Mfalme wa Mbinguni Analeta Baraka Nyingi Duniani
41 Yehova alifanya Yesu awe Mfalme mbinguni.—Isaya 9:6; Danieli 7:13, 14; Matendo 2:32-36
42 Yeye atatawala dunia yote akiwa juu.—Danieli 7:14; Mathayo 28:18
43 Wewe unakumbuka ni jambo gani litapata wabaya?—Zaburi 37:9, 10; Luka 13:5
44 Unakumba jina la malaika wa kwanza kufanya dhambi? Yesu ataondoa huyo pamoja na wale malaika wengine wabaya. Sanamu zao na mifano yao ya ibada zitaharibiwa.—Waebrania 2:14; Ufunuo 20:2, 10
45 Yesu atafanya mambo mengi mema kwa ajili ya watu wenye kutii.—Waebrania 5:9
46 Hakuna mtu atakuwa mgonjwa tena.—Isaya 33:24; Ufunuo 22:1, 2
Wewe unakumbuka vile Yesu aliponesha wagonjwa?
47 Kila mtu atakuwa na vitu vizuri.—Isaya 65:17, 21-23
48 Mungu anakumbuka hata watu ambao wamekufa. Atatumia Yesu arudishie watu hao uzima. Tendo la kufanya hivyo linaitwa ufufuo.—Yohana 5:28, 29; 11:25
49 Wakati wabaya wote watakapokwisha kuuawa waondolewe kabisa, hakuna mtu atakufa tena. Hata wanyama wa mwituni hawatakuwa hatari. Kila mtu atakuwa na furaha milele.—Ufunuo 21:4; Isaya 65:25; Zaburi 37:11, 29