwezi kuwaona kama vile ambavyo hatuwezi kumwona Mungu. Yehova alimuumba malaika wa kwanza na huyo akawa msaidizi wake. Malaika huyo alimsaidia Yehova kuumba nyota, sayari, na vitu vingine vyote. Dunia yetu maridadi ni moja kati ya sayari hizo.

Kisha, Yehova aliitayarisha dunia ili wanadamu na wanyama waishi. Alifanya mwanga wa jua uangaze duniani. Aliumba milima, bahari na mito.

Alifanya nini baadaye? Yehova akasema: ‘Nitaotesha nyasi, mimea na miti.’ Miti ya matunda ya aina mbalimbali, mboga na maua yakaanza kumea. Kisha, Yehova akaumba wanyama wote—wanaoruka, wanaotambaa na wanaoogelea. Aliwaumba wanyama wadogo kama vile sungura, na wanyama wakubwa, kama vile tembo. Ni mnyama gani unayempenda?

Kisha, Yehova akamwambia yule malaika wa kwanza: “Na tufanye mtu.” Wanadamu wangekuwa tofauti na wanyama. Wangeweza kubuni vitu, kuzungumza, kucheka, na kusali. Wangetunza dunia na wanyama. Je, unajua mwanadamu wa kwanza aliitwa nani? Acha tuone.

“Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.”​—Mwanzo 1:1

Maswali: Yehova Mungu ni nani? Yehova aliumba nini?

Mwanzo 1:1-26; Methali 8:30, 31; Yeremia 10:12; Wakolosai 1:15-17

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki