Kifo ni Nini?
15 Wakati mwanadamu anapokufa, anarudi katika mavumbi. Sasa anakuwa hajui jambo lo lote tena.—Zaburi 146:4
Watu waliokufa hawawezi kusema na wewe na hawawezi kufanya jambo lo lote.—Mhubiri 9:5, 10
16 Lakini malaika wengi waligeuka wakawa wabaya. Sasa wanajifanya kwamba wao ndio watu ambao wamekufa. Wanataka tuamini kwamba tunapokufa tunaendelea kuishi.—Mwanzo 6:1, 2; Yuda 6
17 Kwa hiyo Yehova Mungu hataki sisi tuamini maneno ya malaika hao wabaya, wanaoitwa mashetani.—Kutoka 22:18; Kumbukumbu la Torati 18:10, 11; 32:17
Yeye hataki tuendee wachawi, tufanye mambo ya ulogi na kuvaa hirizi. —Wagalatia 5:19-21