Inakupasa Kufanya Nini?
50 Je! wewe unataka kuishi milele katika hiyo paradiso nzuri?
Basi jifunze habari zaidi ambazo Mungu anasema. Jaribu kujua kusoma Biblia.—Yohana 17:3; Ufunuo 1:3
51 Jifunze habari zaidi juu ya Yesu.—Kumbukumbu la Torati 18:18, 19; Yohana 3:16; Matendo 3:19-23
52 Jaribu kufanya mambo mazuri tu na kutii Yehova.—Warumi 6:17, 18, 22
53 Kumbuka kwamba Yehova anasema tusiue watu hata kidogo.—Kutoka 20:13; 1 Yohana 3:11, 12
54 Haitupasi hata kidogo kuchukua mali za watu wengine.—Kutoka 20:15; Waefeso 4:28
55 Haipasi mwanamume kuishi na kulala pamoja na mwanamke ambaye si mke wake aliyemwoa kisheria.—Kutoka 20:14, 17; 1 Wathesalonike 4:3
56 Je! unakumbuka Mungu anampa mwanamume ruhusa ya kuwa na wanawake wangapi? Inapasa mwanamume kukaa na mke wake mpaka wakati gani?—Mwanzo 2:22, 24; Mathayo 19:5, 6; 1 Wakorintho 7:2, 10, 11
57 Kumbuka, pia, kwamba lazima tuabudu Yehova peke yake.—Mathayo 4:10; 1 Wakorintho 8:6
58 Sanamu na mifano ya ibada haziwezi kutusaidia. Kwa sababu gani?—1 Wakorintho 8:4
Je! ni vizuri kuwa na sanamu?—Kumbukumbu la Torati 27:15; 1 Yohana 5:21
59 Kwa sababu gani ni vibaya kuwa na hirizi na kuvaa mifupa na shanga ili kujikinga tusiumizwe?—Kumbukumbu la Torati 18:10-13; Ufunuo 21:8
60 Malaika wale wabaya au mashetani walikataa kutii Mungu. Wanatumia wabashiri (watu wanaotabiri wakati ujao kwa nguvu za mashetani) ili kupoteza wanadamu.—Matendo 16:16
61 Lazima tutolee Mungu sala. Sala ni kuzungumza na Mungu, kumwambia tunataka kumtumikia na kumwomba msaada.—Wafilipi 4:6, 7
62 Lazima sisi tutii Yesu na kumwamini.—Waebrania 5:9; Yohana 3:16
63 Kumbuka kwamba yeye alikufa ili kutuokoa sisi.—Warumi 5:8
64 Kumbuka kwamba Yesu ndiye Mfalme wetu ambaye haonekani kwa macho. Inatupasa kumtii.—Wafilipi 2:9-11; Ufunuo 19:16
65 Yesu alisema inakupasa wewe ueleze wengine mambo mazuri ambayo unajifunza na akasema wale wanaotaka kutumikia Mungu wanapaswa kubatizwa.—Mathayo 28:19, 20; Yohana 4:7-15
66 Kwa hiyo wewe unaweza kusema na rafiki zako juu ya mambo hayo mazuri.—Mathayo 10:32
67 Ukijifunza kusoma vizuri, utaweza kujifunza mambo mengine mengi na utaweza kusaidia wengine kwa njia nzuri zaidi.—2 Timotheo 2:15
68 Yesu alifundisha watoto wadogo pia kutii Mungu. Yeye hakukosa nafasi ya kusema nao.—Mathayo 19:13-15
69 Inapasa wazazi kufundisha watoto wao sikuzote kutii Mungu na kumpenda.—Kumbukumbu la Torati 6:6, 7; Mithali 6:20-22; Waefeso 6:4
70 Kuna makanisa mengi tofauti tofauti. Mengi ya mafundisho yao hayatoki katika Biblia. Yehova anatuambia sisi tuache dini ambazo hazifundishi ile kweli.—Ufunuo 18:4; Yohana 4:23, 24
71 Duniani Yehova ana watu ambao wanaweza kukufundisha habari zaidi juu yake. Wewe unajua watu hao?—Matendo 15:14; Warumi 10:14, 15
72 Wao ni Mashahidi wa Yehova. Wanaishi wakiwa na amani katikati yao. Unajua sababu? Sababu ni kwamba wanapendana.—Isaya 43:10-12; Yohana 13:34, 35
73 Kwa sababu wanapenda Yehova pia, wamebatizwa. Kwa njia hiyo wanaonyesha watu wote waziwazi kwamba wameacha njia yao mbaya ya maisha na wanataka kutumia maisha yao kumtumikia Mungu.—Matendo 2:41
74 Mashahidi wa Yehova wanatumaini kuishi katika paradiso mpya yenye kupendeza.—Zaburi 37:9-11, 29
Wewe unaweza kufanya nini ili uishi katika paradiso hiyo pamoja nao?—Yakobo 1:22, 25; 2:20-26
75 Jiunge nao kujifunza kutumikia Yehova. Wao wanapenda na kutii Yehova na Kristo Yesu. Je! wewe pia unapenda Yehova na Kristo Yesu? Je! ungependa kusaidia wengine wajue habari za Mungu?—Yohana 6:45-47
76 Yehova na Kristo Yesu wanakupenda wewe na wanataka uwe na maisha ya milele katika paradiso.—Yohana 3:16
Kwa uhakika mambo ambayo umejifunza kwa kuangalia picha na habari za kitabu hiki kidogo yamefanya utake kufurahia milele maisha duniani. Ikiwa ungependa kujifunza habari zaidi, sema na mmoja wa Mashahidi wa Yehova mahali unapoishi. Au, unaweza kuandika barua, au uambie mtu fulani akuandikie barua, uitume kwenye afisi ya nchi ya kwenu. Sanduku la posta limeonyeshwa katika ukurasa wa pilli wa kitabu hiki kidogo.