Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 27
  • Mfalme Mbaya Anatawala Misri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mfalme Mbaya Anatawala Misri
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Musa Aliamua Kumwabudu Yehova
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Kuvuka Bahari Nyekundu (ya Shamu)
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Yehova Ni Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
Pata Habari Zaidi
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 27
Waisraeli wakiwa watumwa wa Farao nchini Misri

HADITHI YA 27

Mfalme Mbaya Anatawala Misri

WANAUME hawa wanalazimisha watu kufanya kazi. Mtazame yule mwanamume anayempiga mfanya kazi mmoja kwa fimbo! Wafanya kazi hao ni wa jamaa ya Yakobo, nao wanaitwa Waisraeli. Na wanaume hao wanaowalazimisha kufanya kazi ni Wamisri. Waisraeli wamekuwa watumwa wa Wamisri. Ilikuwa hivyo namna gani?

Kwa miaka mingi jamaa ya Yakobo ilikaa kwa amani huko Misri. Yusufu, aliyekuwa mkuu katika Misri na wa pili kwa mfalme Farao, aliwaangalia vizuri. Lakini Yusufu akafa. Farao mpya, ambaye hakuwapenda Waisraeli, akawa mfalme wa Misri.

Basi Farao huyo mbaya akawafanya Waisraeli kuwa watumwa. Naye akaweka wasimamizi juu yao, wanaume waliokuwa wakali na bila huruma. Wakawalazimisha Waisraeli kufanya kazi ngumu wakijenga miji ya Farao. Lakini Waisraeli waliendelea kuongezeka. Baada ya muda mfupi Wamisri waliogopa kwamba Waisraeli wangekuwa wengi mno na wenye nguvu mno.

Watumwa Waisraeli wakitendewa isivyofaa na kupigwa na Wamisri

Unajua Farao alifanya nini? Aliwaambia wanawake waliosaidia akina mama Waisraeli wakati wa kuzaa watoto wao, akasema: ‘Ueni kila mtoto wa kiume anayezaliwa.’ Lakini wanawake hao walikuwa wazuri, hawakuwaua watoto wachanga.

Basi Farao akaamuru watu wake hivi: ‘Waueni watoto wachanga Waisraeli. Acheni tu watoto wa kike waishi.’ Ilikuwa amri mbaya sana, sivyo? Na tuone namna mtoto mmoja wa kiume alivyookolewa.

Kutoka 1:6-22.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki