Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • te sura 3 kur. 15-18
  • Aliyefanya Vitu Vyote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Aliyefanya Vitu Vyote
  • Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Nani Aliyeviumba Vitu Vyote?
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
  • Mungu Aanza Kuumba Vitu
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Mungu Aliumba Mbingu na Dunia
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Kumwonyesha Mungu Kuthamini Kwetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
Pata Habari Zaidi
Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
te sura 3 kur. 15-18

Sura ya 3

Aliyefanya Vitu Vyote

MIMI najua ajabu fulani. Ungependa kuisikia?— Tazama mkono wako. Kunja vidole vyako. Sasa okota kitu. Mkono wako waweza kufanya mambo mengi, na waweza kuyafanya vizuri. Unamjua aliyefanya mkono wako?— Alikuwa Mungu.

Sasa tazama uso wangu. Unaona nini?— Unaona kinywa changu, pua yangu na macho yangu mawili. Waweza kuviona namna gani?

Kwa macho yako mwenyewe. Na nani aliyefanya macho?— Alikuwa Mungu. Si ajabu hiyo?—

Unaweza kuona vitu vingi kwa macho yako. Unaweza kutazama maua. Unaweza kuona ndege. Unaweza kutazama majani mabichi na anga la buluu.

Lakini nani aliyefanya vitu hivi?— Je! mwanadamu fulani alivifanya? Hapana. Wanadamu wanaweza kufanya nyumba. Lakini mwanadamu hawezi kufanya majani yanayomea. Wanadamu hawawezi kufanya ndege, maua au kitu kingine cho chote chenye uhai. Unajua hilo?—

Mungu Ndiye aliyefanya vitu hivi vyote. Mungu alizifanya mbingu na dunia. Yeye alifanya watu vile vile. Yeye alimwumba mwanamume wa kwanza na mwanamke wa kwanza. Yesu, Mwalimu Mkuu, alifundisha hili.—Mathayo 19:4-6.

Yesu alijua namna gani kwamba Mungu alimfanya mwanamume na mwanamke? Je! Yesu alimwona Mungu akifanya? Ndiyo. Yesu alikuwa pamoja na Mungu wakati Mungu alipomfanya mwanamume na mwanamke. Yesu alikuwa mtu wa kwanza ambaye Mungu aliumba. Yeye alikuwa malaika, naye aliishi akafanya kazi mbinguni pamoja na Baba yake.

Biblia inatuambia kwamba Mungu akasema: “Na tufanye mtu.” Unajua ambaye Mungu alikuwa akisema naye? Alikuwa akisema na Mwana wake ambaye nyuma alikuja duniani akawa Mwalimu Mkuu!—Mwanzo 1:26.

Kila kitu ambacho Mungu amefanya kinaonyesha upendo wake. Mungu alifanya jua. Jua linatupa sisi nuru na kutupasha moto. Kila kitu kingekuwa baridi na kusingekuwako uhai duniani ikiwa tusingekuwa na jua. Wewe huoni furaha kwa vile Mungu alifanya jua?—

Tena Mungu ananyesha mvua. Mara nyingine labda hupendi mvua kwa sababu huwezi kwenda kucheza nje wakati mvua inakunya. Lakini mvua inasaidia maua kumea.

Basi wakati tunaona maua mazuri, tutamshukuru nani?— Mungu. Na imetupasa tum–shukuru nani tunapokula matunda na mboga tamu?— Imetupasa tumshukuru Mungu, kwa sababu jua lake na mvua yake inafanya vitu vimee. Mungu ni mzuri sana kwa kutufanyia sisi vitu hivi vyote vya ajabu.

Unajua Mungu yuko wapi?— Biblia yatuambia Mungu anaishi mbinguni.

Unaweza kumwona Mungu?— Hapana. Biblia inasema: ‘Hapana mtu awezaye kumwona Mungu.’ Hivyo mtu asijaribu kufanya picha au mfano wa Mungu. Mungu hata anatuambia tusijaribu kufanya sanamu yake. Basi tusiwe na vitu kama hivyo nyumbani mwetu, sivyo?⁠— —Kutoka 33:20; 20:4, 5.

Lakini ikiwa huwezi kumwona Mungu, wajuaje kweli kuna Mungu?— Fikiria hili. Je! waweza kuona upepo?— Hapana. Hapana mtu aweza kuona upepo. Lakini unaweza kuona vitu ambavyo upepo unafanya. Unaweza kuona majani yakipeperuka wakati upepo unavuma katika majani ya mti. Hivyo unaamini kuna upepo.

Tena unaweza kuona vitu ambavyo Mungu amefanya. Wakati unaona ua au ndege, unaona kitu fulani ambacho Mungu amefanya. Hivyo unaamini kweli kuna Mungu.

Pengine mtu atakuuliza hivi, “Nani aliyefanya jua na dunia?” Ungesema namna gani? Unaweza kusema Mungu alivifanya. Biblia inasema: “Mungu aliziumba mbingu na nchi.”—Mwanzo 1:1.

Namna gani mtu akikuuliza hivi, “Je! Mungu alifanya watu na wanyama vile vile?” Utasema namna gani? Mwambie: “Ndiyo, Mungu alifanya watu na wanyama. Mungu alifanya ndege vile vile.” Biblia inasema: ‘Mungu aliumba vitu vyote.’—Waefeso 3:9.

Labda mtu atakuambia kwamba yeye hamwamini Mungu. Hapo utasema namna gani? — Sababu gani usimwonyeshe nyumba? Mwulize mtu huyo: “Nani aliyefanya nyumba ile?” Mtu fulani alifanya. Nyumba haikujifanya yenyewe, sivyo? —

Mpeleke mtu huyo bustanini mwonyeshe ua. Mwulize: “Nani alifanya hiki? Si mwanadamu. Kwa kuwa nyumba haikujifanya yenyewe, ua hili halikujifanya lenyewe. Mtu fulani alilifanya. Mungu ndiye aliyefanya.

Mwulize mtu huyo asimame na kusikiliza wimbo wa ndege. Halafu mwulize: “Nani alifanya ndege akawafundisha kuimba?” Ni Mungu. Ni Mungu aliyezifanya mbingu na dunia na vitu vyote vyenye uhai! Ndiye anayetupa sisi uhai.

Lo! ni vizuri kuwa hai wee! Twaweza kusikia nyimbo nzuri za ndege. Twaweza kuona maua na vitu vingine ambavyo Mungu amefanya. Tena twaweza kula vyakula ambavyo Mungu ametupa.

Kwa vitu hivi vyote imetupasa tumshukuru Mungu. Zaidi ya yote, imetupasa tumshukuru kwa kutupa uhai. Ikiwa tunapiga asante kwa Mungu kweli kweli, tutafanya jambo fulani. Jambo gani? — Tutamsikiliza Mungu na tutamwabudu katika njia ambayo anatuambia katika Biblia. Katika njia hiyo twaweza kuonyesha twampenda Yeye aliyefanya vitu vyote.

(imetupasa tumshukuru Mungu kwa vitu vyote ambavyo amefanya. Namna gani? Soma yaliyoandikwa katika Zaburi 139:14, Ufunuo 4:11, Yohana 4:23, 24 na 1 Yohana 5:21.)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki