Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • kc sura 14 kur. 127-140
  • Mfalme Atawala!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mfalme Atawala!
  • “Ufalme Wako Uje”
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KUFASIRI NDOTO
  • “NYAKATI ZILIZOWEKWA ZA MATAIFA”
  • “YERUSALEMU” MAANA YAKE NINI?
  • “UTAKANYAGWA” KWA MUDA GANI?
  • UTIMIZO ULIO MKUBWA
  • ZILE “NYAKATI SABA”—ZINA UREFU GANI?
  • ILE MILEANI (MIAKA ELFU)—LINI?
  • “KIZAZI HIKI”—KIPI?
  • 1914 ni Mwaka Uliotiwa Alama—Kwa Sababu Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1984
  • Ndoto Inafunua Kwamba Wakati Umesonga Sana
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • 1914—Mwaka Muhimu Katika Unabii wa Biblia
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Mfuatano wa Matukio Katika Biblia Unaonyesha Nini Kuhusu Mwaka wa 1914?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
“Ufalme Wako Uje”
kc sura 14 kur. 127-140

Sura ya 14

Mfalme Atawala!

1, 2. (a) Mwaka wa 1914 ulikuwa wenye maana gani iliyo kubwa zaidi? (b) Gazeti Watch Tower lilikaziaje mwaka wa 1914 miaka mingi mapema?

BILA shaka, ule mwaka wa 1914 ulionyesha badiliko kubwa katika mambo ya mataifa na ya wanadamu. Lakini ulikuwa wenye maana sana kuliko wanahistoria wengi wanavyojua. Ndio wakati matukio yenye kusisimua yanayohusiana na ‘kuja’ kwa ufalme wa Mungu yalipotukia. Miaka iliyotangulia, wanafunzi waaminifu wa Biblia walikuwa wakitazamia mwaka huo kwa taraja kubwa. Kwa msingi gani?

2 Miaka 34 kabla ya mwaka wa 1914, gazeti Zion’s Watch Tower and Herald of Christ’s Presence, katika matoleo yalo ya Desemba 1879 na Machi 1880, lilikuwa likielekeza kwenye mwaka wa 1914 kuwa tarehe iliyotiwa alama katika unabii wa Biblia. Makala katika toleo lake la Juni 1880 ilivuta fikira juu ya kukaribia kwa mwisho wa “majira ya Mataifa (Luka 21:24).” Ingawa wakati huo mwandikaji hakufahamu maana kamili ya matukio yaliyokuwa yakikaribia, alitumia orodha ya tarehe ya Biblia kuonyesha kwamba kipindi cha “nyakati saba,” au miaka 2,520, ya utawala wa serikali ya mataifa yasiyomwabudu Mungu, kuanzia ule uharibifu wa kwanza wa Yerusalemu wa kale, kilikuwa kinakaribia kukoma katika “A. D. 1914.” Alieleza hivi: “Kile kipindi kirefu cha miaka 2520 na matukio machungu [yaliyowapata watu wa Mungu] chini ya utawala wa wale wanyama, (serikali za kibi nadamu, Dan. 7) kinafananishwa waziwazi katika Dan. 4 na zile ‘nyakati saba’ za Nebukadreza na matukio machungu yaliyompata kati ya wanyama.” Basi, zile “nyakati saba” ni nini?

KUFASIRI NDOTO

3. Ni kweli gani ya msingi inayotajwa katika Danieli 4:25?

3 Sura ya 4 ya kitabu cha Biblia cha Danieli inasimulia ndoto ya unabii yenye maana kubwa. Inaonyesha kwamba “Aliye juu anatawala katika ufalme wa watu, naye anamupa yeye anayemutaka.” (Danieli 4:25, ZSB) Nebukadreza, mfalme wa Babuloni, alikuwa ameota ndoto na akamsimulia nabii Danieli ili apate fasiri.

4-6. (a) Nebukadreza aliota ndoto gani? (b) Danieli abifasirije? (c) Ilitimizwaje? (d) Aliporudishwa, Nebukadreza alikiri nini?

4 Nebukadreza aliona katika njozi mti mkubwa sana uliokuwa ukionekana mpaka kwenye mwisho wa dunia. Mti huo ulitolea wote chakula na makao. Lakini “mtakatifu” kutoka mbinguni akaamuru mti huo ukatwe na kuangushwa chini na kisiki chake kifungwe kwa pingu za chuma na za shaba, madini zilizokuwa zenye nguvu zaidi sana wakati huo. “Nyakati saba” zilitakiwa zipite huku mti huo ukiwa katika hali ya kuzuiwa usikue.

