Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • kc sura 15 kur. 141-150
  • Watetezi Washikamanifu wa Ufalme

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watetezi Washikamanifu wa Ufalme
  • “Ufalme Wako Uje”
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUTETEA NENO LA MUNGU
  • “BABULONI MKUU” WAANGUKA!
  • USHUHUDA WA DUNIANI POTE WAANZISHWA
  • “MTUMWA” MWAMINIFU
  • Ufalme wa Mungu Watawala
    Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
  • “Roho ya Uhai Itokayo kwa Mungu Ikawaingia”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1980
  • Ufalme wa Mungu Ni Bora Katika Njia Zote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Uharibifu wa Ulimwengu Uliotabiriwa Utakuja Lini?
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
Pata Habari Zaidi
“Ufalme Wako Uje”
kc sura 15 kur. 141-150

Sura ya 15

Watetezi Washikamanifu wa Ufalme

1. Ni matukio gani makubwa ambayo Danieli alitabiri?

AMANI mapema, unabii wa Danieli ulikuwa umeonyesha mwaka wa 29 W.K. kuwa ndio mwaka barabara wa kutokea kwa Masihi akiwa mwanadamu, na vilevile mwaka wa 1914 W.K. kuwa ndio mwaka wa kutawazwa kwake katika utukufu wa kimbingu. Tena, Danieli alitabiri kirefu jinsi ule ubishani mkubwa juu ya utawala wa ulimwengu utakavyomalizwa.

2. Ni suala gani ambalo ni lazima liamuliwe sasa, na katika mahaka-ma gani?

2 Sasa lile suala kuu la utawala halali wa dunia lazima likatiwe maneno kabisa. Lakini katika mahakama ipi? Katika mahakama kuu zaidi sana ya ulimwengu mzima wote! Danieli anaisimulia kwa maneno haya:

“Nikaendelea kutazama mpaka kukawa na viti vya enzi vilivyowekwa, na yule Mzee wa Siku akaketi. Vazi lake lilikuwa jeupe pe kama theluji, na nywele za kichwa chake zilikuwa kama sufu safi. Kiti cha enzi chake kilikuwa miali ya moto; magurudumu yake yalikuwa moto unaowaka. Kulikuwa na kijito cha moto kikitiririka na kutoka mbele zake. Kulikuwako maeIfu elfu walioendelea kumhudumia, na elfu kumi mara elfu kumi walioendelea kusimama pale pale mbele zake. Ile Mahakama ikafanya kikao, na kulikuwako vitabu vilivyofunguliwa.”—Danieli 7:9, 10, “NW.”

3. (a) Nani ndiye Hakimu? (b) Vile “vitabu” vinaonyesha nini? (c) Ni hukumu gani inayotolewa?

3 Kwa njia hiyo yule “Mfalme wa umilele,” Yehova Mungu, anachukua kikao cha kuhukumu. (Ufunuo 15:3, NW) Lakini vile ni “vitabu” gani ambavyo sasa viko wazi mbele zake? Ni maandishi yenye matendo ya kuhuzunisha sana ya utawala, ambayo mataifa yamefanya katika historia yote. Yale Majira ya Mataifa yanapomalizika mwaka wa 1914 W.K., kwa kufaa “ile Mahakama” inaondoa mamlaka ya “tawala zao,” ingawa kuna “Kurefushwa kwa maisha ambako walipewa kwa wakati fulani na majira fulani”—mpaka hukumu itekelezwe hakika juu yao penye Har-Magedoni.—Da-nieli 7:12, NW; Ufunuo 16:14, 16.

4, 5. (a) Nani anapewa utawala? (b) Ni kwa njia gani pekee tunaweza kufahamu kuwapo kwa Mfalme?

4 Basi, nani atapewa utawala? Danieli anaendelea kusema:

““Nikaendelea kutazama katika njozi za usiku, na, ona kule! pamoja na mawingu ya zile mbingu mtu fulani mfano wa mwa-na wa mtu akawa anakuja; na kwa yule Mzee wa Siku akapata ruhusa ya kukaribia, na wakamleta karibu sana hata mbele za Huyo. Na kwake kulipewa utawala na adhama na ufalme, iii jamii za watu, vikundi vya mataifa na lugha zote zimtumikie hata yeye. Utawala wake ni utawala unaodumu kwa wakati usiojulikana ambao hautatoweka, na ufalme wake ni ule ambao hautaharibiwa.”—Danieli 7:13, 14, “NW.”

5 Ni nani huyo “mtu fulani mfano wa mwana wa mtu”? Ni Bwana Yesu Kristo aliyetukuzwa. Kwa ku-wa “mawingu ya zile mbingu” yanafananisha kuto-kuonekana, tunaiona kwa jicho la imani lenye ufaha-mu ile “ishara” iliyoonekana katika mambo yaliyotukia duniani wakati wa “mwanzo wa maumivu makali ya taabu” katika mwaka wa 1914 W.K.—Mathayo 24:3, 7, 8, 30, NW; Ufunuo 1:7.

6. (a) Hukumu inatolewa kwa habari ya nani mwingine? (b) Hao wa-napokea nini, na jinst gani?

6 Kutokana na unabii wa Danieli tunaona kwamba hukumu inafuata kutolewa “kwa kupendelea wale watakatifu wa yule Mkuu Zaidi,” na kwamba hao, pia, wanaupokea “ule ufalme na ule utawala na ile fahari ya zile falme chini ya mbingu zote.” (Danieli 7:22, 27, NW) “Watakatifu hao ni nani? Ni wazi kwa-mba wao ni tofauti na watawala wapotovu, wenye kutaka faida yao katika serikali ya kibinadamu, ambao kwa muda mrefu sana wamegandamiza watu. Ni wale “watakatifu” 144,000 waliopakwa mafuta, nao ni wa-nadamu ambao “hawana mawaa” katika ukamilifu wao na ambao “wamenunuliwa katika wanadamu” wawe watawala wenzi wa “wana wa mtu” katika ufalme wake wa kimbingu. Wanafufuliwa “siku ya mwisho” wawe pamoja naye. (Ufunuo 14:3-5; Matha-yo 24:30, NW; Yohana 6:40) Wakati wa kuja kwa Yesu katika ufalme wake, mabaki ya “watakatifu” hao wanapatikana wakiwa hai kabisa duniani. Nao wana kazi ya kufanya!

KUTETEA NENO LA MUNGU

7, 8. (a) Ni kikundi gani kilichoanza kazi ya kutayarisha, na wakati gani? (b) Walitupa nini kando? (c) Walitetea nini kwa uthabiti? (d) Walielekeza kwenye tarehe gani? (e) Wametumia chombo gani kutangaza ufalme wa Mungu?

7 Ulipokaribia wakati wa “Mwana wa mtu” kupokea ufalme wake, ni wazi yalikuwa mapenzi ya Mungu kazi ya kutayarisha ifanywe hapa duniani. Katika mwaka wa 1870 na kitu, Charles T. Russell alianzisha katika Pittsburgh, Pennsylvania, U.S.A., kikundi cha Wakristo waliojiweka wakf. Upesi hao wakafahamu kwamba dini za Jumuiya ya Wakristo zilitegemea imani na sherehe za Kibabuloni pamoja na fundisho la kutokufa kwa nafsi la Plato, wala hazikutegemea Neno la Mungu. Kwa kutupa kando dini ya uongo, kikundi hicho kikawa watetezi imara wa mafundisho ya Biblia juu ya ukombozi wa Yesu. Kilitetea ufufuo pia na kuonyesha kwamba ufalme wa Mungu ndilo tu-maini la wanadamu wanaoteseka.

8 Kupitia gazeti Mnara wa Mlinzi, ambayo limeku-wa likichapwa daima tangu Julai 1879, Russell na wenzi wake walitetea waziwazi lile fundisho la Biblia juu ya uumbaji wakipinga kisio la mageuzi la Darwin. Wakazima moto wa mateso kwa kuonyesha kutoka Biblia kwamba hakujapata kuwa na mahali penye moto wa kutesea “roho [au nafsi] za wafu.” Walielekeza kwenye mwaka wa 1914 W.K. kuwa tarehe iliyotiwa alama kuhusiana na kule ‘kuja’ kwa ufalme wa Mungu. Mpaka leo hii, Mnara wa Mlinzi Unaota-ngaza Ufalme wa Yehova, gazeti linalochapwa katika lugha mbalimbali zaidi ya 100, na kwa mamilioni ya nakala kila toleo, unatetea kishikamanifu ufalme wa Mungu kupitia Kristo kuwa ndio tumaini pekee la mataifa ya wanadamu.—Mathayo 12:21; Zaburi 145: 10-12.

