Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 2
  • Bustani Nzuri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Bustani Nzuri
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Mungu Aliumba Mbingu na Dunia
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Ni Nani Aliyeviumba Vitu Vyote?
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
  • Sababu Walipoteza Makao Yao
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Aliyefanya Vitu Vyote
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
Pata Habari Zaidi
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 2
Wanyama, maua, miti, na maji yanayotiririka katika bustani nzuri ya Edeni

HADITHI YA 2

Bustani Nzuri

TAZAMA dunia hii! Kila kitu ni kizuri sana! Tazama majani na miti, maua na wanyama wote. Unaweza kumjua tembo na simba hapa?

Bustani hii nzuri ilitokea namna gani? Na tuone Mungu alivyotuwekea dunia tayari.

Kwanza, Mungu aliumba majani mabichi yaifunike nchi. Alifanya namna zote za mimea na miti midogo. Mimea hiyo inapamba dunia. Zaidi ya hivyo, mimea mingi inatupa chakula kitamu sana.

Tena Mungu aliumba samaki waogelee katika maji na ndege waruke katika anga. Aliumba mbwa na paka na farasi; wanyama wakubwa na wadogo. Ni wanyama gani wanaokaa karibu na nyumba yenu? Je! si vizuri kufurahi kwa vile Mungu alitufanyia vyote hivyo?

Halafu, Mungu alifanya sehemu moja ya dunia kuwa ya pekee sana. Aliita bustani ya Edeni. Ilikuwa nzuri sana. Kila kitu ndani kilikuwa kizuri. Mungu alitaka dunia nzima iwe kama bustani nzuri hii.

Lakini tazama tena picha hii ya bustani. Je! unajua kitu ambacho Mungu aliona hakipo? Tuone.

Mwanzo 1:11-25; 2:8, 9.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki