Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lfb somo la 87 uku. 204-uku. 205 fu. 3
  • Mlo wa Mwisho wa Jioni wa Yesu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mlo wa Mwisho wa Jioni wa Yesu
  • Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Habari Zinazolingana
  • Kutii Maneno ya Yesu ya Kuaga
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Mlo wa Jioni wa Bwana
    Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
  • Katika Chumba cha Juu
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • ‘Fanyeni Hivi kwa Kunikumbuka Mimi’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
lfb somo la 87 uku. 204-uku. 205 fu. 3
Yesu akianzisha Mlo wa Jioni wa Bwana akiwa na mitume wake kumi na moja waaminifu

SOMO LA 87

Mlo wa Mwisho wa Yesu

Wayahudi walisherehekea Pasaka kila mwaka katika siku ya 14 ya mwezi wa Nisani. Hilo liliwakumbusha jinsi Yehova alivyowakomboa kutoka katika utumwa nchini Misri na kuwaleta kwenye Nchi ya Ahadi. Katika mwaka wa 33 W.K., Yesu na mitume wake walisherehekea Pasaka katika chumba cha juu jijini Yerusalemu. Mwishoni mwa mlo huo, Yesu alisema hivi: ‘Mmoja wenu atanisaliti.’ Mitume walishtuka na kumuuliza Yesu: ‘Ni nani huyo?’ Yesu alijibu: ‘Ni mtu ambaye nitampa mkate huu.’ Kisha, akampa mkate Yuda Iskariote. Mara moja, Yuda akaondoka katika chumba hicho.

Baada ya hapo, Yesu akasali, akaumega mkate vipande-vipande, na kuwagawia mitume waliokuwepo. Akasema hivi: ‘Kuleni mkate huu, unawakilisha mwili wangu, ambao nitautoa kwa ajili yenu.’ Halafu, akasali kwa ajili ya divai na kuwapa mitume wake. Akasema: ‘Kunyweni divai hii, inawakilisha damu yangu, ambayo nitaitoa ili msamehewe dhambi zenu. Ninawaahidi kwamba mtakuwa wafalme pamoja nami mbinguni. Fanyeni hivi kila mwaka, ili kunikumbuka.’ Wafuasi wa Yesu hukutana jioni ya Nisani 14 kila mwaka. Mkutano huo unaitwa Mlo wa Jioni wa Bwana.

Baada ya mlo huo, mitume wakaanza kubishana kuhusu ni nani aliye mkuu kati yao. Lakini Yesu akawaambia: ‘Yule aliye mkuu kati yenu ni yule ambaye anajiona kuwa mdogo zaidi.

‘Ninyi ni rafiki zangu. Ninawaambia kila kitu ambacho Baba anataka niwaambie. Baada ya muda mfupi nitaenda kwa Baba yangu aliye mbinguni. Nitawaacha ninyi, na watu watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu mkiwa na upendo kati yenu wenyewe. Mnapaswa kupendana kama vile mimi nilivyowapenda.’

Mwishowe, Yesu alisali akimwomba Yehova awalinde wanafunzi wake wote. Alimwomba Yehova awasaidie wanafunzi wake wafanye kazi kwa amani. Alisali ili jina la Yehova litakaswe. Kisha, Yesu na mitume wake waliimba nyimbo za kumsifu Yehova na kuondoka. Wakati wa Yesu kukamatwa ulikuwa umekaribia.

“Msiogope, ninyi kundi dogo, kwa sababu Baba yenu amekubali kuwapa Ufalme.”​—Luka 12:32

Maswali: Yesu aliwaahidi nini mitume wake? Yesu aliwafundisha mitume somo gani muhimu katika mlo wake wa jioni wa mwisho?

Mathayo 26:20-30; Luka 22:14-26; Yohana 13:1, 2, 26, 30, 34, 35; 15:12-19; 17:3-26

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki