Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • hp sura 1 kur. 4-9
  • Je! Inawezekana Kweli Kuwa na Maisha ya furaha?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je! Inawezekana Kweli Kuwa na Maisha ya furaha?
  • Furaha​—Namna ya Kuipata
  • Habari Zinazolingana
  • Kupata Furaha ya Kweli kunategemea Wewe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1981
  • Je! Uhai Una Kusudi?
    Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai?
  • Uhai Wako—Kusudi Lao ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • “Kwa Jumla Ndiyo Impasayo Mtu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
Pata Habari Zaidi
Furaha​—Namna ya Kuipata
hp sura 1 kur. 4-9

Sura ya 1

Je! Inawezekana Kweli Kuwa na Maisha ya furaha?

“NI VIZURI kuwa hai!” Hivyo ndivyo mtu anavyojisikia anapokuwa na furaha. Lakini tukisema kweli, tunajua kwamba si nyakati zote maisha yanapokuwa mazuri. Kuna matatizo (magumu). Huenda yakawa mengi sana na mazito sana mpaka furaha y kweli ionekane kuwa ndoto tu. Je! ni lazima iwe hivyo?

2 Unajua kwamba maisha yenye furaha yanakuwa na mambo mengi ya kufurahisha. Ili tufurahie maisha tunahitaji chakula cha kututosha, na mavazi yanayofaa. Tunahitaji makao tunapoweza kupata ulinzi na pumziko. Lakini hayo ndiyo mambo yale ya kwanza tu. Urafiki wa watu wenye kupendeza na afya nzuri ni mambo ya maana pia.

3 Lakini hata wale walio na kadiri fulani ya mambo hayo huenda bado wakatamani sana furaha ya kweli. Mtu anaweza kuacha kutosheka (kuridhika) kwa sababu ya kazi anayofanya, au kwa sababu ya hali za kazi yake. Vilevile, katika jamaa nyingi kuna magombano kati ya mume na mke au kati ya wazazi na watoto. Wala tusisahau kwamba sisi sote tunaelekea sana kupatwa na ugonjwa au kifo cha ghafula. Je! wewe unaamini inawezekana kuyavumilia matatizo hayo na mengine kwa njia yenye kututosheleza kikweli? Kuna sababu ya kuamini hivyo. Lakini ili mtu yeyote apate maisha ya furaha anahitaji kwanza kupata jambo fulani wasilo nalo watu wengi, yaani, sababu ya kuwa hai.

4 Ni lazima uwe na kusudi la kuishi ndipo uweze kufurahi kweli kweli. Katika kitabu chake The Transparent Self, Profesa S. M. Jourard anaandika hivi:

“Mtu anaishi mradi maisha yake yanakuwa na kusudi na ubora na mradi yeye ana jambo la kuishilia . . . Mara tu kusudi, ubora na tumaini viondokapo maishani mwa mtu, yeye anaanza kukoma kuishi; anaanza kufa.”

Jambo hili sasa linakubaliwa kuwa kweli hata viwandani. Ripoti ya kutoka Kanada juu ya kukosa kwa wafanya kazi kufika kazini ilieleza hivi:

“Watu wanatafuta kusudi la kuwa hai, na sasa hawatosheki tena wanapotumiwa kuwa vidude tu vya kufanyizwa kazi kama vibaraka kwa faida ya wengine.”—Atlas World Press Review.

5 Hayo yanasaidia kueleza sababu ya matajiri wengi kukosa kutosheka. Ni kweli kabisa kwamba wanakula, wanalala, wana jamaa zao na wanapata raha fulani na starehe za maisha. Lakini wao huenda wakaona kwamba hata wanyama wengi wanafanya mambo ayo hayo. Wanaona maisha yanahitaji kuwa na mambo mengi zaidi ya hayo.

6 Wala kuishi maisha marefu hakumalizi tatizo lenyewe. Watu wengi walio wazee-wazee wanajua kwa mambo waliyoona kwamba kuishi maisha marefu bila kujisikia unatimiza jambo fulani au kujisikia unahitajiwa na watu kunachosha mtu. Je! wewe umeona hivyo?

7 Si wazee-wazee peke yao wanaokosa kuwa na sababu nzuri ya kuishi. Uchunguzi mmoja ulioongozwa na Chuo Kikuu cha Daito Bunka, Japan, ulionyesha kwamba kati ya wanafunzi 1,500 wa masomo ya juu, asilimia (%) 50 ya wasichana na asilimia 34 ya wavulana walikuwa wamekwisha kufikiria kujiua. Kwa nini? Sababu ya kwanza kati ya zile nyingi zilizotolewa ni kwamba ‘maisha hayakuwa na kusudi lo lote.’ Na je! unadhani mambo ni tofauti katika Ulaya, katika zile bara mbili za Amerika na katika Afrika? Ongezeko kubwa la watu wenye kujiua linaonyesha kwamba watu zaidi na zaidi hawana furaha, tena wamechoka na maisha.

8 Huenda sisi wenyewe tukawa hatujisikii kuwa wenye shida nyingi. Huenda tukaweza kuwa na furaha ya kadiri fulani tujapokuwa na matatizo. Hata hivyo, tunalazimika kujiuliza, Je! maisha yana kusudi la kweli? Nawezaje kuwa na furaha isiyokwisha?

9 Karne nyingi zilizopita mfalme mmoja alichunguza shughuli nyingi za maisha—kuwa na jamaa, kupata utajiri, kuwa na elimu bora, kufurahia chakula kizuri na kujenga majengo yenye kuvuta macho. Huenda vitu kama hivyo vikasikika kuwa vya kufurahika. Hata hivyo yeye aliona kwamba vinaweza pia kukoroga sana moyo wa mtu. Aliuliza hivi: “Mtu hupata nini kwa kazi yake yote, na kwa juhudi ya moyo wake alivyojitahidi chini ya jua? Kwa kuwa siku zake zote ni masikitiko, na kazi yake ni huzuni; naam, hata usiku moyoni mwake hamna raha. Hayo nayo ni ubatili.”a

10 Ubatili wavyo ulikaziwa baadaye alipoeleza mambo yanayongoja mtu baada ya kuishi miaka michache—macho yanashindwa kuona vizuri, mikono na miguu inakuwa dhaifu, meno yanakuwa yameoza au yaliyoacha mapengo, usingizi unakuwa wenye masumbuko na mwishowe anapatwa na kifo.b

11 Kwa hiyo, hata tukijisikia kwamba tunafurahia maisha kwa kadiri fulani, bado kuna maulizo magumu yanayotupata sote. Sana-sana sasa. Kwa sababu gani? Mhariri Vermont Royster alieleza kwamba kwa muda unaozidi kidogo miaka 50 wanadamu wamepanua sana maarifa yao na ujuzi wao wa kuunda vitu, lakini yeye anaongeza kusema hivi:

“Hili ni jambo la kushangaza. Tunapomfikiria mwanadamu mwenyewe, na mashaka yanayompata, hata cheo chake katika huu ulimwengu mkubwa, tunaona tumezidi kusonga mbali kuliko muda ule wakati ulipoanza. Tungali na maulizo ya kutaka kujua sisi ni akina nani na kwa sababu gani tunaishi hapa na ni wapi tunakoelekea.”—Science Digest.

12 Ni kweli kwamba mtu anaweza kujaribu kuyapuza maulizo hayo ‘afurahie maisha’ kama anavyotaka. Watu wanaweza kusema mengi wakitaka kupata furaha ya maisha hata kama yana matatizo. Lakini hakuna faida ya kuishi maisha ya kudhania-dhania tunafurahi, kumbe sivyo.c Maisha zetu zingepata kusudi halisi na msingi wa kuwa na furaha kama tungeweza kuanza kufahamu “sisi ni akina nani na kwa sababu gani tunaishi hapa na ni wapi tunakoelekea.” Je! tunaweza kufahamu?

13 Watu wenye kufikiri sana wamekata kauli mara nyingi kwamba majibu yanategemea lile ulizo la maana zaidi, ‘Je! Mungu yuko?’ Ikiwa kuna Mungu, ni wazi yeye angejua sisi tulitoka wapi, kwa sababu gani tunaishi hapa na ni wapi tunakoelekea. Angejua pia kwa nini kuna maovu, ajue kama yatakwisha. Na kama yatakwisha, ajue yatakwishaje. Tena angejua tunaweza kufanya nini ili maisha yetu yatufurahishe zaidi kisha yawe yenye kusudi zuri zaidi. Basi, ‘Je! Mungu yuko?’

[Maelezo ya Chini]

a Mhubiri 2:22, 23, katika Biblia.

b Mhubiri 12:1-7.

c Linganisha Mhubiri 7:2-6.

[Jambo la Kuzungumzwa]

Ni jambo gani linalohitajiwa ili mtu afurahie maisha? (1-10)

Ni maulizo gani ya maisha tunayopata, na kuamini Mungu kunahusikaje? (11-13)

[Sanduku katika ukurasa wa 7]

‘JE! KUNA FAIDA YA KUISHI?’

Michele, mwanamke Mfaransa, anasimulia kwamba yeye alitoroka nyumbani na mtaani “ili kuukimbia ulimwengu wa wanafiki na kuepuka kukatishwa tumaini na wale walio karibu nami.” Halafu—

“Nikaanza uasherati, nikatumia dawa za kulevya na kushirikiana na watu hatari. Polisi na wapelelezi wenye kusaka wahalifu katika mataifa yote walinitafuta. Nikawa karibu kutumiwa na weupe kama mtumwa wao. Nilihama-hama huku na huku nikitafuta kusudi linalotufanya tuishi, nikahudhuria madhehebu mbalimbali za kidini. Lakini bado maisha yakawa hayana faida. Nikajiona sifai kitu kisha nikawa nikifikiria kufa tu.”

[Sanduku katika ukurasa wa 9]

MWANAMUME MWENYE MAHANGAIKO

Mwanamume mmoja katika Japan jina lake Yamamoto anasimulia hivi:

“Nilipokuwa nikijitayarishia mitihani ya kuingia chuo kikuu miaka kadha iliyopita, muda mwingi nilikuwa nikijaribu kufikiria nina kusudi gani la kuishi. Nilivyozidi kuchunguza vitabu vya filosofia, ndivyo nilivyozidi kukatishwa tumaini. Baada ya kupita mtihani wangu nikajiunga na chama cha kisiasa. Lakini kwa sababu ya kuona mabaya mengi yakitendeka kila mahali, lile ulizo lilinirudia tena, ‘Kusudi la kuishi ni nini?’”

Yeye hakupata majibu yenye kumtosheleza katika falsafa (filosofia) za wanadamu, ambao ni wazi wameshindwa kutatua matatizo ya wanadamu. Wala kuchunguza kwake historia wala mambo aliyoona kwenye siasa hayakumsadikisha kwamba serikali yo yote ya kibinadamu inaweza kuyatatua matatizo yaliyopo. Aliona wanadamu wametumia namna zote za serikali, na bado lile ulizo la kusudi la kuishi halikujibiwa. Mjapani huyo anaongeza kusema hivi:

“Nilianza kuishi kwa kujitafutia anasa, sababu moja ikiwa ni kwamba nilikata tumaini. Lakini muda si muda nikaona nilikuwa nimefanya upumbavu. Mwishowe nikakata kauli kwamba ulizo langu lililonihangaisha kwa muda mrefu juu ya sababu au kusudi la kuishi lilitegemea kama Mungu yuko au hayuko.”

[Picha katika ukurasa wa 4]

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki