Mungu Anaharibu Ulimwengu Mbaya
18 Watoto ambao walizaliwa na Adamu waliongezeka wakawa wengi. Wao pia wakawa wabaya sana. Basi Mungu akaamua kuwaharibu.—Mwanzo 6:1, 5, 7
19 Lakini alikuwako mwanamume mmoja mzuri jina lake Noa.—Mwanzo 6:8, 9
Yehova Mungu alimwambia ajenge meli kubwa sana ambayo yeye na jamaa yake wangeokolewa wakiwa ndani wakati watu wabaya wangekuwa wakiharibiwa. Meli hiyo ilikuwa kama sanduku kubwa. Iliitwa safina.—Mwanzo 6:13, 14
20 Waliingiza wanyama wengi ndani ya safina.—Mwanzo 6:19-21
21 Yehova alinyesha mvua kubwa sana. Wabaya wote walikufa. Wale waliokuwa ndani ya safina waliokolewa. Wewe unajua sababu?—Mwanzo 6:17; 7:11, 12, 21; 1 Petro 3:10-12