9. Ufunuo 11:7-12 ulitimizwaje juu ya “mashahidi” hao?

9 Baada ya kutumikia kwa uaminifu muda wa miaka zaidi ya 30 akiwa msimamizi wa kwanza wa Sosaiti, C. T. Russell akafa Oktoba 31, 1916, akafuatwa na J. F. Rutherford. Viongozi wa kidini walikuwa wakitumia hali ile ya vita ili wachochee upinzani juu ya ujumbe wa Ufalme. Mikutano ya Kikristo ilivunjwa. Katika nchi kadha, watumishi waaminifu wa Mungu walitiwa gerezani. Rutherford na wahudumu wengine saba wenye madaraka kutoka makao makuu ya Sosaiti katika Brooklyn, New York, U.S.A., walihukumiwa kifungo cha miaka mingi. Walakini, watumishi hao wa Mungu hawakuvunjika moyo, maana unabii wa Biblia ulikuwa umetabiri mateso hayo. Kwa mfano, Ufunuo 11:7-12 unasimulia mataifa ya kilimwengu kuwa yakiongozwa na yule “mnyama” wa mfano, wafanye vita juu ya “mashahidi” wa Mungu, ‵wakiwashinda na kuwaua.’ Kutabiri kwao kungezuiwa, na kwa jinsi ya mfano wangekuwa kama mizoga yenye kuachwa wazi muda mrefu iwe harufu mbaya sana katika “njia” pana ya Jumuiya ya Wakristo. Yote hayo yalitukia wakati watumishi wa Mungu ulimwenguni pote wall-pokamatwa iii wadhihakiwe na watu. Walakini, wazi-mu wa vita ulipotulia, na wale waliokuwa gerezani walipofunguliwa—wakaondolewa kabisa mashtaka ya uongo waliyoshtakiwa—“roho ya uhai itokayo kwa Mungu ikawaingia.” Waliinuliwa kwenye cheo cha upendeleo wa kimungu, na tangu mwaka wa 1919 wakaanza kipindi cha utendaji wenye bidii wa Ufalme.—Isaya 52:7, 8; Warumi 10:15.

“BABULONI MKUU” WAANGUKA!

10. Dini za Jumuiya ya Wakristo zilijiletea hatia gani, na jinsi gani?

10 Wakati wa miaka hiyo ya vita, viongozi hao wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo hawakuongoza tu katika kutesa Wakristo wa kweli, bali pia waliukataa ule ushuhuda wa kwamba ufalme wa Mungu ulikuwa karibu. Walikuwa na ‵ufalme’ wao wenyewe, ule wa “Babuloni mkuu.” (Ufunuo 17:5, 6, 18, HNWW) Katika pande zote za vita, waliwahubiri vijana waingie katika mahandaki ya vita na wakaunga mkono kwa moyo wote machinjo hayo mabaya sana. Kwa hatua kama hiyo, viongozi wa Jumuiya ya Wakristo lazima bado wawe na hatia nzito ya damu, kama vile wale viongozi wa kidini wa Yerusalemu wa kale, ambao nabii wa Yehova aliambia hivi: “Katika marinda yako yameonekana damu ya nafusi zao hao masikini wasio [na hatia].”—Jeremiah 2:34, The Old Testament in Swahili (Mombasa, chapa ya mwaka wa 1949); 19:3, 4; ona pia Mathayo 23:34, 35.

11. Maneno ya Ezekieli 22:3, 4, 16 yanahusuje Jurnuiya ya Wakristo?

11 Sasa hiyo hatia ya damu iliongezwa kwenye ibada ya sanamu ya Jumuiya ya Wakristo na mafundisho yake ya imani za Kibabuloni. Kwa sababu hiyo, maneno ya Ezekieli, yule nabii, yakahusu pia Jumuiya ya Wakristo yenye ukafiri:

“Yeye Bwana Mngu asema: Mji umwayao damu ndani yakwe, illi kwamba wakati wakwe upate kuja, ufanyao sanamu kinyume cha nafusi yakwe illi kujitia najisi! Wewe umekuwa na uaili katika hiyo damu yako uliyoimwaya, nawe umekuwa na najisi katika hao sanamu wako uliowafanya; nawe umezileta siku zako karibu, na kufikilia karibu ya myaka yako: basi kwa ajili ya hayo mimi nimekufanya utukanwe ni hizo taifa, na kufanyiwa dhihaka ni hizo nti zote. Nawe utatiwa najisi ndani ya nafusi yako, mbele ya mato ya hizo taifa, nawe utajua kuwa mimi ndimi Jehova.”—Ezekieli 22:3, 4, 16, “OTSW” (Mombasa, chapa ya mwaka wa 1949)

12. (a) Ni matukio gani ya maana sana yaliyotukia mwaka wa 1919? (b) Hiyo ilifaidije watu wa Mungu duniani?

12 Dini yenye hatia ya Jumuiya ya Wakristo ilitupiliwa mbali na Mungu mwenyewe, Yehova, ambaye inadai kuabudu, lakini ambaye jina lake haipendi tena kulitumia. Katika mwaka ule wa 1919 W.K., ilipata anguko kuu pamoja na dini yote ya Kibabuloni ulimwenguni pote. Haingeweza tena kuwa na msimamo wo wote mbele za yule Aliye Juu Zaidi Sana. Haingeweza tena kutawala waabudu wa kweli wa Yehova. Wala sehemu nyingine yo yote ya Babuloni Mkuu, ile milki ya ulimwengu ya dini ya uongo, haingeweza kufanya hivyo. Maana sasa “Jehova Mwenyiezi” alivumisha wito huu kwa wale “watakatifu” walio waaminifu duniani:

“Mimi ni Jehova Mwenyiezi Mngu wako, nikufunzae illi upate faida, nikuongozae katika ndia hiyo ikupasayo kuiendea. Haya, tokani Babulon, . . . hubirini kwa sauti ya kuimba, tangazani habari hii.” (Isaiah 48:16, 17, 20, “OTSW” (Mombasa, chapa ya mwaka wa 1949)

Hii “sauti ya kuimba” ni sauti gani, nayo imesikiwa wapi?

USHUHUDA WA DUNIANI POTE WAANZISHWA

13. (a) Ni sehemu gani ya ile “sauti ya kuimba” ambayo sasa ikawa kubwa? (b) Ni wito gani kama wa sauti ya parapanda uliotolewa?

13 Yule “Mwana wa mtu” alieleza sehemu kubwa ya hiyo “sauti ya kuimba” katika unabii wake juu ya “umalizio wa mfumo wa mambo,” akisema:

“Na habari njema hizi za ufalme zitahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda kwa mataifa yote; na ndipo ule mwisho utakapokuja.” (Mathayo 24:3, 14, 37, “NW”)

Lakini wale “watakatifu” walihitaji kupangwa kitengenezo iii kazi hiyo ifanywe. Wala hawangeweza kuitimiza kwa nguvu za kibinadamu tu. Kwa matokeo mazuri, kwenye makusanyiko ya mataifa yote yaliyo-pangwa katika Cedar Point, Ohio, U.S.A., katika mwaka wa 1919, na tena katika mwaka wa 1922, roho ya Yehova ilimiminwa juu yao kwa njia ya ajabu. Iliwapanga kuwa tengenezo na kuwatia nishati ‘wamtangaze, wamtangaze, wamtangaze Mfalme na ufalme wake.’ (Mathayo 24:31) Kazi kubwa ilikuwa mbele ya “wateule” hao wenye kushikilia sana tumaini la ki-mbingu.

