Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 3
  • Mwanamume na Mwanamke wa Kwanza

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mwanamume na Mwanamke wa Kwanza
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Mungu Aliumba Mwanamume na Mwanamke wa Kwanza
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Adui wa Mwisho, Kifo, Aangamizwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Adamu na Hawa
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Ikiwa Adamu Alikuwa Mkamilifu, Angeweza Jinsi Gani Kufanya Dhambi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
Pata Habari Zaidi
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 3
Adamu na Hawa wakiwa katika bustani ya Edeni

HADITHI YA 3

Mwanamume na Mwanamke wa Kwanza

UNAONA tofauti gani katika picha hii? Kuna watu. Mwanamume na mwanamke wa kwanza. Nani aliwaumba? Ni Mungu. Unajua jina lake? Ni Yehova. Mwanamume na mwanamke waliitwa Adamu na Hawa.

Yehova Mungu aliumba Adamu hivi. Alichukua mavumbi akafanya mwili mzuri wa mwanamume. Kisha akapuliza katika pua, Adamu akawa hai.

Yehova Mungu alimpa Adamu kazi ya kuwapa wanyama wote majina. Labda Adamu aliwatazama wanyama muda mrefu ili aweze kuwachagulia wote majina bora. Adamu alipokuwa akiwapa wanyama majina, aliona jambo fulani. Unajua ni jambo gani?

Wanyama wote walikuwa na wenzao. Tembo baba na mama walikuwapo, hata simba baba na mama. Lakini Adamu hakuwa na mwenzake. Basi Yehova akampa Adamu usingizi mzito, akachukua ubavu wake mmoja. Kwa ubavu huo, Yehova alimfanyia Adamu mke.

Adamu akafurahi! Wazia Hawa alivyofurahi alipowekwa katika bustani hiyo nzuri! Wangeweza kuzaa watoto wakae pamoja kwa furaha.

Yehova alitaka Adamu na Hawa wakae milele. Alitaka waifanye dunia nzima iwe nzuri kama bustani hii ya Edeni. Adamu na Hawa walifurahia sana hilo! Wewe ungependa kuifanya dunia iwe bustani nzuri? Lakini furaha ya Adamu na Hawa haikuendelea. Na tuone kwa nini.

Zaburi 83:18; Mwanzo 1:26-31; 2:7-25.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki