Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 46
  • Kuta za Yeriko

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuta za Yeriko
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Rahabu Awaficha Wapelelezi
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Jinsi Lilivyo Tukufu Jina la Yehova!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Rahabu Anaficha Wapelelezi
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Rahabu alimwamini Yehova
    Wafundishe Watoto Wako
Pata Habari Zaidi
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 46
Yoshua anawaongoza Waisraeli wanaopaaza sauti na kupiga pembe huku kuta za Yeriko zikianguka

Hadithi ya 46

Kuta za Yeriko

NI NINI kinachoangusha kuta hizo za Yeriko? Ni kama zimepigwa na kombora kubwa. Lakini siku hizo hawakuwa na makombora; wala hawakuwa na bunduki. Ni mwujiza mwingine wa Yehova! Na tujifunze inavyotukia.

Sikiliza Yehova anavyomwambia Yoshua: ‘Wewe pamoja na watu wako wa vita zungukeni mji. Mzunguke mara moja kila siku muda wa siku sita. Mchukue na sanduku la agano. Makuhani saba watangulie na kupiga tarumbeta zao.

‘Siku ya saba mzunguke mji mara saba. Kisha mpige sauti ndefu ya tarumbeta zenu, na kila mtu apige yowe kuu ya vita. Kuta zitaanguka chini kabisa!’

Kuta za Yeriko zikianguka, isipokuwa za nyumba ya Rahabu ambayo kamba nyekundu inaning’inia

Yoshua na watu wanafanya kama Yehova anavyosema. Wanapozunguka, kila mtu yuko kimya. Hakuna anayesema. Sauti ya tarumbeta na mshindo wa miguu tu ndio unasikika. Bila shaka adui za watu wa Mungu waliogopa huko Yeriko. Unaiona ile kamba nyekundu inayoning’inia katika dirisha? Ni dirisha la nani lile? Ndiyo, Rahabu amefanya alivyoambiwa na wale wapelelezi wawili. Jamaa yake yote imo nyumbani ikitazama pamoja naye.

Mwishowe, siku ya saba, wakiisha kuuzunguka mji mara saba, tarumbeta yalia, watu wa vita wanapiga kelele, na kuta zaanguka. Ndipo Yoshua anasema: ‘Ueni kila mtu mjini. Okoeni tu fedha, dhahabu, shaba na chuma, mvipeleke kwenye hazina ya hema ya Yehova.’

Yoshua anawaambia wale wapelelezi wawili hivi: ‘Ingieni nyumbani kwa Rahabu, mmtoe yeye na jamaa yake yote.’ Rahabu na jamaa yake wanaokolewa, kama wale wapelelezi walivyokuwa wamemwahidi.

Yoshua 6:1-25.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki