Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • my hadithi 99
  • Katika Chumba cha Juu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Katika Chumba cha Juu
  • Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Mlo wa Jioni wa Bwana
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Chakula cha Kutusaidia Sisi Tukumbuke
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Mwadhimisho Unaokuhusu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Mlo wa Mwisho wa Jioni wa Yesu
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
Pata Habari Zaidi
Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
my hadithi 99
Chakula cha Bwana cha jioni pamoja na mitume wake waaminifu

HADITHI YA 99

Katika Chumba cha Juu

SASA ni usiku wa Alhamisi, zimepita siku mbili. Yesu na mitume wake 12 wamekuja kwenye chumba kikubwa hiki cha juu ili wale chakula cha Kupitwa. Yule mwanamume unayeona akiondoka ni Yuda Iskariote. Anakwenda kuwaambia makuhani namna ya kumkamata Yesu.

Jana, Yuda aliwaendea akawauliza: ‘Mtanipa nini nikiwasaidia kumkamata Yesu?’ Wakasema: ‘Vipande 30 vya fedha.’ Basi Yuda sasa anakutana na watu hao ili awaongoze kwa Yesu. Je! si jambo baya hilo?

Chakula cha Kupitwa ndiyo sasa chamalizika. Lakini Yesu anaanza chakula kingine cha pekee. Anawapa mitume wake mkate na kusema: ‘Uleni, kwa sababu unamaanisha mwili wangu utakaotolewa kwa ajili yenu.’ Kisha anawapa kikombe cha divai na kusema: ‘Nyweni, kwa sababu kinamaanisha damu yangu, itakayomwagwa kwa ajili yenu.’ Biblia yakiita ‘chakula cha Bwana cha jioni.’

Waisraeli walikula chakula cha Kupitwa kiwakumbushe wakati malaika wa Mungu ‘alipozipita’ nyumba zao huko Misri. Lakini sasa Yesu anataka wafuasi wake wamkumbuke, na namna alivyowatolea uhai wake.

Baada ya kula Chakula cha Bwana cha Jioni, Yesu anawaambia mitume wake wawe hodari na kuwa na imani yenye nguvu. Mwishowe, wanamwimbia Mungu nyimbo kisha wanaondoka. Ebu tuone wanakokwenda.

Mathayo 26:14-30; Luka 22:1-39; Yohana sura za 13 mpaka 17; 1 Wakorintho 11:20.

Maswali ya Funzo

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki