HADITHI YA 71
Mungu Anatoa Ahadi ya Paradiso
HII ni picha ya paradiso ambayo labda Mungu alimwonyesha nabii wake Isaya. Isaya alikaa mara baada ya Yona kufa.
Paradiso ni “bustani” au “shamba zuri.” Je! inakukumbusha jambo ambalo tumeona katika kitabu hiki? Ni kama bustani nzuri ambayo Yehova Mungu alifanyia Adamu na Hawa, sivyo? Lakini dunia nzima itakuwa paradiso?
Yehova alimwambia nabii wake Isaya aandike habari za paradiso mpya inayokuja kwa ajili ya watu wa Mungu. Alisema: mbwa-mwitu na kondoo watakaa pamoja kwa amani. Ndama na simba-watoto watakula pamoja, na mtoto mdogo atawachunga. Hata mtoto mchanga hataumwa akicheza karibu na nyoka mwenye sumu.’
Mungu aliweka Adamu na Hawa katika paradiso. Walipoteza makao yao mazuri, wakazeeka na kufa, kwa sababu hawakumtii Mungu. Mungu anaahidi kuwapa watu wanaompenda vitu hivyo ambavyo Adamu na Hawa walipoteza.
‘Watu hawataumizwa wala kuharibiwa na kitu katika paradiso mpya inayokuja. Kutakuwako amani kamili. Watu wote watakuwa wenye afya na furaha. Itakuwa kama vile Mungu alivyotaka iwe hapo mwanzoni. Lakini tutajifunza baadaye namna Mungu atakavyotokeza hayo.