5 Akifasiri njozi hiyo ya unabii, Danieli akaeleza kwamba ule mti ukiwa katika fahari yake ulifananisha Nebukadreza. Alipaswa ‘akatwe mpaka chini’ au ashushwe. “Nyakati saba” zingepita na Nebukadreza angekuwa kama wale wanyama wa pori. Lakini kama vile ule “mti” haukuharibiwa kabisa, hivyo baada ya zile “nyakati saba” mfalme huyo angerudishwa. —Danieli 4:19-27.

6 Hayo ndiyo hasa yaliyompata Nebukadreza. Alishushwa, akawa kama mnyama aliyeondolewa katika kao la wanadamu, akila majani. “Nyakati saba” hizo kwa wazi zilikuwa miaka saba, ambayo Nebukadreza ‘alipatwa na matukio machungu kati ya wanyama.’ Nywele zake mwenyewe zikawa ndefu kama vile manyoya ya tai, na kucha zake zikawa kubwa kama kucha za ndege. Lakini mwishowe akarudiwa na akili, akarudishwa kwenye uufalme wake. Hilo lilipotokea, akamsifu na kumtukuza “Mfalme wa mbinguni” kuwa ndiye Yule anayetawala kweli kweli na ambaye “ufalme wake hudumu toka kizazi hata kizazi.” —Danieli 4:28-37.

7-9. (a) Ni katika unabii upi Yesu alitaja mwisho wa Majira ya Mataifa? (b) Kwa hiyo ni maulizo gani yamepasa kutupendeza?

7 Walakini, yote hayo yanahusianaje na ule mwaka wa 1914 wa Wakati wa Kawaida wetu?

“NYAKATI ZILIZOWEKWA ZA MATAIFA”

8 Ni wakati alipokuwa akisimulia habari ya ‘ile ishara ya umalizio wa mfumo wa mambo’ Yesu Kristo aliposema:

“Yerusalemu utakanyagwa na mataifa, mpaka nyakati zilizo-wekwa za mataifa zitimie.” (Luka 21:24, “NW”)

Yale “mataifa” yaliyotajwa na Yesu yalikuwa mataifa yasiyo ya Kiyahudi. Hapa Biblia Union Version ya Kiswahili inatumia usemi “majira ya Mataifa.” Hivyo, wengi wanauliza, ‘Majira ya mataifa ni nini? Ni kipindi gani cha wakati ambacho Yesu alikuwa akifikiria? Kilianza wakati gani, na kingemalizika lini?’

9 Tumekwisha kuona kwamba unabii mkubwa wa Yesu juu ya ile “ishara” una maana kubwa kwetu leo. Hivyo sisi pia tunahitaji kujua majibu ya maulizo hayo.

“YERUSALEMU” MAANA YAKE NINI?

10-12. (a) Kulingana na mwanachuo mmoja, yale matukio ya mwaka wa 29-70 W.K. yalikuwa mfano wa nini? (b) Lakini “Yerusalemu” ungeweza kuwa na maana gani kubwa zaidi katika Luka 21:24? (c) Kitabu cha saiklopedia chenye kujulikana sana kinatusaidiaje kwa maoni hayo? (d) Hivyo “Yerusalemu” unafananisha nini?

10 Katika kufasili unabii wa Yesu, Profesa A. T. Robertsona anaeleza kwamba Yesu alitumia “ule uharibifu wa hekalu la Yerusalemu, uliotukia katika kizazi hicho mwaka wa A.D. 70, kuwa mfano wa kuja kwake mara ya pili pia na wa mwisho wa ulimwengu au ukamilifu wa kizazi.” Kwa hiyo, tunaweza kuuliza: Zaidi ya mambo yaliyoupata Yerusalemu mwaka wa 70 W.K., ingeweza kuwa Yesu alikuwa akionyesha katika Luka 21:24 kwamba “Yerusalemu” una maana gani kubwa zaidi?

11 Yesu aliuona Yerusalemu kuwa mji mkuu wa Israeli mahali wafalme wapakwa-mafuta wa Yehova katika ukoo wa Daudi walikaa “juu ya kiti cha enzi cha Yehova,” wakitawala kwa ajili ya Yehova Mungu. Pia, hekalu la mji huo lilikuwa ndiyo makao makuu ya ibada ya kweli kwa dunia yote. (1 Mambo ya Nyakati 28:5; 29:23, NW; 2 Mambo ya Nyakati 9:8) Kitabu Cyclopaedia cha M’Clintock na Strong kinaeleza hivi: “Yerusalemu ulikuwa umefanywa kuwa makao ya kimilki ya mfalme wa Israeli yote; na Hekalu, ambalo mara nyingi liliitwa ‘ile nyumba ya Yehova,’ lilikuwa pia makao ya yule Mfalme wa wafalme, yeye aliye kichwa kikuu cha serikali ya kitheokrasi, . . . kwa kweli, Yerusalemu haukuwa wa maana kisiasa: haukuwa mji mkuu wa milki yenye nguvu yenye kuelekeza mambo ya serikali nyingine, bali ulikuwa mashuhuri kwa sababu ya mataraja yale mazuri yaliyotabiriwa na Daudi alipokuwa akitangaza anaamini kuja kwa Masihi (Zaburi 2:6; 110:2].”—Kitabu cha 4, ukurasa wa 838.

12 Uhakika wa kwamba wale wafalme katika ukoo wa Daudi walikaa juu ya “kile kiti cha enzi cha uufalme wa Yehova” ulikazia kweli ya kwamba hakika ufalme ulikuwa wa Mungu. Ule ufalme wa Israeli ambao makao yake yalikuwa katika Yerusalemu ulikuwa ufalme wa Mungu wa mfano. Hivyo “Yerusalemu” ulifananisha ufalme wa Mungu.

13, 14. ‘Mkanyago’ unaotajwa katika Luka 21:24 ulianza lini na jinsi gani?

13 Kumbuka, sasa, maneno ya Yesu: “Yerusalemu utakanyagwa na mataifa, mpaka nyakati zilizowekwa za mataifa zitimie.” (Luka 21:24, NW) ‘Mkanyago’ huo ulianza wakati gani? Ulianza zamani kabla ya kuzaliwa kwa Yesu huko Bethlehemu, maana wafalme wa kibinadamu katika ukoo wa Daudi walikuwa wamekoma kitambo kutawala katika Yerusalemu. Ile nasaba ya Daudi ya wafalme ilikoma wakati Mfalme Sedekia alipoondolewa katika kiti cha enzi na Wababuloni wavamizi wakiongozwa na Nebukadreza.

14 Historia sahihi ya Biblia inatuambia yaliyotukia kwa sababu ya ubaya wa watu na wa Mfalme Sedekia. Inasema: “Hasira kali ya Yehova ikaja juu ya watu wake, mpaka kukawa hakuna dawa. Hivyo akaleta juu yao mfalme wa Wakaldayo [Wababuloni], ambaye alianza kuua vijana wao wanaume kwa upanga . . . Kila kitu [Mungu] akakitia katika mkono [wa Nebukadreza]. Na vyombo vyote, vikubwa na vidogo, vya nyumba ya Mungu wa kweli na hazina za nyumba ya Yehova na hazina za mfalme na wana-wafalme wake, kila kitu akapeleka Babuloni. Naye akaanza kuiteketeza nyumba ya Mungu wa kweli na kuubomoa ukuta wa Yerusalemu.” (2 Mambo ya Nyakati 36:11, 12, 16-20, NW) Huko ndiko ule ‘mkanyago’ ulianzia.

“UTAKANYAGWA” KWA MUDA GANI?

15-17. (a) Nani alipoteza ile “haki ya ufalme wa Daudi, na jinsi gani? (b) Nani angeipata tena haki hiyo, na kwa muda gani? (c) Hivyo ni ulizo gani lenye kuhusika linalotokea? (d) Sababu gani ingemfaa Danieli ajibu ulizo hilo?

15 Nabii Ezekieli alitabiri kuondolewa kwa Sedekia katika kiti cha enzi, akiwa ndiye wa mwisho katika ukoo wa Daudi wa wafalme kutawala katika Yerusalemu wa kidunia. Alisema:

“Hivi ndivyo amesema Bwana Yehova Mwenye Enzi Kuu, ‘Kiondoe kilemba, na livue lile taji. Hiyo haitakuwa namna ile ile. . . . Uharibifu, uharibifu, uharibifu nitaufanya. Kwa habari ya hiyo pia, hakika haitakuwa ya mtu mpaka aje yeye aliye na ile haki halali, nami lazima nimpe yeye hiyo.’ ”—Ezekieli 21:26, 27, “NW.”

16 Ingawa wakati huo Mfalme Sedekia alipoteza ile “haki halali” ya ufalme wa Daudi, yule Masihi aliyeahidiwa angeirudisha “haki” hiyo, atawale katika ufalme wa Mungu “milele.” (Luka 1:32, 33) Lakini ingekuwa muda gani mpaka ufalme wa Kimasihi uanze kutawala—uliokuwa umefananishwa na ule ufalme wa kidunia wa Israeli wenye makao katika Yerusalemu?

17 Yehova Mungu alijua, naye angeweza kuonyesha kipindi cha wakati katika Neno lake, kama vile alivyokuwa ametabiri mambo mengine mengi ya wakati ujao. Katika hotuba yake juu ya “umalizio wa mfumo wa mambo,” mara kadha Yesu alielekeza kwenye unabii wa Danieli, ambamo Mungu alikuwa ametabiri kwa usahihi matukio mengi ambayo yangetukia mbinguni na duniani. (Linganisha Mathayo 24:3, 15, 21, 30 NW, pamoja na Danieli 9:27; 11:31; 12:1; 7:13.) Je! si unabii wa yale “majuma sabini,” katika Danieli 9:24-27, ulikuwa umetoa pia orodha sahihi ya wakati wa kuja kwa Masihi mara ya kwanza? Je! haingefaa nabii yule yule ndiye atoe orodha ya wakati wa kuja Masihi mara ya pili? Tunapata habari hiyo ya unabii inayotuhusu sisi moja kwa moja katika Danieli sura ya nne.

UTIMIZO ULIO MKUBWA

18. (a) Huenda ikawa ni sababu gani inayofanya historia za kilimwengu zisiutaje wazimu wa Nebukadreza? (b) Sababu gani imetupasa tutii yale ambayo Neno la Mungu linasema hapa?

18 Tumekwisha kuchunguza matumizi ya kwanza na yenye kifano ya unabii wa Danieli juu ya “nyakati saba” na tumeona kwamba yalihusu ile miaka halisi saba ya wazimu wa Nebukadreza. Uhakika wa kwamba historia ya ulimwengu haitoi habari nyingi juu ya kutokuwapo kwa Nebukadreza miaka saba katika kiti cha enzi haupasi kushangaza. Maandishi ya kale ya Wamisri, Waashuru na Wababuloni yanajulikana sana kuwa na mazoea ya kutotaja habari yo yote ambayo huenda ikawa inaaibisha mtawala. Hiyo ni sababu moja inayofanya yasiwe yenye kutegemeka kama Neno la Mungu lililoongozwa kwa roho yake. Ni Neno la Mungu linalotuhakikishia kwamba ile njozi ya ndoto ilitimizwa. Usemi wa unabii huo pia unaonyesha kwamba kungekuwako utimizo ulio mkubwa hata zaidi, na huo vilevile umetukia. Kwa njia gani?

19. Kwa sababu gani ingefaa kutazamia njozi hiyo itusaidie kuujua urefu wa yale Majira ya Mataifa?

19 Na ijulikane kwamba aliyepewa ndoto hiyo ni yule mfalme wa Babuloni, mtawala wa ulimwengu mwenyewe aliyetumiwa kupindua duniani ule ufalme wa Mungu wa mfano, na kwa njia hiyo akaanzisha milki ya ulimwengu yenye kusimamiwa na utawala wa Mataifa. Pia, ni wazi kwamba njozi hiyo ilitolewa si miaka mingi baada ya kutukia badiliko hilo kubwa sana—wakati ufalme wa mfano ulipokuwa umekoma ambao kupitia huo Yehova alitumia enzi kuu. Zaidi ya hayo, Danieli sura ya 4 inakazia mara nyingi kichwa cha habari ‘kwamba Aliye juu ndiye Mtawala katika ufalme wa wanadamu, naye humpa yeye amtakaye.’ (Danieli 4:17, 26, 34, 35) Kwa hiyo tuna sababu nzuri ya kutegemea njozi hiyo tupate habari juu ya muda wa utawala wa Mataifa juu ya dunia.

20. Tunauliza ulizo gani, na tunaweza kwenda wapi tupate jibu?

20 Tukihesabu tangu wakati ule ufalme wa mfano wa Mungu kupitia mfalme wa ukoo wa Daudi ulipopinduliwa, ingechukua muda gani mpaka Mungu aonyeshe tena enzi kuu yake kupitia ufalme unaohusiana na ukoo wa kifalme wa Daudi, Masihi akiwa ndiye mfalme anayetawala? Danieli sura ya 4 inatoa msingi wa kuamulia urefu wa yale Majira ya Mataifa au “nyakati zilizowekwa za mataifa,” muda ambao mataifa hayo yangekanyaga “Yerusalemu,” au ule ufalme wa Mungu.—Luka 21:24, NW.

21. Maandiko ya Danieli 4:15-17 na Ayubu 14:7 yanaonyesha nini kwa habari ya ile hali iliyofuata kuondolewa kwa Sedekia katika kiti cha enzi?

21 Mkanyago huo unaanza tangu mwaka ule ambao Nebukadreza aliondoa Mfalme Sedekia kutoka kiti cha enzi Yerusalemu. Tangu wakati huo enzi kuu ya Yehova kama ilivyotumiwa kwa kuwakilishwa katika ukoo wa wafalme wa Yuda ‘ilikatwa ikaangushwa chini.” Ilizuiwa, kama kile kisiki cha mti cha ndoto ya Nebukadreza, kilichofungwa kwa pingu. Mamlaka za Mataifa zilizo mfano wa wanyama zikatawala dunia yote. Lakini kulikuwa na tumaini kwa “mti” huo, la kwamba ‘ungechipuka tena.’ Na ndipo watu wanaoishi ‘wangejua ya kuwa Aliye juu ndiye anayemiliki katika ufalme wa wanadamu.’—Danieli 4:15-17; Ayubu 14:7; linganisha Isaya 11:1, 2; 53:2.

22. Ule “mti” wa Ufalme ulisitawi tena lini na kwa njia gani?

22 Katika ufalme huo uliorudishwa, Aliye Juu Zaidi anatawala kupitia Masihi wake. Haanzi kutawala wakati Masihi huyo alipoonekana mara ya kwanza duniani akiwa mwanadamu mkamilifu, alipodharauliwa na Wayahudi kisha wakamkataa asiwe mfalme. Lakini zile pingu juu ya kile kisiki cha mti zinafunguliwa, na ule “mti” wa Ufalme unasitawi tena. Hiyo ni wakati huyo “aliye mnyenyekevu zaidi sana kati ya wanadamu” anapofika katika utukufu wake akiwa Mfalme wa kimbingu wa watu wa mataifa yote. Ndipo, yale Majira ya Mataifa yanapokwisha, ule ufalme wa ulimwengu unakuwa “ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake.”—Ufunuo 11:15, UV; Danieli 4:17, 25, NW.

ZILE “NYAKATI SABA”—ZINA UREFU GANI?

23. Sababu gani ni lazima yale Majira ya Mataifa yaendelee mpaka wakati wetu?

23 Kwa wazi, basi, zile “nyakati saba” zinazohusu yale Majira ya Mataifa lazima ziwe muda mrefu zaidi ya miaka saba halisi. Kumbuka, Yesu alisema juu ya ‘kutimia’ au kwisha kwa hayo Majira ya Mataifa kuhusiana na “umalizio wa mfumo wa mambo.” (Luka 21:7, 24; Mathayo 24:3, NW) Kwa hiyo lazima ziendelee mpaka kufikia wakati wetu huu. Hasa zina urefu wa muda gani?

24. Tunaweza kufasirije urefu wa zile “nyakati saba”?

24 Tukigeukia sura ya 12 ya Ufunuo, tunaona kwamba mistari ya 6 na 14 inaonyesha kipindi cha siku 1,260 kuwa “wakati na nyakati na nusu ya wakati,” au 1 + 2 + 1/2. Jumla ni nyakati 31/2. Kwa hiyo, “wakati” mmoja ungekuwa siku 360, au miezi 12 kila mmoja ukiwa na wastani ya siku 30. “Nyakati saba” zingekuwa siku 2,520; na njia ya Biblia ya kiunabii ya “kila siku kuhesabiwa mwaka” inaonyesha kwamba hakika siku hizo zingejumlika ziwe kipindi cha miaka 2,520 ya kalenda. (Hesabu 14:34; Ezekieli 4:6) Kwa hiyo, huo ndio muda wa zile “nyakati saba”—yale Majira ya Mataifa.