14. Sasa unabii wa Yoeli ulipataje utimizo mkubwa?

14 Kama vile unabii wa Yoeli ulivyokuwa umetimi-zwa katika Pentekoste wa mwaka wa 33 W.K. wakati wa zile “siku za mwisho” za ule mfumo wa mambo wa Kiyahudi, sasa unabii huo ulianza kupata utimizo mkubwa wakati wa “siku za mwisho” za mfumo wa ulimwengu wa Shetani. Wakitiwa nuru na kuchoche-wa na roho ya Mungu, ‘wana na mabinti’ wa kisasa waliopakwa mafuta wa Yehova ‘walitabiri hakika,’ walipojibidiisha katika kuuonya ulimwengu wa wanadamu juu ya kukaribia kwa “ile siku ya Yehova iliyo kuu na iliyo maarufu sana,” na juu ya uhitaji wa haraka wa ‘kuita juu ya jina la Yehova’ ili kuokolewa.—Matendo 2:16-21; Yoeli 2:28-32, NW.

“MTUMWA” MWAMINIFU

15. (a) Ni nani ambaye ndlye yule “mtumwa mwaminifu mwenye akili”? (b) Jamii hiyo imetambulishwaje tena nyakati za kisasa?

15 Katika unabii wake mkubwa juu ya ile “ishara,” Yesu alikuwa ameuliza ulizo hili:

“Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, amba-ye bwana wake alimweka juu ya nyumba yake, awape watu chakula kwa wakati wake?”

Jamii ya “mtumwa” mwaminifu ilikuwa imetumikia kati ya wale Wakristo wa kwanza mpaka ule ukafiri mkubwa ulipoingia. Je! tena tunaona tengenezo kama hilo lililo kama “mtumwa” likigawa chakula cha kiroho wakati Bwana Yesu anapoingia katika ufalme wake? Ndiyo! Wale “Wanafunzi wa Biblia,” kama walivyokuwa wakiitwa wakati huo, walikuwa wamefanya kazi ya duniani pote ya kutayarisha. Na Yesu alisema:

“[Mwenye furaha ni] mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo. Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote.”—Mathayo 24:45-47.

16. (a) “Mtumwa” huyo ameangaliaje “vitu” vya Bwana? (b) Ni jina gani la Kimaandiko ambalo “mtumwa” huyo amekubali kwa shangwe?

16 Ikithamini kuwekwa hivyo na yule Bwana, ile jamii ya “mtumwa” imetunza vizuri faida za Ufalme duniani, ikisimamia kutangazwa kwa “habari njema.” Wakati wa mwaka wa 1920 na kitu, habari za hukumu zenye nguvu zilitangazwa juu ya Shetani na tengenezo lake, na hasa juu ya dini ya Kibabuloni. Katika mwaka wa 1931, jamii ya “mtumwa” ilikubali kwa shangwe jina ambalo liliitofautisha waziwazi na dini yote ya uongo, yaani, jina “Mashahidi wa Yehova”—pamoja na lile daraka na pendeleo lililoonyeshwa na nabii Isaya kwa maneno haya:

“Nyinywi mu mashahidi yangu anena Jehova, na mtumishi wangu ambae nimemtagua: . . . Mimi, naam, mimi ni Jehova; tena zaidi ya mimi hapana mwokozi. . . . Nyinywi mmekuwa mashahidi yangu, anena Jehova, nami ni Mwenyiezi Mugu.” —Isaiah 43:10-12, “OTSW” (Mombasa, chapa ya mwaka wa 1949)

17. Sasa ni ulizo gani lililotaka kujibiwa?

17 “Mtumwa” huyo, ambaye washiriki wake walio-pakwa mafuta wamebaki wakiwa makumi to ya mae-lfu, angewezaje sasa ‘kuhubirisha habari njema hizi za ufalme katika dunia yote inayokaliwa na watu kwa ushuhuda’? Upesi Yehova alitazamiwa kutoa jibu.

[Picha katika ukurasa wa 148, 149]

KILE KICHWA CHA UFALME CHA BIBLIA

AHADI YA KIEDENI YA “UZAO” WA UFALME

“UZAO” WA KIFALME WATABIRIWA KUPITIA ABRAHAMU, DAUDI

KUHUBIRI UFALME​—DHABIHU YA UKOMBOZI YA MFALME

UFALME WASIMAMISHWA​—“SIKU ZA MWISHO” TANGU 1914

UFALME ‘WAJA’ KUHARIBU UTAWALA WA WANADAMU

UFALME WA MIAKA 1,000 WARUDISHA PARADISO

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki