Je! Mungu Ataharibu Wabaya Tena?
22 Hata watu wa siku hizi ni wabaya sana. Ni mambo gani mabaya ambayo yanafanywa hapa?
23 Wengine wanaua wenzao. Mungu anasema usifanye hivyo hata kidogo.—Kutoka 20:13; 1 Yohana 3:11, 12
24 Wengine wanaiba. Mungu anasema usiibe hata kidogo.—Kutoka 20:15; Waefeso 4:28
25 Watu wengine wanaoa wanawake wengi. Wengine wanaishi pamoja na wanawake wawili au zaidi katika nyumba mbali mbali. Hata wanaume na wanawake wengine wanaishi pamoja bila kuoana kisheria. Mambo hayo yote hayapatani na maneno ya Biblia.—Mathayo 19:4-6; 1 Wakorintho 7:1-4; 1 Timotheo 3:1, 2
26 Je! wewe unakumbuka kwamba Mungu alimpa Adamu mke mmoja tu?—Mwanzo 2:22, 24
27 Wengine wanaabudu sanamu. Mungu anasema usitumie hata kidogo sanamu au mifano katika ibada.—Kutoka 20:4, 5; Isaya 44:9-17; 1 Yohana 5:21
28 Yehova ataharibu wabaya ambao hawageuki.—Zaburi 37:9, 10; Luka 13:5; 1 Wakorintho 6:9, 10