25. Ile “miaka sabini” inayotajwa katika Yeremia 25:11 inahusika katika kuamua mwanzo wa yale Majira ya Mataifa?

25 Tunasaidiwa kuweka tarehe ya kalenda ya mwanzo wa yale Majira ya Mataifa kwa kuliendea Neno la Mungu. Kama tulivyokwisha kuona, Yehova aliruhusu Wababuloni washinde watu wake, waharibu Yerusalemu na hekalu lake, wamwondoe Sedekia kutoka “kile kiti cha enzi cha uufalme wa Yehova” na kuingiza Wayahudi katika uhamisho wa Babuloni. (1 Mambo ya Nyakati 28:5, NW) Matukio yaliyofuata “katika mwezi wa saba” yaliongoza wale Wayahudi wa chache waliokuwa wamebaki katika nchi hiyo waki mbilie Misri. Ndipo Yuda ikawa ukiwa kabisa. (2 Wafalme 25:1-26; Yeremia 39:1-10; 41:1-43:7) Yeremia, nabii wa Yehova, alikuwa ametabiri kwamba ukiwa huo ungeendelea kwa miaka 70. (Yeremia 25:8-11) Ndipo Yehova ‘angemwadhibu mfalme wa Babeli kwa sababu ya uovu wake’ na ‘kuwarudisha watu Wake mahali hapa,’ yaani, nchi ya kwao.—Yeremia 25:12; 29:10.

26. (a) Danieli alikuwa shahidi aliyejionea mambo gani, naye alifahamu nini? (b) Tunaweza kujuaje ule mwezi na mwaka ambao unabii wa Danieli wa kurudishwa ulitimizwa? (c) Kwa kusema wazi, hiyo ni tarehe gani?

26 Danieli mwenyewe aliishi katika uhamisho wa Babuloni muda wa miaka mingi. Usiku ule Babuloni ulipoangushwa na Wamedi na Waajemi, yeye alikuwa shahidi mwenye kuona kwa macho yake mwenyewe utimizo wa unabii wake, na wa matabiri mengine juu ya mji huo. (Danieli 5:17, 25-30; Isaya 45:1, 2) Wanahistoria wanakadiri kwamba Babuloni ulianguka mwanzoni mwa Oktoba wa mwaka wa 539 K.W.K. Upesi baada ya hapo, Danieli alifahamu kutokana na unabii wa Yeremia kwamba ule utumwa wa miaka 70 na ukiwa wa Yerusalemu ulikuwa ni kama umekwisha. (Danieli 9:2) Na alikuwa sahihi! Katika mwaka wa kwanza wa Koreshi yule Mwajemi, ambao wanahistoria wengi wanahesabu kuanzia masika ya mwaka wa 538 K.W.K., Koreshi alitoa amri yenye kuruhusu Wayahudi warudi kwenye nchi ya kwao wakaikae tena na kujenga upya hekalu la Yehova huko. (2 Mambo ya Nyakati 36:20-23; Ezra 1:1-5) Masimulizi ya kihistoria yaliyoongozwa na Mungu yanatuambia kwamba wale Wayahudi waliitikia vyepesi amri ya Koreshi, hivi kwamba “wakati mwezi wa saba ulipofika wana wa Israeli wakawa wamo katika miji yao.” (Ezra 3:1, NW) Kulingana na kalenda yetu, hiyo ingekuwa Oktoba mwaka wa 537 K.W.K., na tarehe hiyo ndiyo inayoonyesha kumalizika kwa ile miaka 70 ya ukiwa iliyotabiriwa.

27. (a) Basi, ni lazima ile miaka 70 iwe ilianza wakati gani, na kwa tukio gani? (b) “Nyakati saba” zilikuwa na urefu gani, na kwa hiyo ni lazima ziwe zilikwisha lini? (c) Ni unabii gani mwingine mkubwa ulioanza kutimizwa tarehe hiyo barabara? (d) Mnara wa Mlinzi umekuwa ukitetea habari gani kwa muda wa miaka zaidi ya 100?

27 Habari hiyo ya kihistoria ni ya maana kwetu katika kutusaidia tujue mwanzo wa zile “nyakati zilizowekwa za mataifa.” Kwa kuwa ile miaka 70 ya ukiwa wa Yuda na Yerusalemu ilimalizika mwaka wa 537 K.W.K., ilianza mwaka wa 607 K.W.K. Huo ungekuwa ndio mwaka ambao Sedekia alikoma kukaa juu ya kile “kiti cha enzi cha uufalme wa Yehova” katika Yerusalemu. Kwa hiyo ndio tarehe ya mwanzo pia wa yale Majira ya Mataifa. Kama tulivyokwisha kuona, tukihesabu tangu Oktoba mwaka wa 607 K.W.K., zile “nyakati saba” za miaka 2,520 zinatufikisha kwenye Oktoba mwaka wa 1914 W.K., wakati unabii mkubwa wa Yesu juu ya “umalizio wa mfumo wa mambo” ulianza kutimizwa. Habari yenye kutegemeka katika Neno la Mungu ndio msingi wa uamuzi huo, na gazeti Mnara wa Mlinzi limekuwa likiutetea kwa miaka zaidi ya 100 sasa.

28, 29. (a) Ni jambo gani juu ya maandishi ya kilimwengu linalopasa kutufanya tushukuru kwa vile mambo mengi yalihifadhiwa katika Neno la Mungu? (b) Kwa nini kuna sababu yenye nguvu ya kupendelea Oktoba mwaka wa 1914 kuliko tarehe nyingine kuhusu mwisho wa yale Majira ya Mataifa?

28 Kweli kweli, tunaweza kuwa wenye shukrani kwa vile Yehova alihifadhi katika Neno lake lililoongozwa kwa roho yake hali sahihi ya habari zinazohitaji kujulikana kuhusu Wayahudi, Wababuloni na Wamedi na Waajemi katika ale karne ya sita K.W.K. Kama sivyo, ingekuwa vigumu kuunganisha wakati barabara wa matukio yaliyotendeka nyuma huko, maana maandishi ya kilimwengu ya kipindi hicho si kamili.

29 Walakini, wakitegemea hasa maandishi hayo ya kilimwengu, watu fulani wanakadiri kwamba Yerusalemu uliharibiwa mwaka wa 587/6 K.W.K. na kwamba Wayahudi walikuja chini ya utawala wa Wababuloni katika mwaka ambao Nebukadreza alipanda kiti cha enzi. Na wanaukadiri mwaka huo kuwa mwaka wa 605 K.W.K.b Kwa njia hiyo wanashikilia mwaka wa 605 K.W.K. kuwa ndiyo tarehe ambayo unabii wa Yeremia 25:11 ulianza kutimizwa: “Nchi yote itakuwa ukiwa; nao watatumikia miongoni mwa wale Mataifa miaka sabini.” (Septuagint ya Kigiriki ya Bagster) Kama ingekuwa hivyo na yale Majira ya Mataifa yahesabiwe tangu wakati huo, “nyakati saba” za unabii zingekuja kukoma mwaka wa 1916, wakati wa Vita ya Ulimwengu. Lakini, kama ilivyoelezwa, sisi tunaamini kwamba kuna sababu yenye nguvu zaidi kuikubali habari iliyo katika Neno la Mungu lililoongozwa kwa roho yake, inayoonyesha mwanzo wa Majira ya Mataifa ulikuwa Oktoba mwaka wa 607 K.W.K. na yakamalizika katika Oktoba mwaka wa 1914 W.K.

30. Ni matukio gani yanayoungana kutambulisha kile kipindi cha tangu mwaka wa 1914 kuwa ndizo “siku za mwisho”?

30 Tunaweza kufurahi kwa vile zamani Mungu aliandikisha katika Neno lake matabiri yanayoonyesha waziwazi wakati wa kuja kwa Yesu akiwa Masihi katika mwaka wa 29 W.K., na pia “kuwapo” kwake akiwa Mfalme wa kimbingu tangu mwaka wa 1914 W.K. Wakati “umalizio wa mfumo wa mambo” unapoendelea kukoma, tunaona hali ambazo Yesu alituambia tuzitazame zikiongezeka pande zote kutuzunguka. Vile vita vya ulimwengu, njaa kuu, magonjwa ya kipuku, matetemeko ya ardhi, uhalifu, kukosa upendo, kuchukiwa na kuteswa kwa wale wanaofuata kanuni za Biblia—yote hayo kwa jumla yametutarnbulishia zile “siku za mwisho.”—2 Timotheo 3:1; Mathayo 24:3-12; Marko 13:7-13, NW.

ILE MILEANI (MIAKA ELFU)—LINI?

31. (a) Ni shauri gani ambalo Yesu anatolea wakati wetu, na kwa sababu gani? (b) Ni ulizo gani ambalo huenda tukaelekea kuuliza, na jibu la Yehova ni nini?

31 Hali hiyo yenye kuogopesha itaendelea kwa muda gani? Kwa kuwa sasa Kristo Yesu ametawazwa akiwa Mfalme-Shujaa-wa-Vita, kuna sababu nzuri ya kuamini kwamba haitachukua muda mrefu kabla hajatekeleza hukumu juu ya adui za Mungu. “Habari ya siku ale na saa ale hakuna aijuaye,” hivi kwamba hatupati faida kwa kukisia-kisia. Hata hivyo, imetupasa tutii shauri hili la Yesu: “Endeleeni kulinda.” (Marko 13:32, UV; Mathayo 24:42, NW) Tunapozitazama hali duniani zinazozidi kuwa mbaya na kuona jinsi watu kwa jumla wasivyoitikia habari njema za Ufalme, huenda tukaelekea kuuliza kama alivyouliza nabii wa Mungu kuhusu kazi yetu ya kuhubiri: “Ee [Yehova], hata lini?” Yehova anajibu:

“Hata miji itakapokuwa ukiwa, haina wenyeji, na nyumba zitakapokuwa hazina watu, na nchi hii itakapokuwa ganjo kabisa.” (Isaya 6:10-12)

Wakati wake uliowekwa ukifika, Yehova atatekeleza hukumu hiyo, kwanza juu ya Jumuiya ya Wakristo kisha juu ya sehemu nyingine zote za ulimwengu wa Shetani. Utawala wenye amani wa Kristo wa miaka 1,000 utafuata mara hiyo.—Ufunuo 20:1-3, 6.

“KIZAZI HIKI”—KIPI?

32. Ni ulizo gani linalotokea kulingana na Mathayo 24:34?

32 Katika unabii wake mkubwa juu ya ale “ishara,” Yesu anatuhakikishia hivi: “Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia.” (Mathayo 24:34) Kwa kuwa hataji wazi urefu wo wote wa wakati wa kizazi, tutafahamuje usemi huu “kizazi hiki”?

33. (a) “Kizazi” cha wakati wa Yesu kilikuwa nini? (b) Kulingana na hilo, ni nini linaloweza kusemwa juu ya kile “kizazi” cha miaka ya 1914-1918?

33 Katika siku za Yesu, baadhi ya wanafunzi wake waliosikia maneno yake, na wengine walioishi wakati huo pamoja nao, waliendelea kuishi kupita ile “dhiki” ya mwisho iliyoupata mfumo wa mambo wa Kiyahudi. Walikuwa ndicho kile “kizazi” cha wakati wa Yesu. Wakati wa kuandika kitabu hiki, katika United States pekee kuna watu zaidi ya 10,000,000 ambao bado wanaishi, waliokuwa wenye umri wa kutosha kutazama “mwanzo wa maumivu makali ya taabu” katika miaka ya 1914-1918. Baadhi ya hao huenda bado wakaendelea kuishi muda wa miaka kadha. Hata hivyo Yesu anatuhakikishia kwamba, kabla “kizazi hiki” hakijapita, atakuja akiwa “mwana wa mtu” ili atekeleze hukumu juu ya mfumo wa mambo wa Shetani. (Mathayo 24:8, 21, 37-39, NW) Imetupasa tuendelee kukesha, tutazamie ‘kuja kwa ufalme.’—Luka 21:31-36.

[Maelezo ya Chini]

a Word Pictures in the New Testament, Vol. I. uku. 188.

b Ona Nyongeza, ukurasa wa 186.

[Sanduku katika ukurasa wa 135]

KUHESABU ZILE “NYAKATI SABA”

“Nyakati” 7 = 7 x 360 = miaka 2,520

(“wakati” au mwaka wa Kibiblia ni muda ulio kati ya mwaka wa mwezi wenye siku 354 na mwaka wa jua wenye siku 3651/4)

607 K.W.K. kufika 1 K.W.K. = miaka 606

1 K.W.K. kufika 1 W.K. = mwaka 1

1 W.K. kufika 1914 W.K. = miaka 1,913

607 K.W.K. kufika 1914 W.K. = miaka 2,520

[Sanduku katika ukurasa wa 140]

“KIZAZI CHA MWAKA WA 1914”

Katika kitabu chenye jina hilo juu, Robert Wohl “anapendekeza kwamba vizazi havihesabiwi kwa kutaja miaka, lakini vinahesabiwa kwa kutegemea matukio makubwa, na vita ya ulimwengu ya kwanza ndio mfano ulio mkubwa zaidi wa matukio hayo.”—“The Economist,” Machi 15, 1980

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki